Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Ahl al-Bayt (a.s) - ABNA -; Harakati ya Hamas imetangaza: Ripoti ya gazeti la Yediot Aharonot kuhusu kusitishwa kwa mawasiliano au kusitishwa kwa mazungumzo kuhusu makubaliano ya kubadilishana wafungwa si ya kweli. Bado tuko katikati ya mazungumzo na tunafuatilia mazungumzo na wasuluhishi kwa uwajibikaji na umakini.
Kwa mujibu wa ripoti ya Al Jazeera, Hamas imesisitiza: Tunazingatia pendekezo la Steven Whitkoff, mjumbe wa Marekani katika Mashariki ya Kati, na mawazo mbalimbali ya kutekeleza makubaliano ya kubadilishana wafungwa na kumaliza vita na kuhakikisha Israel inajitoa ndani ya Gaza.
Siku ya Jumanne, utawala wa Kizayuni ulianza tena mashambulizi yake dhidi ya Ukanda wa Gaza, ambayo yamesababisha Vifo vya Kishahidi na kujeruhi mamia ya watu.
Your Comment