Ijumaa
-
Swala ya Ijumaa Yaswaliwa katika Chuo Cha Jamiat Al-Mustafa (s), Dar-es-Salaam:Khatibu wa Ijumaa Sheikh Bakari Mtulia Azungumzia "Umuhimu wa Kusamehe"
Kutoa Msamaha, hakupunguzi Heshima ya Mtu, Bali kunaongeza Heshima ya Mtu mbele ya Mwenyezi Ahlul-Bayt (as), Familia ya Mtume Muhammad (s.a.w.w) walikuwa mfano wa Hali ya Juu ya huruma, subira, na Kusamehe.
-
Ugumu uliopo katika kuwatangaza Kizazi Kitukufu cha Mtume Muhammad (saww) ambao ni Mawalii wa Mwenyezi Mungu (s.w.t) | Watu hawawajui Ahlu-Bayt (as)!
Leo hii, jambo la kuwatangaza Ahlul-Bayt (a.s) ambao ndio tumeusiwa na Mtume wetu Muhammad (s.a.w.w) tushikamane nao baada yake na kuwafuata wakiwa wakiwa kama Kizito cha Pili baada ya Qur'an Tukufu, ni jambo gumu kulingana na jamii ya watu tunayokabiliana nayo.
-
Tunajifunza nini baada ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhan?
Aliyekuwa akifanya Ibada za Usiku ndani ya Ramadhani na mwendo wake ukabadilika na tabia zake kuwa nzuri ndani ya Ramadhan, basi aendelee kuwa na tabia nzuri hivyo hivyo hata baada ya Ramadhan. Na hii ni sehemu ya wito na funzo zuri toka kwa Mtume wetu Muhammad (s.a.w.w).
-
Takriban watu 20 Wameuawa baada Wanajeshi wa Nigeria kushambulia Maandamano ya Siku ya Quds Mjini Abuja
Makumi ya waandamanaji wanaounga mkono Palestina wameuawa na kujeruhiwa baada ya vikosi vya usalama kuwafyatulia risasi wakiwa kwenye Maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds katika Mji Mkuu wa Nigeria.
-
Siku ya Quds Duniani:
Amani ya Palestina, ni Amani ya Tanzania
Wito wa kujitokeza kwa watu wote, Waislamu na Watanzania wote wapenda Haki katika siku ya Kimataifa ya Quds, ili kuungana na Wapalestina katika kutetea Haki zao za Kibinadamu katika Taifa lao la Palestina, na vile yakiwa ni Matembezi ya Masjid Al_Aqsa, ambayo ni Kibla cha Kwanza cha Waislamu.