Kwa mujibu wa shirika la habari la ABNA likinukuu Russia Al-Youm, tovuti ya Kizayuni ya Walla iliripoti kuwa kundi maarufu la wadukuzi la Handala lilichapisha ujumbe wenye kichwa cha habari "Siku ya hesabu inawangoja wauaji wa watoto".
Katika ujumbe huo uliolenga wakazi wa maeneo yanayokaliwa kwa mabavu, imeelezwa kuwa, ni lazima ieleweke kwamba njia pekee ya kufikia amani ya kudumu na ya haki ni kufanya uchaguzi huru kwa ushiriki wa wakazi wote wa Ardhi Takatifu kuanzia Waislamu, Wayahudi na Wakristo bila uwepo wa makundi yenye msimamo mkali na wauaji wa watoto. "Siku ya Hanukkah inapokaribia, tunataka kujua ni habari za afisa gani wa Kizayuni mna hamu ya kuzipata."
Handala pia ilitaja majina ya Itamar Ben-Gvir, Waziri wa Usalama wa Taifa, Benny Gantz, waziri wa zamani, Tally Gotliv, mbunge wa Knesset, na Yoav Gallant, waziri wa zamani wa ulinzi.
Your Comment