21 Mei 2025 - 22:57
Mashambulizi ya Kombora ya Harakati ya Jihad Islami Dhidi ya Ashdod na Ashkelon Kufuatia Uhalifu wa Israel

Harakati ya Jihad Islami Yajibu Jinai za Utawala wa Kizayuni kwa Kulenga Miji ya Ashdod na Ashkelon Harakati ya Jihad Islami imejibu uhalifu wa utawala wa Kizayuni wa Israel kwa kulenga kwa makombora miji ya Ashdod na Ashkelon. Kufuatia mashambulizi hayo, king’ora cha tahadhari kilisikika mjini Ashkelon, huku vyombo vya habari vya Israeli vikieleza kuwa kombora moja limenaswa angani juu ya jiji hilo.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA-, Tawi la kijeshi la harakati ya Jihad Islami lijulikanalo kama Saraya al-Quds, limetangaza kuwa limevilenga kwa makombora miji ya Ashdod na Ashkelon kama jibu la jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel.

Mamlaka ya ulinzi wa ndani ya Israel siku ya Jumatano ilitangaza kuwa king’ora cha tahadhari kimesikika katika mji wa Ashkelon, hali iliyoashiria uwepo wa shambulio la makombora.

Vyombo vya habari vya Israel vimeeleza madai ya kuyarikisha kombora moja lililokuwa likielekea angani juu ya Ashkelon.

Vyanzo vya habari pia vimeripoti kuwa makundi ya muqawama kutoka Ukanda wa Gaza yametuma kombora moja kuelekea mji wa Ashkelon unaokaliwa kwa mabavu.

Saraya al-Quds imesisitiza kuwa mashambulizi hayo ni sehemu ya kujibu jinai na uvamizi unaoendelea wa Israel dhidi ya watu wa Palestina.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha