Uamuzi wa Israel wa kuzuwia kiasi cha dola milioni 130 kwa mwezi katika mapato yaliyokusanywa kwa niaba ya mamlaka ya Palestina yanaubana uchumi wa nchi hiyo na kusababisha mfumo wa benki kutokuwa na fedha.
Gavana wa benki kuu ya Palestina amesema kwamba Israel imesitisha upelekaji wa fedha hizo za kodi na ushuru mwezi Januari ikipinga hatua ya Palestina kujiunga na mahakama ya kimataifa ya uhalifu ifikapo Aprili mosi, wakati mashtaka ya uhalifu wa kivita yatakapofikishwa dhidi ya Israel, ambapo Israel iliivamia kijeshi Palestina na kufanya mauaji ya kinyama kwa muda wa siku 50 mutawaliya, watu wengi wasio na hatia waliuawa ambapo wengi wao ni wanawake na watoto mpaka sasa wengi wa wakazi wa palestina hawana sehem za kuishi wanaisi kwenye mapango na magofu.
Tangu wakati huo zaidi ya dola milioni 500 zimezuiwa na Israel , kuingia katika uchumi wa Palestina , na kusababisha mamlaka ya Palestina , ambayo inatawala ukingo wa magharibi , kupunguza mishahara ya wafanyakazi wake kwa asilimia 40 na kuanza kutumia bajeti ya dharura.