18 Julai 2025 - 02:09
Lariyani: “Mazungumzo Sio Kipaumbele Sasa – Adui Lazima Kueleza Kwanza Sababu ya Vita”

Mazungumzo ni (Taktiki) mbinu tu ya Kisiasa inayotumika kufikia lengo Maalum. “Muachieni Kiongozi wa Mapinduzi aamue ni wakati gani na wapi ni sahihi kutumia mbinu hii.”

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Ali Lariyani, Mshauri Mkuu wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatollah Ali Khamenei, amesema kuwa suala la kuanza mazungumzo kwa sasa halipo mezani, akisisitiza kuwa: “Mpinzani wetu ameanzisha vita dhidi yetu. Hatua ya kwanza ni aeleze ni kwa nini walitushambulia.”

Lariyani: “Mazungumzo Sio Kipaumbele Sasa – Adui Lazima Kueleza Kwanza Sababu ya Vita”

Akiwa na msimamo thabiti, Lariyani alionya dhidi ya haraka katika suala la mazungumzo, akieleza kuwa: “Mazungumzo ni mbinu tu ya kisiasa (Taktiki), na si lengo lenyewe.”

Aliongeza kuwa ni juu ya Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi kuamua ni lini na wapi mbinu hiyo itumike: “Muachieni Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi aamue ni wakati gani na wapi ni sahihi kutumia mbinu hii.”

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha