31 Agosti 2025 - 08:45
Source: Parstoday
Yemen yawaonya Wazayuni: Siku za giza zinakuwajihini, hamtaonja tena ladha ya usalama

Rais wa Yemen ameuonya utawala wa Israel kuhusu uhakika wa serikali ya Sana'a kulipiza kisasi cha mauaji ya hivi karibuni yaliyofanywa na Tel Aviv dhidi ya waziri mkuu wa taifa hilo la Peninsula ya Kiarabu, pamoja na maafisa wengine wanane.

"Kisasi chetu hakilali, na siku za giza zinakungojeeni. Hutaonja usalama baada ya leo," Mahdi al-Mashat, Rais wa Yemen alitoa indhari hiyo katika hotuba yake ya jana Jumamosi.

Ameeleza bayana kuwa, "Damu ya Mashahidi hawa wakuu itakuwa chachu na motisha zaidi kwa ajili ya kusimama kidete, kuwa na uthabiti, ustahimilivu, na kujitolea,"  akiahidi kwamba taifa hilo litaendelea kuimarisha vikosi vya jeshi lake.

"Hutaweza kuvunja uthabiti wetu kwa sababu tuko pamoja na Allah. Heshima yetu kutoka kwa Mwenyezi Mungu ni kufa shahidi, na ahadi Yake ya uhakika kwetu ni ushindi usioepukika," afisa huyo amesisitiza. Rais wa Yemen ameongeza kuwa, mashahidi hao wa Yemen wamelipa gharama ya kusimama dhidi ya “maadui wakubwa zaidi wa Mwenyezi Mungu, yaani Wazayuni watenda jinai.”

Matamshi hayo yametolewa baada ya mashambulizi ya anga ya Israel katika mji mkuu wa Yemen kupelekea kuuawa shahidi Waziri Mkuu wa wa Serikali ya Kitaifa ya Mabadiliko na Ujenzi ya nchi hiyo, Ahmed Ghaleb Al-Rahawi na maafisa wengine walokuwa wakihudumu katika nyadhifa mbalimbali.

Yemen yawaonya Wazayuni: Siku za giza zinakuwajihini, hamtaonja tena ladha ya usalama

Mashambulizi hayo yametokea huku utawala wa Kizayuni wa Israel ukishadidiisha hujuma zake za kinyama dhidi ya nchi hiyo maskini ya Kiarabu.

Mashambulizi hayo yalianza baada ya wanajeshi wa Yemen kuanza kufanya operesheni za karibu kila siku dhidi ya shabaha nyeti za Israel, ili kukabiliana na vita vya mauaji ya halaiki ambavyo Tel Aviv ilianzisha dhidi ya Ukanda wa Gaza mnamo Oktoba 2023.

Your Comment

You are replying to: .
captcha