Mwanadiplomasia wa ngazi ya juu nchini India ameahidi kuimarisha uhusiano na Pakistan leo baada ya mkutano wa kwanza na mwenzake wa India tangu pale nchi hiyo ilipositisha mazungumzo yenye lengo la kupunguza mizozo mingi baina yao mwaka jana.
Hali ya wasi wasi baina ya nchi hizo jirani yenye silaha za kinyuklia imesababisha majeshi ya nchi hizo kufyatua risasi katika mapaka wao katika jimbo la Kashmir mara kadhaa katika muda wa mwaka mmoja uliopita.
Kiasi ya watu 12 wameuwawa na maelfu wamelazimika kukimbia kutoka majumbani mwao katika mapigano ya hivi karibuni mwezi wa Januari.
Pakistan na India zimepigana vita mara mbili kuhusiana na jimbo la Kashmir tangu mapigano yaliyofuatia kugawanywa kwa nchi hizo mbili mwaka 1947 , baada ya kumalizika kwa utawala wa kikoloni wa Uingereza.
Muungano mpya kati ya chama tawala cha Hindu nationalist na chama cha Peoples Democratic Party, PDP ambacho kinataka utawala huru katika jimbo la Kashmir linalodhibitiwa na India , umetoa ishara kuwa ushirikiano unawezekana.