25 Novemba 2014 - 19:44
Urusi yatoa onyo kali kwa Ufaransa

Serikali ya Urus imetoa onyo kali kwa Ufaransa kutokana na kuzuiliwa meli zake za kijeshi.

Serikali ya Urus imetoa onyo kali kwa Ufaransa kutokana na kuzuiliwa meli zake za kijeshi.

  Waziri  wa  mambo  ya  kigeni  wa  Ufaransa  Laurent fabius amesema  leo  kuwa  mazingira  kwa sasa si sahihi kuipatia  Urusi  meli  ya  kivita  kutokana  na  mzozo  wa Ukraine, wakati  mbinyo  unaongezeka  kutoka  Urusi  kwa Ufaransa  kukabidhi  meli  hiyo.

  Serikali ya Urusi  imesisitiza na kuionya  Ufaransa  kuwa  inakabiliwa  na matokeo  mabaya  hadi  pale  Ufaransa  itakapokabidhi meli  hiyo  ya  kwanza  miongoni  mwa  meli  mbili  za kubebea  helikopta  za  kijeshi  zilizotakiwa  kukabidhiwa ifikapo  mwishoni  mwa  mwezi  huu.

Lakini  kutokana  na  mzozo  wa  Ukraine  uliozuka  katikati ya  mwaka  huu,   Fabius  amesema , nchi  yake  imekuwa katika  mbinyo  mkubwa  kutoka  kwa  washirika  wake , hususan  Marekani , na  imeahirisha  hatua  ya  kuikabidhi Urusi  meli  hiyo  mwezi  Septemba mwaka huu.

Tags