makubaliano
-
Mtaalamu wa Marekani: Vita dhidi ya Iran havipendwi nchini Marekani, Kongamano linaweza kusaidia njia ya kumaliza mzozo
Mtaalamu wa masuala ya Iran na Mashariki ya Kati, Ray Takeyh, amesema vita dhidi ya Iran havina uungwaji mkono mkubwa miongoni mwa wananchi wa Marekani, Chama cha Democrats na baadhi ya vyombo vya habari, akisisitiza kuwa Bunge la Marekani linaweza kuwa na nafasi ya kutafuta njia ya kutoka katika mzozo huo.
-
Afisa wa Lebanon: Makubaliano Mapya na Israel Hayana Uhalali wa Kisheria
Afisa wa Lebanon, Bassam Al-Hashem, amesema kuwa makubaliano ya mfumo yaliyopendekezwa na Israel hayana thamani ya kisheria bila kuidhinishwa na Baraza la Mawaziri na Bunge la Lebanon, akionya kuwa baadhi ya vipengele vyake vinakiuka mamlaka ya taifa.
-
Iran: Marekani Imekiuka Mara Kadhaa Hati ya Maelewano; Tehran Yasisitiza Haitaanzisha Ukiukaji wa Makubaliano
Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imesema Hati ya Maelewano kati ya Tehran na Washington inapitia kipindi cha mgogoro, huku ikiishutumu Marekani kwa kukiuka mara kwa mara masharti ya makubaliano hayo na kuhatarisha usalama wa usafiri wa baharini katika eneo.
-
Iran: Utekelezaji wa Makubaliano na Marekani Unategemea Kutekelezwa kwa Ahadi za Washington | Makubaliano hayo Yamekwisha baina ya Iran na Marekani
Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imesema kuwa utekelezaji wa makubaliano yoyote na Marekani unategemea Washington kutekeleza kikamilifu ahadi zake, huku ikisisitiza kuwa hakuna shaka kuwa makubaliano ya awali ya hati ya maelewano (Memorandum of Understanding) yamefikia mwisho.
-
Iran: Ukiukaji wa Ahadi za Marekani Utakabiliwa na Hatua za Kujibu
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Ismail Baqaei, amesema Iran haijaomba mazungumzo na Marekani, akisisitiza kuwa sera ya Jamhuri ya Kiislamu inategemea kanuni ya "ahadi kwa ahadi" na kwamba ukiukaji wowote wa ahadi za Washington utakabiliwa na jibu la Iran.
-
Khatibu wa Sala ya Ijumaa Tehran: Makubaliano kati ya Iran na Marekani Yanategemea Kanuni ya “Ahadi kwa Ahadi”
Khatibu wa Sala ya Ijumaa mjini Tehran amesema kuwa makubaliano ya maelewano kati ya Iran na Marekani hayajajengwa juu ya msingi wa kuamini serikali ya Marekani, bali yanazingatia kanuni ya “utekelezaji wa ahadi kwa pande zote,” huku akisisitiza kuwa Iran haitaruhusu Marekani kuingilia masuala ya Mlango wa Hormuz.
-
Araghchi Amjibu Trump: Iran Haiombi Mazungumzo ya Makubaliano, Marekani Ndio Inayoomba Mazungumzo
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amekanusha kauli ya Rais wa Marekani Donald Trump kwamba Iran inaomba kufikiwa kwa makubaliano, akisisitiza kuwa ni Washington ambayo imekuwa ikiomba mazungumzo mara kwa mara huku Tehran ikitaka suluhisho la kudumu.
-
Balozi wa Iran katika Umoja wa Mataifa Aitaka Baraza la Usalama Kuepuka Hatua za Uchochezi
Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa, Amir Saeid Iravani, amesema Baraza la Usalama linapaswa kuunga mkono diplomasia na kuepuka hatua zinazoweza kuchochea mvutano au kudhoofisha mazungumzo yanayoendelea.
-
Iran: Mashambulizi ya Marekani Kusini mwa Nchi Yathibitisha Kutoheshimu Ahadi za Kimataifa
Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imelaani mashambulizi ya anga ya Marekani dhidi ya vituo vya ufuatiliaji kusini mwa Iran, ikisema kuwa hatua hiyo inaonesha wazi kwamba Washington haithamini wala kuheshimu ahadi na wajibu wake wa kimataifa.
-
Kauli ya Sheikh Naim Qassem: Makubaliano ya Mfumo kati ya Lebanon na Israel ni “Fedheha na Kusaliti Mamlaka ya Taifa”
Katibu Mkuu wa Hezbollah, Sheikh Naim Qassem, amekosoa vikali makubaliano ya mfumo yaliyofikiwa mjini Washington kati ya serikali ya Lebanon na Israel, akiyataja kuwa ni makubaliano ya fedheha yanayokiuka mamlaka ya taifa la Lebanon na kutoa fursa kwa Israel kuendeleza uvamizi wake.
-
Jenerali Mohsen Rezaei: Jibu kwa ukiukaji wowote wa hati ya maelewano litakuwa la haraka na lenye nguvu
Kamanda wa zamani wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC), Jenerali Mohsen Rezaei, amesema kuwa Iran itajibu kwa haraka na kwa nguvu ukiukaji wowote wa hati ya maelewano, akiishutumu Marekani kwa kukiuka baadhi ya vipengele vya makubaliano hayo kupitia kuunga mkono makundi washirika wake katika eneo na kuendelea kuchochea mvutano katika Mlango wa Hormuz.
-
Marekani yafichua rasimu ya makubaliano ya amani kati ya Israel na Lebanon kwa upatanishi wa Washington
Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imeweka wazi maandishi ya makubaliano ya awali ya amani kati ya Israel na Lebanon yaliyofikiwa kupitia upatanishi wa Marekani mjini Washington. Makubaliano hayo yanalenga kumaliza uhasama wa muda mrefu, kuimarisha usalama wa mipaka, na kuweka utaratibu wa hatua kwa hatua wa kuimarisha mamlaka ya dola nchini Lebanon huku vikosi vya Israel vikijipanga upya kwa awamu.
-
Umoja wa Ulaya Washindwa Kufikia Makubaliano Kuhusu Kumuwekea Vikwazo Itamar Ben-Gvir
Msemaji wa masuala ya nje wa Tume ya Ulaya amesema kuwa nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya hazikufikia mwafaka kuhusu pendekezo la kumuwekea vikwazo Waziri wa Usalama wa Ndani wa Israel, Itamar Ben-Gvir, huku zikilaani kauli zake za uchochezi dhidi ya Lebanon.
-
Mzunguko wa Kwanza wa Mazungumzo ya Uswisi Wafikia Makubaliano Matano Muhimu Kuhusu Iran
Kamati ya habari ya timu ya mazungumzo ya "Minab 168" imetangaza kuwa mzunguko wa kwanza wa mazungumzo yaliyofanyika mjini Bürgenstock, Uswisi, umefikia makubaliano matano muhimu yanayohusu usalama wa Lebanon, Mlango wa Hormuz, mpango wa nyuklia wa Iran, mali zilizogandishwa na kuondolewa kwa baadhi ya vikwazo vya mafuta.
-
Mshauri wa Kiongozi wa Mapinduzi: Marekani Inaelewa Zaidi Lugha ya Uchumi Kuliko Ahadi za Kisiasa
Mshauri wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Mohammad Mokhber, amesema Iran haitakubali makubaliano yasiyotekelezwa kikamilifu na kusisitiza kuwa haki za wananchi wa Iran pamoja na damu za mashahidi haziwezi kusahaulika.
-
Iran Yafunga Mlango wa Bahari wa Hormuz; Yaanza Hatua za Kujibu Ukiukaji wa Makubaliano na Marekani na Israel
Khalil Nasrallah: Iran yafunga Mlango wa Bahari wa Hormuz kama hatua ya kwanza ya kujibu ukiukaji wa makubaliano unaodaiwa kufanywa na Marekani na Israel; sasa mpira uko kwa Donald Trump.
-
J.D. Vance: Trump Ndiye Mshirika Pekee Mwenye Nguvu wa Israel
Makamu wa Rais wa Marekani, J.D. Vance, amesema Rais Donald Trump ndiye mshirika pekee mwenye nguvu wa Israel kwa sasa, akiwataka viongozi wa Tel Aviv kuacha kuikosoa Washington huku akisisitiza kuwa sehemu kubwa ya silaha za Israel hutolewa na Marekani kwa fedha za walipa kodi wa Marekani.
-
Rais Pezeshkian: Juhudi za Pakistan Zitabaki Kwenye Kumbukumbu ya Wairan Milele
Rais wa Iran ameipongeza Pakistan kwa juhudi zake za dhati katika upatanishi uliochangia kufikiwa kwa makubaliano ya awali ya kumaliza vita, huku Tehran na Islamabad zikiahidi kuendelea kuimarisha ushirikiano wa kimkakati kwa ajili ya amani na maendeleo ya kikanda.
-
Ufaransa Yaunga Mkono Njia ya Diplomasia na Hati ya Makubaliano ya Islamabad
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa amethibitisha uungaji mkono kamili wa nchi yake kwa mchakato wa kidiplomasia na Hati ya Makubaliano ya Islamabad, huku Iran ikisisitiza wajibu wa Marekani katika kumaliza vita na kuimarisha amani ya kikanda.
-
Kiongozi wa Mapinduzi Atoa Ujumbe kwa Wairan Kuhusu Makubaliano kati ya Iran na Marekani
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema aliruhusu kutiwa saini kwa hati ya makubaliano kati ya Iran na Marekani baada ya kupokea dhamana kutoka kwa Rais wa Iran kwamba haki za wananchi wa Iran na Kambi ya Muqawama zitalindwa, huku akisisitiza kuwa mazungumzo ya baadaye hayatamaanisha kujisalimisha kwa matakwa ya Marekani.
-
Rais wa Falme za Kiarabu Apongeza Makubaliano ya Marekani na Iran na Kusisitiza Amani ya Kudumu Mashariki ya Kati
UAE yaunga mkono makubaliano ya Marekani na Iran, ikisisitiza amani ya Mashariki ya Kati ijengwe juu ya heshima ya mamlaka ya mataifa na sheria za kimataifa.
-
Makubaliano ya Iran na Marekani Yazua Mabadiliko Mapya ya Kisiasa Mashariki ya Kati
Makubaliano ya amani kati ya Iran na Marekani yameibua mabadiliko makubwa ya kisiasa Mashariki ya Kati, huku yakionekana kuwa ushindi wa diplomasia lakini yakizua mvutano mpya kuhusu Lebanon, Israel na mustakabali wa uhusiano wa Washington na Tel Aviv.
-
Mehr Yafichua Rasimu ya Makubaliano ya Vipengele 14 Kati ya Iran na Marekani
Shirika la Habari la Mehr limechapisha maelezo ya rasimu ya makubaliano yenye vipengele 14 kati ya Iran na Marekani, ikijumuisha kusitishwa kwa vita, kuondolewa kwa vikwazo, kufunguliwa kwa Mlango-Bahari wa Hormuz, kurejeshwa kwa fedha za Iran na mazungumzo kuhusu nyuklia, huku ikisisitiza kuwa mpango wa makombora wa Iran na uhusiano wake na Muqawama havitakuwa sehemu ya makubaliano hayo.
-
Uchambuzi: Kinachoendelea kati ya Iran na Marekani; Makubaliano au Mkakati wa Kusubiri?
Kwa mujibu wa hali halisi ilivyo, kikwazo kikubwa katika mazungumzo kati ya Iran na Marekani si kufikia makubaliano, bali ni ukosefu wa uaminifu na dhamana ya utekelezaji wake. Tehran inasisitiza kuwa haitasaini makubaliano yoyote kwa shinikizo la Washington, bali yale yatakayolinda maslahi yake na usalama wa eneo.
-
Mbunge wa Hizbullah: Israel Itaondoka Kusini mwa Lebanon kwa Mujibu wa Makubaliano kati ya Marekani na Iran
Mbunge wa Hizbullah amesema Lebanon itakuwa sehemu ya makubaliano yoyote ya usitishaji vita, akisisitiza kuwa kuondoka kwa majeshi ya Israel kusini mwa Lebanon na dhamana za Marekani ni masharti muhimu ya utekelezaji wake.
-
Trump: Lebanon Si Sharti Katika Makubaliano ya Muda Mfupi Kati ya Marekani na Iran
Rais Donald Trump amesema kuwa Marekani haitoi sharti la Lebanon kujumuishwa katika makubaliano ya muda mfupi na Iran, huku akisisitiza kuwa kuondolewa kwa vikwazo dhidi ya Tehran kutategemea kufikiwa kwa makubaliano ya amani kwanza.
-
Aliyekuwa Waziri wa Ulinzi wa Marekani Aonya: Mgogoro wa Iran Unaweza Kuwa “Vietnam ya Trump”
Waziri wa zamani wa Ulinzi wa Marekani ameonya kuwa mgogoro wa sasa unaohusishwa na Iran unaweza kufanana na vita vya Vietnam, akisisitiza uwezekano wa matokeo yasiyo thabiti na hitaji la makubaliano dhaifu ambayo yanaweza kusababisha mivutano ya baadaye.
-
Mshauri wa Kiongozi wa Mapinduzi: Marekani Itakubali Masharti ya Iran au Ikabiliwe na Matokeo Makubwa
Mshauri wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu wa Iran ameonya kuwa Marekani italazimika kukubali masharti ya Tehran au kukabiliwa na matokeo makubwa, akiihusumu Washington kwa kuhujumu diplomasia na kutoheshimu makubaliano ya kusitisha mapigano.
-
Bunge la Iran: Lebanon Lazima Iwe Sehemu ya Makubaliano ya Mwisho ya Kusitisha Mapigano
Kamati ya Usalama wa Taifa ya Bunge la Iran imesema Lebanon ni sehemu muhimu ya makubaliano yoyote ya mwisho ya kusitisha mapigano, huku wabunge wa Iran wakisisitiza kuendelea kuiunga mkono Lebanon na harakati za muqawama pamoja na kutaka kukomeshwa kwa vitendo vya uhasama katika eneo hilo.
-
Qalibaf: Marekani Italazimika Kubeba Gharama ya Uhalifu wa Utawala wa Kizayuni nchini Lebanon
Kwa Mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) – ABNA – Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, ametoa onyo kali kwa Marekani kufuatia mashambulizi makali yanayoendelea kufanywa na utawala wa Kizayuni nchini Lebanon, akisema kuwa Washington italazimika kubeba gharama ya uhalifu huo. Kwa mujibu wa Shirika la Habari la IRNA, Qalibaf aliandika katika ukurasa wake kwenye mtandao wa X siku ya Jumatatu kwamba kuzingirwa kwa njia za baharini na kuongezeka kwa vitendo vinavyotajwa kuwa uhalifu wa kivita dhidi ya wananchi wa Lebanon ni ushahidi wa wazi kwamba Marekani haijaheshimu makubaliano ya kusitisha mapigano. Spika huyo wa Bunge la Iran alisisitiza kuwa kila hatua inayochukuliwa katika medani ya kisiasa na kijeshi ina gharama zake, akionya kuwa wale wanaounga mkono au kufumbia macho mashambulizi hayo hawataepuka kuwajibika kwa matokeo yake. Qalibaf aliongeza kuwa kuendelea kwa mashambulizi dhidi ya Lebanon kunathibitisha ushiriki wa Marekani katika kutoa uungaji mkono wa kisiasa na kijeshi kwa utawala wa Kizayuni, jambo ambalo, kwa mujibu wake, linachangia kuongezeka kwa mzozo na mateso ya raia wasio na hatia. Kauli hiyo imekuja wakati mashambulizi ya Israel dhidi ya maeneo mbalimbali ya Lebanon yakiendelea kuzua wasiwasi mkubwa wa kimataifa kuhusu usalama wa raia na hatari ya kupanuka kwa mzozo katika eneo la Mashariki ya Kati.