Kwa Mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) - ABNA - Msemaji wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC), Brigedia Jenerali Hussein Mohabbi, amesema kuwa uharibifu uliotokea katika jengo la abiria la Uwanja wa Ndege wa Kuwait ulisababishwa na hitilafu ya mifumo ya ulinzi ya Marekani ya Patriot, na si shambulio la makombora ya Iran.
Akizungumza Jumatano, Brigedia Jenerali Mohabbi alisema uchunguzi uliofanywa na mamlaka husika um
eonyesha kuwa Kikosi cha Anga na Anga za Juu cha IRGC hakikurusha kombora lolote kuelekea uwanja huo wa ndege.
Alifafanua kuwa jengo la abiria liliharibiwa baada ya kombora la mfumo wa Patriot kuanguka katika eneo hilo kufuatia kushindwa kuzuia makombora ya Iran yaliyokuwa yakielekezwa katika malengo mengine.
Msemaji huyo alisisitiza kuwa matokeo ya uchunguzi yanaondoa madai kwamba Iran ilihusika moja kwa moja na tukio hilo, akieleza kuwa hitilafu ya mfumo wa ulinzi wa Patriot ndiyo iliyosababisha uharibifu huo.
Your Comment