Ijumaa
-
Imamu wa Ijumaa wa Baghdad: Waislamu wote wanapaswa kusimama na Ayatollah Khamenei
Imamu wa Ijumaa wa Baghdad ametoa taarifa yenye maneno makali kufuatia jinai ya hovyo ya Trump.
-
Mada ya Ijumaa Masjidul Ghadir Kigogo Post: "Hijjah na Athari Zake Katika Malezi (ya Watoto na Jamii)"
Tarehe: Ijumaa, 30 Mei 2025. Mahali: Masjidul Ghadir, Kigogo Post – Dar-es-Salaam, Tanzania. Khatibu wa Swala ya Ijumaa: Maulana Sheikh Hemed Jalala. Mada ya Khutba ya Ijumaa: "Hijjah na Athari Zake Katika Malezi". Khutba hii iliangazia Nafasi ya Hijjah kama Shule ya Malezi ya kina, ikihimiza wazazi na jamii kwa ujumla kutumia mafundisho ya Hijjah kuwalea watoto katika misingi ya Utii, Ucha Mungu, Uvumilivu, Unyenyekevu na Umoja. Pia, iliweka msisitizo wa umuhimu wa Mwezi wa Dhilhijja katika historia ya Uislamu na fadhila za ibada ndani yake.
-
Sheikh Hemed Jalala | Khutba ya Ijumaa (Malezi ya Watoto) - Masjidul Ghadir, Kigogo Post, Dar-es-Salaam
Sheikh Hemed Jalala alisisitiza umuhimu wa malezi bora ya watoto kwa kufuata misingi thabiti ya Kiislamu. Alibainisha kuwa familia ni msingi wa jamii, na hivyo malezi ya mtoto yanapaswa kuakisi maadili na mafundisho ya dini.
-
Sheikh Abdul Ghani Khatibu | Khutba ya Ijumaa: “Karama na Heshima ya Mwanadamu - Msimamo Wetu wa Kiutu”
Lengo letu si mkate - Bali ni kuishi kwa hadhi, kwa karama, kwa ujasiri wa kusimamia ukweli, hata kama ni mchungu. Tusimame na wanyonge: Tusisahau ndugu zetu wanaodhulumiwa, kama Wapalestina, ambao kila siku wanapigania si mkate - bali heshima yao, ardhi yao, utu wao na Karama yao.
-
Swala ya Ijumaa Yaswaliwa katika Chuo Cha Jamiat Al-Mustafa (s), Dar-es-Salaam:Khatibu wa Ijumaa Sheikh Bakari Mtulia Azungumzia "Umuhimu wa Kusamehe"
Kutoa Msamaha, hakupunguzi Heshima ya Mtu, Bali kunaongeza Heshima ya Mtu mbele ya Mwenyezi Ahlul-Bayt (as), Familia ya Mtume Muhammad (s.a.w.w) walikuwa mfano wa Hali ya Juu ya huruma, subira, na Kusamehe.
-
Ugumu uliopo katika kuwatangaza Kizazi Kitukufu cha Mtume Muhammad (saww) ambao ni Mawalii wa Mwenyezi Mungu (s.w.t) | Watu hawawajui Ahlu-Bayt (as)!
Leo hii, jambo la kuwatangaza Ahlul-Bayt (a.s) ambao ndio tumeusiwa na Mtume wetu Muhammad (s.a.w.w) tushikamane nao baada yake na kuwafuata wakiwa wakiwa kama Kizito cha Pili baada ya Qur'an Tukufu, ni jambo gumu kulingana na jamii ya watu tunayokabiliana nayo.
-
Tunajifunza nini baada ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhan?
Aliyekuwa akifanya Ibada za Usiku ndani ya Ramadhani na mwendo wake ukabadilika na tabia zake kuwa nzuri ndani ya Ramadhan, basi aendelee kuwa na tabia nzuri hivyo hivyo hata baada ya Ramadhan. Na hii ni sehemu ya wito na funzo zuri toka kwa Mtume wetu Muhammad (s.a.w.w).
-
Takriban watu 20 Wameuawa baada Wanajeshi wa Nigeria kushambulia Maandamano ya Siku ya Quds Mjini Abuja
Makumi ya waandamanaji wanaounga mkono Palestina wameuawa na kujeruhiwa baada ya vikosi vya usalama kuwafyatulia risasi wakiwa kwenye Maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds katika Mji Mkuu wa Nigeria.
-
Siku ya Quds Duniani:
Amani ya Palestina, ni Amani ya Tanzania
Wito wa kujitokeza kwa watu wote, Waislamu na Watanzania wote wapenda Haki katika siku ya Kimataifa ya Quds, ili kuungana na Wapalestina katika kutetea Haki zao za Kibinadamu katika Taifa lao la Palestina, na vile yakiwa ni Matembezi ya Masjid Al_Aqsa, ambayo ni Kibla cha Kwanza cha Waislamu.