22 Novemba 2014 - 19:17
Mawaziri wa Ujerumani,Iran na Marekani wakutana Vienna kujadili kadhia ya nyuklia

Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier anakutana na mawaziri wenzake wa Iran na Marekani Mohamed Javad Zarif na John Kerry leo mjini Vienna, kujaribu kuondoa vizingiti vya mwisho katika kufikiwa makubaliano juu ya mpango wa nyuklia wa Iran.

   Waziri wa mambo  ya nchi za nje wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier anakutana na  mawaziri wenzake wa Iran na Marekani Mohamed Javad Zarif na John Kerry  leo mjini Vienna, kujaribu kuondoa vizingiti vya mwisho katika kufikiwa makubaliano juu ya mpango wa nyuklia wa Iran.

Jamhuri ya kiislamu ya Iran inajadiliana na Uingereza, China, Ufaransa, Urusi , Marekani na Ujerumani kwa lengo la  kufikia makubaliano ya kadhia ya nyuklia kabla ya kufika muda wa mwisho wa majadiliano uliowekwa  ambao ni Jumatatu ijayo, majadiliano haya yakifanikiwa yata maliza  kutengwa kwa Jamhuri ya kiislamu ya Iran kimataifa na kuondolewa kwa vikwazo. Jamhuri ya kiislamu ya  Iran kwa upande wake inatakiwa kupunguza  kwa kiwango kikubwa  shughuli zake za kinyuklia.Steinmeier  amesema kwamba  mazungumzo kati ya  Iran na madola hayo sita   yako wazi na kwamba licha ya  tafauti ziliopo pande hizo zimekaribiana zaidi kuliko ilivyokuwa kwa kipindi cha miaka 10 iliopita.Pindi makubaliano hayo yatafikiwa, yatamaliza  mgogoro juu ya mpango huo wa nyuklia wa Iran uliodumu kwa miaka  12.

Yafaa kuashiria kwamba Jamhuri ya kiislamu ya Iran bado inashikilia msimamo wake kwamba haina lengo la kutengeneza makombora ya nyuklia.

Tags