12 Januari 2015 - 17:48
Iran yataka Urusi kuchukua nafasi ya juu katika mazungumzo ya nyuklia

Waziri wa mambo ya kigeni wa jamhuri ya kiislamu ya Iran Mohammad Javad Zarif amesema leo kwamba kuhusika zaidi kwa Urusi kunaweza kuharakisha mazungumzo yenye lengo la kufikia makubaliano muhimu juu ya mzozo unaohusisha mpango wake wa kinyuklia.

Waziri wa mambo ya kigeni  wa jamhuri ya kiislamu ya  Iran Mohammad Javad  Zarif amesema  leo  kwamba kuhusika  zaidi  kwa Urusi kunaweza kuharakisha  mazungumzo  yenye  lengo  la  kufikia  makubaliano muhimu  juu  ya  mzozo unaohusisha mpango wake wa kinyuklia.

Wakati   mkutano  kati  ya  jamhuri ya kiislamu ya  Iran  na  mataifa  yenye  nguvu  duniani ukianza  tena  mjini  Geneva  siku  ya  Jumatano, naibu waziri  wa mambo  ya  kigeni  wa  Urusi  Sergei Ryabkov alikuwa  akifanya ziara  nchini  Urusi, ambapo  pande  zote  mbili zimeeleza  nia  yake ya  kutaka  kufikiwa  makubaliano.

Wakati suala kuu ni kufikiwa makubaliano ya mwisho kabla ya muda wa mwisho wa Juni 30, mazungumzo hayo yamekwama kuhusiana na masuala muhimu.

Ryabkov , ambaye  anaongoza  ujumbe  wa  majadiliano  wa  Urusi chini  ya  mazungumzo  ya  mataifa  matano  pamoja  na  Ujerumani , amesema  mahusiano  mzuri  kati  ya  jamhuri ya kiislamu ya  Iran  na  Urusi  unaweza kusaidia  kufikiwa  haraka  kwa  makubaliano  ya  kinyuklia  na Iran.

 

Tags