1 Septemba 2025 - 08:50
Source: Parstoday
Mwanaharakati Greta Thunberg: Hatuwezi kupata haki ikiwa tutaitenga Gaza

Mwanaharakati wa masuala ya hali ya hewa wa Uswidi, Greta Thunberg, ameikosoa jamii ya kimataifa kwa kushindwa kukomesha mauaji ya kimbari yanayoendelea huko Gaza, akionya kuwa haki haiwezi kupatikana huku masaibu ya Wapalestina yakipuuzwa.

Bi Thunberg amesisitiza katika mahojiano aliyofanyiwa na Novara Media  kwamba uanaharakati wake wa masuala ya hali ya hewa hauzuii kipaumbele anachotoa kwa Gaza na kwa Palestina.

Amesema, ikiwa unajali sayari ambapo binadamu wanaweza kuishi unapasa pia kuwajali binadamu. "Mimi si mwanaharakati wa masuala ya hali ya hewa kwa sababu tu nataka kuhudumia miti au chura," amesema Greta Thunberg. 

Ameeleza kuwa utetezi wake wa haki za Wapalestina unatokana na yeye kuwa binadamu,  "kuwa na hisia hai" na "maadili ya msingi."

Kesho Jumapili mwanaharakati huyo wa masuala ya hali ya hewa wa Sweden, Greta Thunberg atasafiri kwa meli hadi Gaza akitokea Barcelona katika msafara wa Global Sumud Flotilla, ambapo wataungana na maelfu ya wanaharakati katika misheni kubwa zaidi ya baharini kuwahi kuratibiwa kwa lengo la kuvunja mzingiro wa Israel dhidi ya watu wa Gaza.

Thunberg amesema kuwa kampeni hiyo ni sehemu ya mwamko wa kimataifa wa watu kutoka maeneo mbalimbali duniani wanaojaribu kuvunja mzingiro wa kikatili wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza. 

342/

Your Comment

You are replying to: .
captcha