Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Tangazo maalum: Kanisa la Glory Outreach Assembly Tanzania - Linayo furaha kubwa kuwalika katika: Ibada kuu na sherehe za kuwekwa wakfu askofu wa makanisa ya Glory Outreach Assembly Tanzania. Tukio hili la kipekee litafanyika:
Tarehe: Jumapili, 27 Julai 2025.
Muda: Kuanzia saa 3:00 asubuhi
Mahali: Mji Mdogo wa Lamadi, Wilaya ya Busega, Mkoa wa Simiyu, Tanzania.
Sherehe hii takatifu itaambatana na:
1_Ibada ya kuwekwa wakfu.
2_Huduma ya Neno la Mungu.
3_Nyimbo za sifa na kuabudu.
4_Wageni maalum kutoka ndani na nje ya nchi.
5_Chakula cha pamoja.
Tunawaalika watu wote — viongozi wa dini, waumini, familia, marafiki, na wapenda kazi ya Mungu — kufika na kushiriki tukio hili la kihistoria katika mwili wa Kristo.
“Mtu akitamani kazi ya askofu, atamani kazi njema.”
1 Timotheo 3:1
Karibu tusherehekee pamoja kwa utukufu wa Mungu!
Kwa mawasiliano na taarifa zaidi:
📞 [+255 624 468 558]
Your Comment