3 Machi 2015 - 20:24
Iran yakataa mapendekezo ya Obama

Jamhuri ya kiislamu ya Iran leo imetupilia mbali na kulipinga vikali pendekezo la rais Barack Obama kwamba nchi hiyo isitishe shughuli zake amani za kinyuklia kwa takriban miaka kumi,

Jamhuri ya kiislamu ya Iran leo imetupilia  mbali  na kulipinga vikali pendekezo la rais Barack Obama  kwamba nchi  hiyo  isitishe  shughuli  zake  amani za  kinyuklia  kwa  takriban miaka  kumi, na  kusema  hilo  halikubaliki. Msimamo  wa  Obama unaelezwa  katika maelezo  yasiyokubalika  na  ya  kitisho, na  Iran haitakubali madai  ya  kuvuka mipaka  na  yasiyo  na  mantiki. 

Hata  hivyo  waziri  wa  mambo  ya  kigeni  wa  Iran  Mohammad Javad Zarif  amenukuliwa  akisema  kwamba  nchi  hiyo  itaendelea na majadiliano  ya  kinyuklia na  mataifa  yenye  nguvu duniani.

Katika  mahojiano  na  shirika  la  habari  la  Reuters  jana Jumatatu, Obama  alisema  Iran inapaswa  kukubali  kusitisha shughuli  zake za  kinyuklia  kwa  muda  ambao  unaweza  kufanyika  uchunguzi  wa kina  kuhusu  shughuli  zake ili  makubaliano  yafikiwe kati  yake  na mataifa  hayo  yenye  nguvu.

Serikali ya Marekani inaona kwamba nguvu za kijeshi za Iran, ni kikwazo kikubwa kwa Israel na kwamba zinahatarisha amani na usalama wa Israel.