Kwa mujibu wa nyaraka zilizovujishwa na "Quds News Network", ushirikiano kati ya idara ya usalama ya Imarati na Mossad unahusisha operesheni za kijasusi ndani ya Gaza na Qatar chini ya maelekezo ya moja kwa moja ya Benjamin Netanyahu. Nyaraka hizo zinaeleza kuwa amri za Israel zilikuwa za "kudhalilisha" na ziliitaka Imarati kuongeza idadi ya maafisa wake nchini Qatar mara tano zaidi ndani ya mwezi mmoja. Maafisa wa Imarati wameonyesha wasiwasi wao kuhusu lugha hiyo ya kiburi ambayo haionyeshi ushirikiano wa usawa.
Nyaraka za siri zinaonyesha kuwa Imarati imekuwa ikishirikiana na Israel katika kuifanyia ujasusi Gaza na Qatar, huku amri za Waziri Mkuu wa Israel zikiwasilishwa kwa upande wa Imarati kwa lugha ya dharau.
Your Comment