Nyuklia
-
Tathmini ya Mashirika 8 ya Kijasusi ya Marekani Kuhusu Kushindwa kwa Trump Katika Kuishambulia Iran
Tathmini nyingi kutoka ndani ya vyombo vya usalama vya Marekani zinaonyesha kuwa Iran bado ina uwezo wa kuendeleza mpango wake wa nyuklia. Badala ya kuuzuia, mashambulizi ya Marekani huenda yameifanya Iran kuwa na msimamo mkali zaidi na kufikiria kuujenga kwa matumizi ya kijeshi.
-
Mchambuzi wa Kiyahudi: "Kwa Nini Tumeshindwa Vita na Iran Imeshinda Vita?"
Mchambuzi huyu wa Kiyahudi, Goldberg alisisitiza zaidi kuwa Makombora ya Iran yalilenga kwa usahihi mno Shabaha zake, na yameibuka kwa heshima kubwa kimataifa. Badala ya kusambaratika, Iran imeonekana kuwa Taifa thabiti na lenye msimamo wa kupambana na uonevu wa yeyote.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran:
"Kila afisa wa Kijeshi au Mwanasayansi wa Nyuklia wa Iran anayeuliwa Kigaidi, kuna wengine mia moja nyuma yake walioko tayari kuchukua nafasi yake"
Abbas Araqchi alisema: "Tofauti na utawala wa Kizayuni, Iran haitaficha kamwe hasara zake na inajivunia Mashahidi wake kama vielelezo vya ujasiri. Taifa la Iran litasimama kidete dhidi ya yeyote anayejaribu kuliamulia mustakabali wake hadi tone la mwisho la damu".
-
CNN: "Kwa nini TRUMP analazimisha Dunia iamini kuwa aliharibu vituo vya Nyuklia vya Iran?! Kuna Lengo lipi nyuma ya Uongo wake?!"
Uongo wa Trump ni Taktiki inayojulikana kama: "uongo ukirudiwa mara nyingi huanza kuaminika," ambayo inakusudia kuathiri mtazamo wa umma na hata maamuzi ya kimataifa.
-
Utafiti unaonyesha kuwa maeneo ya nyuklia ya Iran yaliyoshambuliwa na Marekani bado yanafanya kazi kama kawaida - Iran iliwahadaa na kutoa kila kitu
"centrifuges" (au kwa kiswahili: Visukuma ambavyo hutumika katika teknolojia ya nyuklia) zote ziko salama, na ambazo hutumiwa kimsingi kwa urutubishaji wa uranium, mchakato ambao hutenganisha isotopu za uranium ili kuongeza mkusanyiko wa U-235, ambayo huhitajika kwa vinu vya nyuklia.
-
Hasira ya Lieberman kwa kushindwa kwa Israel kufikia malengo yake maovu
Hili la kusitisha mapigano ni la aibu, si mpango wa makombora wa Iran umeharibiwa wala mpango wao wa nyuklia, huu ni usitishaji mapigano usio na masharti, Iran itarutubisha Uranium (ya Nyuklia) tena.
-
"Kinga ya Dhahabu" ya Trump: Ulinzi wa Kweli au Mbinu ya Vita vya Kisaikolojia?!
Mpango huu wa Trump unafanana sana na mpango wa miaka ya 1980 wa Rais wa zamani Ronald Reagan ulioitwa "Mpango wa Ulinzi wa Kimkakati" (Strategic Defense Initiative), uliolenga kuzuia makombora ya nyuklia ya Urusi kwa kutumia satelaiti na leza — lakini haukuwahi kutekelezwa kutokana na gharama kubwa, ugumu wa kiufundi, na upinzani wa ndani na kimataifa.
-
Raundi mpya ya mazungumzo kati ya Iran na Marekani itafanyika Ijumaa hii Mjini Rome, Italia
Raundi ya tano ya mazungumzo kati ya Iran na Marekani inatarajiwa kufanyika siku ya Ijumaa mjini Rome, Italia. Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ametangaza kuwa nchi yake imekubali pendekezo la Oman kwa ajili ya kikao hiki. Aidha, alisisitiza kuwa ujumbe wa Iran katika mazungumzo haya umejikita katika kulinda haki za taifa hilo na kuhakikisha kuondolewa kwa vikwazo vilivyowekwa dhidi ya Iran.
-
Araghchi: "Kiongozi Mkuu ameweka wazi wajibu wa Iran kuhusu urani na kwamba suala la urutubishaji wa Urani (uranium enrichment) halipo mezani
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqhchi, alizungumza kuhusu msimamo wa Marekani katika mazungumzo ya nyuklia na kusisitiza kwamba suala la urutubishaji wa urani (uranium enrichment) halipo kabisa katika meza ya majadiliano. Alisema kuwa urutubishaji si jambo ambalo linapaswa kujadiliwa, kwani haki ya Iran ya kuendeleza mpango wake wa nyuklia ni jambo la msingi na lililowekwa wazi. Aidha, aliongeza kuwa: Kiongozi Mkuu alisema wazi kuhusu hili katika majadiliano yaliyopita na hakubali kuona suala hili likiingizwa tena katika mchakato wa majadiliano.
-
Kauli ya Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu wa Iran:
"Wamarekani waache kupayuka; Iran haitasubiri ruhusa ya mtu yeyote ili kuendeleza shughuli zake za kurutubisha urani"
Kiongozi wa Mapinduzi alipozungumzia mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja na Wamarekani, alisisitiza kuwa: Kauli ya Wamarekani kwamba 'hawataruhusu Iran irutubishe urani' ni upuuzi mtupu. Hakuna mtu yeyote nchini anayesubiri ruhusa ya huyu au yule. Jamhuri ya Kiislamu itaendelea kufuata sera na njia yake kama kawaida.
-
Raundi ya Nne ya Mazungumzo kati ya Iran na Marekani Kufanyika Jumatano, Mei 7, 2025
Kwa mujibu wa Mwandishi wa Wall Street Journal, muda unaotarajiwa kwa ajili ya mazungumzo yajayo ni tarehe 7 Mei, 2025 (Siku ya Jumatano).