Eid al-Adha ni zaidi ya kusherehekea; ni ishara ya kujisalimisha kwa Mwenyezi Mungu kwa moyo wote, kujenga jamii ya huruma na mshikamano, na kuhuisha roho ya kujitolea. Ni nafasi ya kila Mwislamu kujiangalia upya na kuimarisha uhusiano wake na Muumba na viumbe wenzake.
Ayatullah Ali Khamenei amesema kuwa Ulimwengu wa Kiislamu kwa sasa unayahitaji zaidi kuliko wakati mwingine wowote mafundisho ya Hija, na akibainisha kuwa Hija ya mwaka huu ni msimu wa pili unaofanyika sambamba na jinai za utawala wa Kizayuni huko Gaza, ameuliza swali lifuatalo:“Ni nani anapaswa kusimama dhidi ya janga hili la kibinadamu?” Kisha ameongeza kwa kusisitiza:
“Bila shaka yoyote, serikali za Kiislamu ndizo zinazobeba wajibu wa kwanza wa jukumu hili, na mataifa ya Kiislamu yana haki ya kudai utekelezaji wa wajibu huo kutoka kwa serikali zao.”