Ijumaa
-
Dr. Alhad Mussa Salum: “Tumuadhimishe Mtume (S) na Tufuate Nyayo Zake”:
Jiji la Dar es Salaam Kujumuika Katika Maulid ya Masjid Majmuuat - Temeke Mwisho (Ijumaa: 17 -10-2025)
Dr. Alhad Mussa Salum ametoa wito kwa Waumini na watu wote wa Dar -es- Salaam na vitongoji vyake kuhudhuria kwa wingi katika hafla hiyo akisisitiza: “Tumuadhimishe Mtume Muhammad (s.a.w.w), tumtukuze, na tufuate nyayo zake kwa upendo na amani.”
-
Kuzingatia Umuhimu wa Swala ya Ijumaa na Tabia Njema katika Hawzat ya Wasichana ya Hazrat Zainab (s.a) - Tanzania
Hadithi: “إِنَّمَا بُعِثْتُ لِأُتَمِّمَ مَکَارِمَ الأَخْلَاقِ.” “Mimi nimetumwa ili nikamilishe tabia njema.” Aya Tukufu: «قَدْ أَفْلَحَ مَن زَكَّاهَا وَقَدْ خَابَ مَن دَسَّاهَا» (Surat Ash-Shams, Aya 9–10). "Amefaulu yule aliyeitakasa nafsi yake, na ameharibikiwa yule aliyeichafua (aliyeifisidi)".
-
Imamu Jamaa wa Zamani wa Masjid al-Haram (Msikiti Mtukufu wa Makkah) Aachiwa Huru Baada ya Miaka 7 Gerezani Saudi Arabia
Sheikh Saleh Al-Talib mnamo mwaka 2018 katika moja ya khutba zake alipinga maonesho ya muziki (konseti) na mikusanyiko ya kijinsia iliyochanganyika, jambo lililosababisha kutoridhishwa na viongozi wa Saudia na pia shinikizo kutoka kwa taasisi za kiserikali zinazohusiana na Mamlaka Kuu ya Burudani ya Saudi Arabia, na hatimaye kusababisha kukamatwa kwake.
-
Mwenyekiti wa Baraza la Sera za Maimamu wa Ijumaa nchini:
"Swala ya Ijumaa ni nguzo ya Umoja wa Kitaifa - Lazima iwafikie watu wa makundi yote"
Mwenyekiti wa Baraza la Sera za Maimamu wa Ijumaa nchini: "Swala ya Ijumaa inapaswa kuwa ya watu wote na kuakisi umoja wa kitaifa."Akiangazia umuhimu wa nafasi ya wananchi na ushirikishi mpana katika Swala ya Ijumaa, mwenyekiti huyo alisema: “Makamati ya Swala ya Ijumaa yanapaswa kwa ubunifu na upangaji madhubuti, kuweka mazingira yanayowezesha ushiriki wa watu wa makundi yote ya jamii — kuanzia wanafunzi wa vyuo vikuu, walimu na wasomi, hadi wafanyakazi wa viwandani na wakulima.” Aliongeza kuwa kwa njia hii, ibada hii ya kiroho na kisiasa itakuwa ni taswira kamili ya mshikamano na umoja wa kitaifa.
-
Swala ya Ijumaa - Madrasa Hazrat Zainab (sa) - Kigamboni | Changamoto za Kijamii Zinazotokana na Kuachana na Mafundisho ya Dini
Sala ilisaliwa kwa nidhamu kubwa na utulivu wa hali ya kiroho, na iliacha athari kubwa kwa washiriki wote katika ibada hii.
-
Imamu wa Ijumaa wa Baghdad: Waislamu wote wanapaswa kusimama na Ayatollah Khamenei
Imamu wa Ijumaa wa Baghdad ametoa taarifa yenye maneno makali kufuatia jinai ya hovyo ya Trump.
-
Mada ya Ijumaa Masjidul Ghadir Kigogo Post: "Hijjah na Athari Zake Katika Malezi (ya Watoto na Jamii)"
Tarehe: Ijumaa, 30 Mei 2025. Mahali: Masjidul Ghadir, Kigogo Post – Dar-es-Salaam, Tanzania. Khatibu wa Swala ya Ijumaa: Maulana Sheikh Hemed Jalala. Mada ya Khutba ya Ijumaa: "Hijjah na Athari Zake Katika Malezi". Khutba hii iliangazia Nafasi ya Hijjah kama Shule ya Malezi ya kina, ikihimiza wazazi na jamii kwa ujumla kutumia mafundisho ya Hijjah kuwalea watoto katika misingi ya Utii, Ucha Mungu, Uvumilivu, Unyenyekevu na Umoja. Pia, iliweka msisitizo wa umuhimu wa Mwezi wa Dhilhijja katika historia ya Uislamu na fadhila za ibada ndani yake.
-
Sheikh Hemed Jalala | Khutba ya Ijumaa (Malezi ya Watoto) - Masjidul Ghadir, Kigogo Post, Dar-es-Salaam
Sheikh Hemed Jalala alisisitiza umuhimu wa malezi bora ya watoto kwa kufuata misingi thabiti ya Kiislamu. Alibainisha kuwa familia ni msingi wa jamii, na hivyo malezi ya mtoto yanapaswa kuakisi maadili na mafundisho ya dini.
-
Sheikh Abdul Ghani Khatibu | Khutba ya Ijumaa: “Karama na Heshima ya Mwanadamu - Msimamo Wetu wa Kiutu”
Lengo letu si mkate - Bali ni kuishi kwa hadhi, kwa karama, kwa ujasiri wa kusimamia ukweli, hata kama ni mchungu. Tusimame na wanyonge: Tusisahau ndugu zetu wanaodhulumiwa, kama Wapalestina, ambao kila siku wanapigania si mkate - bali heshima yao, ardhi yao, utu wao na Karama yao.
-
Swala ya Ijumaa Yaswaliwa katika Chuo Cha Jamiat Al-Mustafa (s), Dar-es-Salaam:Khatibu wa Ijumaa Sheikh Bakari Mtulia Azungumzia "Umuhimu wa Kusamehe"
Kutoa Msamaha, hakupunguzi Heshima ya Mtu, Bali kunaongeza Heshima ya Mtu mbele ya Mwenyezi Ahlul-Bayt (as), Familia ya Mtume Muhammad (s.a.w.w) walikuwa mfano wa Hali ya Juu ya huruma, subira, na Kusamehe.
-
Ugumu uliopo katika kuwatangaza Kizazi Kitukufu cha Mtume Muhammad (saww) ambao ni Mawalii wa Mwenyezi Mungu (s.w.t) | Watu hawawajui Ahlu-Bayt (as)!
Leo hii, jambo la kuwatangaza Ahlul-Bayt (a.s) ambao ndio tumeusiwa na Mtume wetu Muhammad (s.a.w.w) tushikamane nao baada yake na kuwafuata wakiwa wakiwa kama Kizito cha Pili baada ya Qur'an Tukufu, ni jambo gumu kulingana na jamii ya watu tunayokabiliana nayo.
-
Tunajifunza nini baada ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhan?
Aliyekuwa akifanya Ibada za Usiku ndani ya Ramadhani na mwendo wake ukabadilika na tabia zake kuwa nzuri ndani ya Ramadhan, basi aendelee kuwa na tabia nzuri hivyo hivyo hata baada ya Ramadhan. Na hii ni sehemu ya wito na funzo zuri toka kwa Mtume wetu Muhammad (s.a.w.w).
-
Takriban watu 20 Wameuawa baada Wanajeshi wa Nigeria kushambulia Maandamano ya Siku ya Quds Mjini Abuja
Makumi ya waandamanaji wanaounga mkono Palestina wameuawa na kujeruhiwa baada ya vikosi vya usalama kuwafyatulia risasi wakiwa kwenye Maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds katika Mji Mkuu wa Nigeria.
-
Siku ya Quds Duniani:
Amani ya Palestina, ni Amani ya Tanzania
Wito wa kujitokeza kwa watu wote, Waislamu na Watanzania wote wapenda Haki katika siku ya Kimataifa ya Quds, ili kuungana na Wapalestina katika kutetea Haki zao za Kibinadamu katika Taifa lao la Palestina, na vile yakiwa ni Matembezi ya Masjid Al_Aqsa, ambayo ni Kibla cha Kwanza cha Waislamu.