Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Likinukuu tathmini ya awali ya kijasusi iliyofanywa na Shirika la Ujasusi la Marekani (DIA), shirika la habari la Marekani CNN liliripoti kuwa vituo vyote vitatu vya nyuklia vya Iran (Fordo, Isfahan, na Natanz) ambavyo vililengwa na mashambulizi ya Marekani bado vinafanya kazi kikamilifu.
Ripoti hii inasema: "Uranium iliyorutubishwa haiharibiwi hata kidogo. "centrifuges" (au kwa kiswahili: Visukuma ambavyo hutumika katika teknolojia ya nyuklia) zote ziko salama, na ambazo hutumiwa kimsingi kwa urutubishaji wa uranium, mchakato ambao hutenganisha isotopu za uranium ili kuongeza mkusanyiko wa U-235, ambayo huhitajika kwa vinu vya nyuklia. Maeneo (saiti) ya siri yote hayajaguswa na moto wowote hata kidogo na yako salama".
Your Comment