Tukio
-
Iran Yalaani Vikali Shambulio la Kigaidi Lililolenga Msikiti Nchini Pakistan
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Ismail Baghaei, amelaani vikali shambulio la kigaidi lililolenga msikiti katika mji wa Kohat, Pakistan. Shambulio hilo limetokea wakati wa Swala ya Ijumaa na kusababisha vifo na majeruhi kwa makumi ya watu. Iran imetoa salamu za rambirambi kwa familia za waathirika, Serikali na wananchi wa Pakistan.
-
Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Washiriki Maandamano ya Arubaini mjini Tehran Wakipeperusha Bendera Nyekundu na Picha za Mashahidi
Maelfu ya wanafunzi wa vyuo vikuu nchini Iran walishiriki maandamano ya Arubaini ya Imam Hussein (as) katika mji mkuu wa Tehran, wakibeba bendera nyekundu na picha za mashahidi wa taifa, wakisisitiza mshikamano wao na njia ya Karbala, utetezi wa haki na kuhifadhi kumbukumbu za mashahidi.
-
Reuters: Benki ya Capital One Yafunga Akaunti za Shirika la Trump kutokana na Uchunguzi wa Utakatishaji Fedha
Benki ya Capital One imetangaza kufunga akaunti zinazohusishwa na Shirika la Trump baada ya uchunguzi unaohusiana na sheria za kupambana na utakatishaji fedha, ikiwa ni mara ya kwanza kwa benki kutaja rasmi sababu za aina hiyo kuhusu biashara ya familia ya rais wa Marekani.
-
Kama tukio la Ashura lingetokea leo, ni simulizi gani lingekuwa gumzo zaidi kwenye mitandao ya kijamii?
Ashura haikuwa tu vita ya kijeshi iliyopiganwa katika jangwa, bali ilikuwa uwanja mkubwa wa mapambano kati ya ukweli mtupu na uongo uliopambwa kwa sura ya kuvutia. Ikiwa tukio hili lingetokea katika zama za mawasiliano ya kisasa, bila shaka mashine ya propaganda ya kambi ya batili ingetumia nguvu zake zote za kishetani kupotosha mapinduzi ya Sayyid al-Shuhadaa (a.s.), kwa lengo la kubadilisha nafasi za dhalimu na mwenye kudhulumiwa.
-
Tukio la Tatu la Kimataifa la “Sisi ni Wana wa Hussein (as)”
Wito kwa wanahabari, watayarishaji wa maudhui na wadau wa vyombo vya habari kushiriki katika kampeni ya kurekodi na kuhifadhi mandhari mbalimbali za Arbaeen ya Imam Hussein (as). Washiriki wanakaribishwa kutuma kazi katika nyanja za picha, video, maudhui ya Akili Bandia (AI) na podcast, zikiwemo mada maalumu kuhusu Kiongozi Shahidi katika njia ya Hussein (as) na Dunia moja katika kumbatio la Hussein (as). Kazi zinapaswa kutumwa kupitia @nahno_abna_alhussain kabla ya 22 Septemba 2026.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu: Kumuaga Shahidi Mkuu wa Iran Kulikuwa Tukio la Kihistoria na Mwamko Mkubwa Usio na Mfano
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu amepongeza wananchi wa Iran kwa kuandaa tukio kubwa la kihistoria la kumuaga shahidi mkuu wa Iran, akisema kuwa ushiriki wa makumi ya mamilioni ya wananchi umeonesha kiwango kipya cha utambulisho wa Kiislamu na Kiirani, uaminifu, uelewa na upendo mkubwa kwa kiongozi wa Umma wa Kiislamu na kiongozi shahidi wa Mapinduzi.
-
IRGC yadai kulenga Kambi ya Anga ya Amir Hassan nchini Jordan kwa makombora na ndege zisizo na rubani
Kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC), vikosi vyake vimedai kulenga majukwaa ya makombora, maghala ya mafuta na maeneo ya kuhifadhia silaha katika Kambi ya Anga ya Amir Hassan nchini Jordan, katika kile ilichokieleza kuwa ni hatua ya kujibu ukiukaji uliofanywa dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Ayatollah Khatami: Trump na Netanyahu Hawatakuwa na Usingizi wa Amani
Mwanachama wa Jumuiya ya Walimu wa Hawza ya Elimu ya Kiislamu ya Qom amesema kuwa ibada za mazishi ya Kiongozi aliyefariki akiwa shahidi katika maeneo mbalimbali ya nchi zimegeuka kuwa jukwaa la umoja, mshikamano na kuhuisha ahadi ya utii kwa Mapinduzi ya Kiislamu. Amesisitiza kwamba: “Trump na Netanyahu hawatakuwa na usingizi wa amani.”
-
Iran Yatangaza Kushambulia Malengo ya Kijeshi ya Marekani Nchini Qatar
Iran imetangaza kuwa imefanya mashambulizi dhidi ya malengo ya kijeshi ya Marekani yaliyoko nchini Qatar ikijibu mashambulizi ya Marekani Dhidi yake na katika hatua inayoashiria kuongezeka kwa mvutano wa kijeshi kati ya Tehran na Washington.
-
Mwanaharakati wa Vyombo vya Habari wa Urusi: Sijawahi Kushuhudia Jambo Kama Hili Maishani Mwangu
Mwanaharakati wa vyombo vya habari kutoka Urusi amesema umati mkubwa wa wananchi waliojitokeza kumuaga kiongozi wao umeandika historia, akisisitiza kuwa mshikamano wa Wairani umeonyesha mapenzi ya dhati kwa taifa na uongozi wao.
-
Hilali Nyekundu: Hakuna Majeruhi Walioripotiwa Katika Hafla ya Kuaga Kiongozi Shahidi Licha ya Mamilioni ya Waombolezaji Kushiriki
Shirika la Hilali Nyekundu limetangaza kuwa hadi sasa hakuna majeruhi walioripotiwa katika hafla ya kuaga Kiongozi Shahidi Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, licha ya mamilioni ya waombolezaji kushiriki. Shirika hilo limeeleza kuwa mafanikio hayo yametokana na usimamizi mzuri wa tukio hilo pamoja na ushirikiano wa wananchi.
-
Wachezaji wa Timu ya Taifa ya Iran Waomboleza Tasu'a ya Imam Hussein (a.s.) nchini Mexico
Wachezaji na viongozi wa msafara wa Timu ya Taifa ya Soka ya Iran wamefanya majlisi ya maombolezo ya Tasu'a ya Imam Hussein (a.s.) katika makazi yao mjini Tijuana, Mexico, wakikumbuka mashahidi wa Karbala na kuonyesha mapenzi yao kwa Ahlul-Bayt (a.s.).
-
Majlisi ya Maombolezo ya Muharram Yafanyika Jamiat Al-Mustafa, Dar es Salaam
Majlisi ya maombolezo ya mwezi wa Muharram imefanyika katika Jamiat Al-Mustafa, Dar es Salaam, Tanzania, ambapo mhadhiri alikuwa Sheikh Taqee Zacharia Athumani, akizungumzia sababu za kuhuishwa kwa kumbukumbu ya Karbala kila mwaka.
-
Uholanzi Yazindua Kumbukumbu ya Kugusa Hisia za Wahanga wa Gaza kwa Maelfu ya Viatu vya Watoto
Maelfu ya viatu vya watoto na picha za waandishi wa habari waliouawa Gaza zimeoneshwa katika uwanja wa Den Bosch nchini Uholanzi katika tukio la kumbukumbu lililolenga kuwakumbuka zaidi ya watoto 21,000 waliopoteza maisha na kulaani ukimya wa kimataifa kuhusu janga hilo.
-
Kamati Yatoa Taarifa ya Kwanza Kuhusu Maandalizi ya Maadhimisho Makubwa Yaliyotajwa Katika Taarifa Rasmi
Kamati ya maadhimisho imesema maandalizi yanaendelea na imezitaka jamii na vyombo vya habari kuepuka kutegemea uvumi, ikiahidi kutangaza maelezo rasmi katika taarifa zijazo.
-
Majibu kwa Shubuhati Zinazohusu Wilayat na Uimamu, na Siri Iliyofichika katika Tukio la Ghadir
«وَلَوْ شِئْتُ أَنْ أُسَمِّیَ الْقَائِلِينَ بِذَلِكَ بِأَسْمَائِهِمْ لَسَمَّيْتُ ... وَلَكِنِّي وَاللَّهِ فِي أُمُورِهِمْ قَدْ تَكَرَّمْتُ» "Na kama ningetaka kuwataja wale waliotoa maneno hayo kwa majina yao, basi ningewataja. Lakini kwa hakika, kwa jina la Mwenyezi Mungu, nimewatendea kwa ukarimu na staha katika mambo yao." Kauli hii inaonyesha kwamba Mtume (s.a.w.w.) aliwajua wanafiki mmoja baada ya mwingine na alikuwa na uwezo wa kuwataja waziwazi. Hata hivyo, kutokana na hekima, ukarimu na maslahi ya Umma wa Kiislamu, hakufanya hivyo. Je, jambo hili lina maana kwamba Mtume (s.a.w.w.) alipuuza wajibu wake? Hapana. Kusudi la utume halikuwa tu kufichua watu, bali lilikuwa kuongoza jamii, kuwapa nafasi ya kutubia na kurejea katika haki, pamoja na kulinda umoja wa Waislamu dhidi ya fitina kubwa zaidi. Kama Mtume (s.a.w.w.) angewataja wanafiki wote hadharani, huenda baadhi yao wangetangaza uasi wao dhidi ya Uislamu, jambo ambalo lingeweza kusababisha migawanyiko mikubwa na hata vita vya ndani katika jamii changa ya Kiislamu. Kwa hiyo, kunyamaza kwake kuhusu majina yao hakukuwa udhaifu wala kuacha wajibu, bali ilikuwa ni sehemu ya hekima ya uongozi wa Mtume katika kuhifadhi maslahi makubwa ya dini na jamii.
-
Wafuasi wa Iran Wakusanyika Mbele ya Bunge la Norway Jijini Oslo - Norway
Kundi la waungaji mkono wa Iran limefanya mkusanyiko mbele ya Bunge la Norway katika mji wa Oslo, likionesha mshikamano wake na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kueleza misimamo yake kuhusu masuala ya kimataifa yanayoihusu nchi hiyo.
-
Mwangwi wa Hamasa Kubwa ya Watu wa Iran katika Vyombo vya Habari vya Kimataifa
Vyombo vingi vya habari vya kimataifa vimezitaja maandamano ya mamilioni ya wananchi wa Iran kuwa ni “onesho la mshikamano” mbele ya uwepo mkubwa wa silaha za kijeshi za Marekani katika eneo hilo, na vikaelezea tukio la 22 Bahman 1404 kuwa ni la kihistoria, kubwa na la kuvutia.
-
Marekani Yatwaa Meli ya Mafuta ya Kirusi Iliyo Husiana na Mafuta ya Venezuela
Hali hii inachangia kuongeza mvutano wa kimataifa, huku washirika wa Venezuela na Urusi wakionya kuhusu matokeo yanayoweza kutokea kutokana na hatua hizo za Marekani.
-
Kuanzia Ulaya hadi Marekani; wimbi jipya na lililopangwa la kudhalilisha Qur’ani chini ya kivuli cha uliberali wa Magharibi
Tukio la kuhujumiwa na kudhalilishwa Qur’an Tukufu huko Stockholm, pamoja na mlolongo wa matusi na dharau zilizotokea Ulaya na Marekani, linafichua uhalisia ambao ndani yake chuki dhidi ya Uislamu imegeuzwa kuwa chombo cha kisiasa mikononi mwa mikondo ya mrengo wa kulia uliokithiri na washirika wao wa Kizayuni.
-
Tamko la Baku limesisitiza kuimarishwa kwa sekta za ubunifu katika ulimwengu wa Kiislamu
Shirika la Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) kupitia Tamko la Baku limesisitiza juu ya umuhimu wa kuimarisha sekta za ubunifu na diplomasia ya kitamaduni katika ulimwengu wa Kiislamu.
-
Mwakilishi wa Ayatullah Sistani:
Licha ya juhudi zote, bado haki ya kueleza na kuonesha kikamilifu ukubwa wa Arbaeen haijatimizwa
Mwakilishi mwenye mamlaka kamili wa Ayatollah Sistani nchini Iran amesema kuwa Arbaeen ni fursa kubwa sana kwa wasimamizi na wenye dhamana wa tukio hili la kimataifa, na hawapaswi kupuuzia au kughafilika na thawabu na malipo makubwa yanayopatikana kutokana nalo.
-
Fadhila za Sayyidat Fatima Zahraa (s.a): Mlinzi Mshikamanifu wa Mtume wa Uislamu (s.a.w.w)
Katika tukio maarufu lililonukuliwa na vitabu vya historia na hadith, Bibi Fatima (a.s) alienda kwa uchungu mkubwa kuondoa matumbo ya ngamia yaliyowekwa na washirikina kichwani mwa Mtume (s.a.w.w) wakati akiwa katika sajda. Tukio hili linabaki kuwa ushahidi wa mapenzi yake ya kipekee na ulinzi usioyumba kwa Mtume wa Uislamu(s.a.w.w).
-
Shia Development Organization na JAI Waongoza Zoezi Kubwa la Uchangiaji Damu Bukoba
Waandaaji wa tukio hilo wamesisitiza umuhimu wa jamii kujitolea na kuwajali wananchi wasiojiweza, hususan wale waliolazwa hospitalini na wanaohitajika kuongezewa damu ili kuendelea kuishi. Wamesema misingi ya Mafundisho ya Kiislamu kupitia watukufu wa Ahlul-Bayt (a.s) inasisitiza thamani ya utu, kusaidiana na kujitoa kwa ajili ya kuimarisha ustawi wa jamii.
-
Daesh wabeba jukumu la shambulio dhidi ya doria ya wanamgambo wa Jolani
Daesh wametekeleza tukio la kushambulia doria inayohusiana na idara ya forodha ya Serikali ya Jolani na kuua watu wawili.
-
Katika mahojiano na ABNA na mwanafalsafa wa Marekani: Kutoka ‘Medina’ hadi New York; Kushindwa kwa Ukuta wa Hofu Dhidi ya Uislamu Marekani
Profesa Charles Taliaferro, profesa mwandamizi wa falsafa katika Chuo cha Saint Olaf, akitaja wimbi la kampeni za propaganda za kupinga Uislamu nchini Marekani, alisema: “Licha ya kuwepo kwa baadhi ya vipengele vya kupinga Uislamu katika jamii ya Marekani, kuna ishara wazi za heshima, utu, na kukubaliana kati ya Waislamu na watu wengine. Ushindi wa Zahran Mamdani katika uchaguzi wa manispaa ya New York ni tukio muhimu katika kuimarisha harakati za kudhoofisha mazungumzo ya hofu dhidi ya Uislamu.”
-
Msimu wa Mizeituni Umekuwa Msimu wa Mauaji katika Ukingo wa Magharibi | Ukandamizaji na mashambulizi ya wakoloni wa Kizayuni yaongezeka kwa ukatili
Msimu wa mavuno ya mizeituni - ishara ya amani na ustawi kwa Wapalestina - umegeuzwa na utawala wa Kizayuni kuwa msimu wa hofu, damu na uharibifu. Ukandamizaji na mashambulizi ya wakoloni wa Kizayuni yaongezeka kwa mpangilio na ukatili mkubwa
-
Spika wa Bunge la Iran: "Iran Haitaikubali Utawala wa Kigeni"
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, ameweka wazi kuwa taifa la Iran halitawahi kukubali kutawaliwa na mataifa ya kigeni na litalinda uhuru wake kwa gharama yoyote.
-
Watu 2 wameuawa katika shambulio la silaha mbele ya sinagogi ya Kiyahudi huko Manchester, Uingereza
Tukio lililotokea sambamba na sherehe ya Yom Kippur mbele ya sinagogi ya Kiyahudi huko Manchester, Uingereza, limesababisha vifo vya watu 2 na kujeruhi wengine 3.