Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) –ABNA– Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Urusi, Kazem Jalali, amesema Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, anatoa umuhimu mkubwa kwa ufuatiliaji wa miradi ya pamoja kati ya Tehran na Moscow, kwa lengo la kuharakisha ushirikiano wa pande mbili.
Jalali amesema Rais Pezeshkian anafuatilia kwa karibu maelezo ya miradi hiyo ili kuhakikisha kasi ya utekelezaji wa ushirikiano kati ya Iran na Urusi inaongezeka kwa namna inayolinda na kutimiza maslahi ya wananchi wa mataifa hayo mawili rafiki.
Akizungumzia mradi wa ujenzi wa reli ya Rasht–Astara, Balozi Jalali amesema kuwa sasa kuna umuhimu wa kusainiwa kwa mkataba wa utekelezaji wa ujenzi wa reli hiyo.
Amesema kuwa Rais Pezeshkian na Waziri wa Barabara na Maendeleo ya Miji wa Iran, Farzaneh Sadegh, wamekuwa wakisisitiza umuhimu wa kuendelezwa kwa mradi huo.
Jalali ameongeza kuwa wakati wa mkutano wake wa hivi karibuni na Rais Pezeshkian, alimwomba Rais huyo kuhakikisha kuwa Waziri wa Barabara na Maendeleo ya Miji anafanya ziara nchini Urusi haraka iwezekanavyo, au ujumbe wa Urusi uje Tehran, kwa lengo la kukamilisha na kusaini mkataba wa utekelezaji wa mradi huo.
Kwa mujibu wa Balozi Jalali, kukamilishwa kwa mkataba huo kutawezesha upande wa Urusi kuanza kazi za utekelezaji wa ujenzi wa reli ya Rasht–Astara, ambayo ni sehemu muhimu ya kuimarisha ushirikiano wa kimkakati wa usafirishaji na miundombinu kati ya Iran na Urusi.
Maoni yako