6 Julai 2026 - 21:11
Hawza ya Hazrat Zainab (as) Kigamboni Yaandaa Khatmu ya Qur'an Tukufu kwa Ajili ya Shahidi Sayyid Ali Khamenei na Mashahidi wote wa Vita vya Ramadhan

Wanafunzi wa Hawza ya Hazrat Zainab (as) Kigamboni, wameshiriki katika Khatmu ya Qur'an Tukufu kwa ajili ya kuwaombea Mashahidi wa vita vya Ramadhan, akiwemo Ayatollah Sayyid Ali Hussein Khamenei.

Kwa Mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (AS) –ABNA– Hawza ya Wasichana ya Hazrat Zainab (as) iliyopo Kigamboni, Dar es Salaam, imeandaa kikao maalumu cha khatmu ya Qur'an Tukufu kwa ajili ya kuwaombea Mashahidi wa Vita vya Ramadhan, akiwemo Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran, Ayatollah Sayyid Ali Hussein Khamenei.
 

Hawza ya Hazrat Zainab (as) Kigamboni Yaandaa Khatmu ya Qur'an Tukufu kwa Ajili ya Shahidi Sayyid Ali Khamenei na Mashahidi wote wa Vita vya Ramadhan


Kikao hicho kilifanyika Jumatatu, tarehe 6 Julai 2026 (20 Muharram 1447 H), kwa ushiriki wa wanafunzi 144 wa Hawza hiyo pamoja na wasimamizi wao, Washiriki (hao) walisoma Qur'an Tukufu na kumuomba Mwenyezi Mungu Awajaalie Mashahidi hao rehema, msamaha na daraja ya juu Peponi.

Hawza ya Hazrat Zainab (as) Kigamboni Yaandaa Khatmu ya Qur'an Tukufu kwa Ajili ya Shahidi Sayyid Ali Khamenei na Mashahidi wote wa Vita vya Ramadhan


Waandaaji wa shughuli hiyo walieleza kuwa lengo la khitma hiyo ni kuenzi mchango wa Mashahidi katika kuutumikia Uislamu, kuimarisha utamaduni wa kushikamana na Qur'an Tukufu, na kuwaombea amani na umoja Waislamu duniani.

Hawza ya Hazrat Zainab (as) Kigamboni Yaandaa Khatmu ya Qur'an Tukufu kwa Ajili ya Shahidi Sayyid Ali Khamenei na Mashahidi wote wa Vita vya Ramadhan

Hawza ya Hazrat Zainab (as) Kigamboni Yaandaa Khatmu ya Qur'an Tukufu kwa Ajili ya Shahidi Sayyid Ali Khamenei na Mashahidi wote wa Vita vya Ramadhan

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha