16 Agosti 2025 - 23:06
Mwanafunzi wa Kitanzania Apewa Heshima ya Kusoma Maatam ya Arubaini ya Imam Hussein (A.S) Katika Haram ya Imam Ali (A.S), Najaf Al-Ashraf

Hii ni kwa mara nyingine tena, Sauti ya Tanzania kuinuliwa Katika Haram Tukufu ya Imam Ali (A.S), katika Mji Mtukufu wa Najaf Al-Ashraf Nchini Iraq, kupitia Mwanafunzi huyu Mpenzi wa Mtume Muhammad (saww) na Aali zake Muhammad (Amani iwe juu yao).

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Sheikh Mustafa Khatibu Nkonga, Mwanafunzi wa Kitanzania anayesoma nchini Iraq, amepata fursa adhimu na ya kipekee ya kusoma Maatam ya Maombolezo ya Arubaini ya Imam Hussein (a.s) - Mjukuu wa Mtume Muhammad (s.a.w.w) - katika Mimbari ya Haram Tukufu ya Imam Ali bin Abi Talib (a.s), iliyopo katika Mji Mtukufu wa Najaf Al-Ashraf.
 

Mwanafunzi wa Kitanzania Apewa Heshima ya Kusoma Maatam ya Arubaini ya Imam Hussein (A.S) Katika Haram ya Imam Ali (A.S), Najaf Al-Ashraf


Hii ni heshima kubwa si tu kwake binafsi, bali pia kwa Tanzania na Waislamu wote Wapenzi wa Ahlul-Bayt (as) Waliopo katika ukaenda wa Afrika Mashariki, kuwakilishwa katika Jukwaa Takatifu la Ahlul-Bayt (a.s).

Kwa mara nyingine tena, Sauti ya Tanzania imeinuliwa katika anga la Najaf Al-Ashraf kupitia Mwanafunzi huyu Mchaji Mungu, na Mpenzi wa Mtume Muhammad (S.A.W.W) na Aali zake Watoharifu (A.S).

Mwanafunzi wa Kitanzania Apewa Heshima ya Kusoma Maatam ya Arubaini ya Imam Hussein (A.S) Katika Haram ya Imam Ali (A.S), Najaf Al-Ashraf

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha