Umoja wa Mataifa ulitangaza Jumatatu iliyopita kwamba unapanga kupunguza idadi ya wafanyikazi wake huko Gaza kufuatia duru mpya ya mashambulio ya Israel.
Umoja wa Mataifa una wafanyakazi zaidi ya 13,000 katika Ukanda wa Gaza, wengi wao wakiwa Wapalestina, wanaofanya kazi muhimu kama vile madaktari, wauguzi, madereva na kazi nyingine.
Zaidi ya wafanyakazi 250 wa UN wameuawa na Israel katika kipindi cha miezi 15 iliyopita.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, anasema hali imekuwa ya hatari kiasi kwamba anapanga kupunguza wafanyakazi wa kimataifa wanaofanya kazi Gaza kwa takriban theluthi moja, kwa msingi huo, wafanyakazi karibu 30 wa UN wataondoka Gaza kwa kuhofia usalama wao.
Msemaji wa Umoja wa Mataifa, Stephane Dujarric amewaambia waandishi wa habari huko New York siku kwamba: "Wiki iliyopita, Israel ilifanya mashambulizi makubwa huko Gaza na kuua mamia ya raia, ikiwa ni pamoja na wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa, na pia imezuia misaada ya kibinadamu kuingia eneo hilo tangu mapema mwezi huu wa Machi."
Afisa huyo wa wa ngazi za juu wa Umoja wa Mataifa amesema: "Katibu Mkuu wa UN analaani vikali mashambulizi haya na anatoa wito wa kufanyika uchunguzi kamili na huru kuhusu tukio hilo."
342/
Your Comment