Kwa taarifa ya Shirika la Habari la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Ali Larijani Jumatatu asubuhi tarehe 11 Agosti, kabla ya kuanza safari yake kwenda Iraq na Lebanon, alisema:
Safari hii ina sehemu mbili, sehemu ya kwanza ni Iraq. Iraq ni nchi rafiki na jirani yetu na tuna uhusiano mzuri wa biashara. Ushirikiano wa mataifa haya mawili uko katika kiwango kizuri sana, mfano wake ni maadhimisho ya Arbaeen ambapo tunashukuru serikali ya Iraq kwa ushirikiano mzuri kwa mazuwaru.
Katibu wa Baraza la Usalama la Kitaifa aliongeza:
“Tumeandaa mkataba wa usalama na Iraq ambao ni jambo muhimu sana; mtazamo wa Iran katika uhusiano na majirani ni kwamba usalama wa Wairani ni msingi lakini pia tunazingatia usalama wa majirani zetu, si kama baadhi ya nchi ambazo zinafikiri usalama wao tu, na kupuuza au kuonea mataifa mengine katika mkoa.”
Aliongeza:
“Katika safari hii mkataba utaasainiwa, na tutakutana na viongozi mbalimbali wa Iraq kutoka pande tofauti, kusikiliza mawazo yao na kujadili ushirikiano wa pande zote mbili.”
Larijani alitangaza Lebanon kama nchi ya pili katika safari hii na kusema:
“Lebanon ni moja ya nchi muhimu sana katika mkoa na yenye ushawishi mkubwa katika Asia Magharibi. Tumekuwa na uhusiano wa muda mrefu na watu na serikali ya Lebanon. Wataalamu wengi na wanasayansi wenye ushawishi nchini Iran wamekuja kutoka Lebanon, na hivyo tunashiriki urithi wa tamaduni. Ushirikiano wetu na serikali na watu wa Lebanon ni wa muda mrefu na pana, na tunapiga mazungumzo kuhusu masuala mbalimbali ya mkoa.”
Katibu wa Baraza la Usalama la Kitaifa alipoulizwa kuhusu msimamo wa Iran katika safari hii alisema:
“Katika Lebanon, msimamo wetu umekuwa wazi; tunasisitiza kuwa umoja wa kitaifa wa Lebanon ni jambo muhimu na lazima udumishwe katika hali zote. Uhuru wa Lebanon umekuwa muhimu kwetu, na tunatilia mkazo kuimarisha uhusiano wa kibiashara kati ya nchi zetu pia.”
LariJani aliongeza kuhusu hali nyeti ya Lebanon hivi sasa:
“Lebanon ina historia ndefu ya changamoto, na hivi karibuni imekuwa na mizozo mikubwa na utawala wa Kizayuni. Kama sisi tulivyokuwa na migogoro na utawala wa Kizayuni, hivyo mazungumzo haya yanaweza kusaidia katika kuleta utulivu mkoani.”
Your Comment