25 Desemba 2014 - 19:18
Serikali ya Urusi yaelezea wasiwasi wake kuhusu madhara ya Ukraine kujiunga na NATO

Waziri wa mambo ya kigeni wa Urusi, Sergei Lavrov, amesema hatua ya Ukraine kutaka kujiunga na Shirika la Kujihami la Mataifa ya Magharibi NATO inaleta kitisho kwa usalama wa Ulaya

Waziri  wa  mambo  ya  kigeni  wa  Urusi, Sergei Lavrov, amesema  hatua  ya  Ukraine  kutaka  kujiunga  na  Shirika  la  Kujihami  la Mataifa  ya  Magharibi  NATO  inaleta  kitisho  kwa  usalama  wa Ulaya na  kwamba  mataifa  ya  Magharibi  yanatumia  juhudi  hizo kama  njia  ya   kuzichonganisha Urusi  na  Ukraine.

Hatua  ya  bunge  la  Ukraine  kujitoa kwenye Jumuiya ya Mataifa Yasiyofungamana na Upande Wowote kama  hatua  ya  kujiunga  na NATO imeikasirisha  Urusi  na  kuongeza  mvutano  kati  ya  Urusi na  mataifa  ya  magharibi  tangu  kumalizika  kwa  vita  baridi.

Lavrov  ni  kiongozi wa juu wa Urusi  wa  hivi  karibuni  kabisa kuzungumzia  dhidi  ya  juhudi  za  Ukraine, na  ambaye  ameweka wazi  kwamba  Urusi  utauona  uanachama  wa   nchi  hiyo  kwa NATO  kuwa  mkakati  wa  jimbo  hilo  la  zamani  la  iliyokuwa  umoja wa  Kisovieti  kuwa  ni  kitisho  cha  moja  kwa  moja  kijeshi.

 

Tags