17 Agosti 2025 - 00:25
Watu Zaidi ya Milioni 21 Wamehudhuria katika Arubaini ya Imam Hussein (a.s) kwa Mwaka huu wa 1447 Hijria / 2025

Kulingana na taarifa ya Haram Tukufu ya Abasi, idadi ya mahujaji waliohudhuria maadhimisho ya Arubaini ya Imam Hussein (a.s) mwaka huu imefikia milioni 21,103,524.

Shirika la habari la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- linaripoti kuwa takwimu hizi zimekusanywa kwa kutumia mfumo wa kuhesabu kielektroniki unaotumia akili bandia (AI), ambao unarekodi idadi ya wahudhuriaji wanaoingia Karbala kupitia njia tano kuu:

1. Baghdad → Karbala

2. Baghdad → Al-Jamaliya

3. Najaf → Karbala

4. Babil → Karbala

5. Husayniya → Karbala.

Wakuu wa Haram wamesema kuwa mfumo huu umekuwa ukifanyakazi kwa mfululizo kwa miaka 10, na unakusanya data kwa wakati halisi.

Katika taarifa yao, Haram Tukufu ya Abasi iliongeza:
“Tunatoa rambirambi zetu kwa Imam wa Zama (a.j), marjaa wakuu, na ummah ya Kiislamu kwa heshima ya Arubaini ya Imam Hussein (a.s), na tunaomba Mwenyezi Mungu awarudishe mahujaji salama na kwa ajili ya ibada zao zilizokubalika.”

Watu Zaidi ya Milioni 21 Wamehudhuria katika Arubaini ya Imam Hussein (a.s) kwa Mwaka huu wa 1447 Hijria / 2025

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha