Mfalme wa Saudi arabia Abdullah amefariki dunia mapema leo Ijumaa akiwa na umri wa miaka 91 na mdogo wake Salman atakuwa mfalme, ufalme wa nchi hiyo umeeleza katika taarifa.
Mfalme Salman amemteua ndugu yake wa baba mmoja Mugrin kuwa mwanamfalme na mfalme mtarajiwa, akichukua hatua ya haraka kuondoa hofu ya mzozo wa kurithi madaraka katika wakati huu ambapo Saudi Arabia inakabiliwa na hali ya mtafaruku katika mipaka yake.
Kuzuka kwa kundi la kigaidi la Daesh nchini Syria na Iraq kumesogeza katika mipaka ya nchi hiyo ya Kifalme kundi la wanamgambo ambao wameapa kuuangusha utawala wa kifalme wa Al Saudi.