23 Julai 2026 - 08:37
Source: ABNA
Tunaonya: Msitumie njia mbadala za Mlango wa Hormuz

Kamandi ya Jeshi la Wanamaji la Pasdaran imechapisha ujumbe ukisema: Njia mbadala si salama na ni hatari; tunaonya zisitumike kwani zitakuwa na matokeo mabaya na yasiyoweza kurekebishwa.

Kwa mujibu wa shirika la habari la Abna, Kamandi ya Jeshi la Wanamaji la IRGC imechapisha katika mtandao mmoja wa kijamii ujumbe ukisema: Kuingia na kutoka kwa Mlango wa Hormuz kumewekwa wazi na iko chini ya udhibiti wetu kamili.

Katika muendelezo wa ujumbe huu imesemwa: Njia mbadala si salama na ni hatari; tunaonya zisitumike kwani zitakuwa na matokeo mabaya na yasiyoweza kurekebishwa.

Maoni yako

You are replying to: .
captcha