-
Sheikh Dr.Alhad Mussa Salum aimarisha Falsafa ya Udugu wa Kibinadamu Katika Kongamano la Kielimu Tanzania +Picha
Kikao cha 5 cha Kielimu kilichojadili mada ya “Mkombozi Katika Mitazamo ya Dini Mbalimbali: Tumaini la Viumbe Wote” kilifanyika tarehe 13 Februari 2026, kikiandaliwa na Jamiat Al-Mustafa International Foundation – Tanzania. Kongamano liliwakutanisha wanazuoni na wawakilishi wa dini mbalimbali kwa lengo la kuimarisha mshikamano, maridhiano na amani. Sheikh Dr. Alhad Mussa Salum, Mwenyekiti wa JMAT-TAIFA, alisisitiza kupinga ukabila, ubinafsi na umimi, na kuhimiza mazungumzo ya heshima kati ya dini. Alieleza kuwa dini zote zinapaswa kutambua udugu wa kibinadamu na kushirikiana kwa manufaa ya mustakabali mwema wa wanadamu. Pia aligusia dhana ya Mkombozi, akieleza nafasi ya Imam Mahdi (as) na Mtume Muhammad (saww) kama muombezi mkuu Siku ya Kiyama.
-
Mkutano wa Mshikamano na Wapalestina Mbele ya Bunge la Moroko
Jioni ya Ijumaa, mji mkuu wa Morocco, Rabat, ulishuhudia mkutano wa kuonesha mshikamano na watu wa Palestina huko Gaza na kudai kuingizwa kwa misaada ya kibinadamu katika eneo hili linalozingirwa na utawala wa Kizayuni.
-
Maadhimisho ya Kuzaliwa kwa Imam Mahdi (AS): Vijana Wakumbushwa Wajibu wa Kuijenga Jamii ya Uadilifu katika Kipindi cha Ghaiba
Katika mnasaba wa maadhimisho ya Kuzaliwa kwa Imam Mahdi (AS), Waislamu wa Shia na Sunni walikusanyika kujadili kuhusu Mwokozi wa Ulimwengu na wajibu wa Waumini katika kipindi cha Ghaiba. Khatibu Sheikh Suleimani Abdully aliwakumbusha vijana juu ya umuhimu wa kumcha Mwenyezi Mungu, kushukuru neema Zake na kujenga tabia njema ili kuandaa jamii yenye utu, uadilifu na iliyoepukana na dhulma na ufisadi.
-
Maulana Sheikh Hemed Jalala: "Uislamu ni Ushindi, Izza na Umoja wa Umma"
Sheikh Hemed Jalala: Uislamu wa kweli ulioshikamana na thaqafa ya Karbala unamtambua adui, na unapambana na dhulma ya adui, na kusimamia haki na uadilifu. Uislamu una nguvu kwa sababu una uongozi, wanazuoni na marjaa wanaoupa Umma mwelekeo hata katika nyakati ngumu.
-
Rais Samia Ampokea Rais Museveni Ikulu Dar es Salaam kwa Ziara ya Kikazi ya Siku Moja +Picha
Ziara hiyo inalenga kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia, kiuchumi na kijamii kati ya Tanzania na Uganda.
-
Sheikh Ibrahim Zakzaky (H) Ahudhuria na Kuongea na Maelfu wa Waumini Katika Maadhimisho ya Nisfu Sha’aban Abuja, Nigeria
Kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, Kiongozi wa Harakati za Kiislamu Nigeria, Seikh Ibrahim Zakzaky (H), amehudhuria Maadhimisho ya Nisfu Sha’aban (Nusu ya Mwezi wa Sha'ban) jijini Abuja kwa mara ya pekee mwaka huu, yakilenga kusherehekea mazazi ya Imam Mahdi (a.j.t.f.s) pamoja na kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa kwa Sheikh Zakzaky ambayo huangukia tarehe 15 Sha’aban.
-
Ziara ya Mwenyekiti wa JMAT-TAIFA Sheikh Dkt.Al-Had Mussa Salum Nchini Misri Yaleta Mafanikio kwa Maendeleo ya Vijana
Ziara ya Sheikh Dkt. Alhad Mussa Salum nchini Misri imefungua ukurasa mpya wa ushirikiano wa kimataifa katika elimu, ajira na maendeleo ya vijana kupitia JMAT.
-
Tanzania Yakamata Pakiti 20 za Skanka Zenye Kilogramu 20 Kwenye Bus la Kimataifa, Temeke - Dar-es-salaam
Mamlaka ya DCEA imekamatwa pakiti 20 za skanka zenye uzito wa kilo 20.03 zilizofichwa kwenye balo la mitumba ndani ya bus la Scania la King Masai Tours, lenye namba za usajili AAM 297 CA, likisafiri kati ya Nampula, Msumbiji na Dar es Salaam. Watuhumiwa waliokamatwa ni Amasha Iddi Mrisho (40) kutoka Dar es Salaam na Seleman Juma Ally (32) raia wa Msumbiji. Uchunguzi na kesi za kiutumishi zinaendelea.
-
Malawi | Baraza la Kumbukumbu ya Kufariki kwa Hadhrat Ibrahim (a.s), Mwana wa Mtume Muhammad (s.a.w.w) +Picha
Baraza la kumbukumbu ya kufariki kwa Hadhrat Ibrahim (a.s), mwana wa Mtume (saww), limefanyika Alhamisi, 08/01/2026, katika Shule ya Imam Al-Hadi(as). Baraza hili lilihudhuriwa na wanafunzi na walimu, na Sheikh Abdulrahman Kachera alihutubia katika mnasaba huu. Katika hotuba yake, alisisitiza upendo kwa Ahlul-Bayt (as) uliosisitizwa na Qur'an Tukufu iliposema: (قُل لَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ أَجْرًا إِلَّا الْمَوَدَّةَ فِي الْقُرْبَىٰ), historia ya watoto wa Mtume (saww), ndoa ya Hadhrat Ma'riya al-Qibtiyya, na kufariki kwa Hadhrat Ibrahim (a.s) akiwa mtoto kiumri. Wahudhuriaji walikumbuka tukio hilo kwa huzuni na kuimarisha dhamira ya kufuata maadili na mafundisho ya Ahlul-Bayt (a.s).
-
Maulidi ya Imam Ali (a.s.) Yaadhimishwa katika Madrasa ya Imam Ali (a.s) Vikindu - Tanzania + (Video - Picha)
Baraza la Maulid lilianza kwa kisomo kitukufu cha Aya za Qur’ani Tukufu, kikifuatiwa na maneno ya utangulizi yaliyobainisha umuhimu wa tukio hili tukufu na nafasi ya pekee ya Imam Ali (a.s.) katika Uislamu, kama mfano wa haki, ucha-Mungu, ushujaa na elimu.
-
Waziri Mkuu Dkt.Mwigulu Nchemba Afungua Skuli ya Sekondari Chukwani Zanzibar Katika Maadhimisho ya Miaka 62 ya Mapinduzi +Picha
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba, amefungua rasmi Skuli ya Sekondari Chukwani Zanzibar iliyogharimu shilingi bilioni 6.1, katika maadhimisho ya miaka 62 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, akisisitiza umuhimu wa uwekezaji katika elimu kwa maendeleo ya taifa.
-
Rais Samia Afanya Mazungumzo na Viongozi wa Wizara ya Ulinzi na JKT Zanzibar
Mazungumzo hayo yamezingatia masuala mbalimbali ya usalama, ulinzi wa taifa, na maendeleo ya majeshi, huku akisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya majeshi na wananchi katika kuhakikisha amani na utulivu wa taifa.
-
Ujumbe wa rambirambi wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (a.s) Kufuatia Kifo cha Mwanachuoni wa Afrika Mashariki Sheikh Ali Mayunga
Marehemu alikuwa na mchango mkubwa katika nyanja za kielimu, ikiwemo nafasi yake kama Katibu wa Baraza la Wanazuoni wa Ahlul-Bayt (a.s), na alikuwa miongoni mwa waliotafsiri Qur’an Tukufu kwa lugha ya Kiswahili iliyoitwa Tafsiri Al-Mubin.
-
Ayatollah Dkt. Abbasi, kupitia ujumbe wake, amempa pole Hujjatul-Islam wal-Muslimin Sayyid Aref Naqavi kufuatia kufariki dunia kwa mke wake mpendwa
Ayatollah Dkt. Abbasi ametoa ujumbe wa rambirambi kwa Hujjatul-Islam wal-Muslimin Sayyid Aref Naqavi kufuatia kufariki dunia kwa mke wake, akimuomba Mwenyezi Mungu amrehemu marehemu na awajaalie wafiwa subira na malipo mema.
-
Sa‘yi kati ya Safa na Marwa: Alama ya Imani na Nguzo Muhimu ya Hija na Umra
Aya hii tukufu inathibitisha kuwa sa‘yi baina ya Safa na Marwa ni sehemu muhimu ya ibada ya Hija na Umra, na kwamba hakuna dhambi wala lawama katika kuitekeleza. Kinyume chake, ni ibada iliyoidhinishwa na Qur’ani na kusisitizwa na Sunna ya Mtume ﷺ, na aya imekuja mahsusi kuondoa shaka na uzito uliokuwepo katika nyoyo za watu kuhusu ibada hii.
-
Viongozi wa Serikali na Jeshi la Polisi Jijini Mwanza Watunukiwa Tuzo za Amani Kupitia Kamati ya Maandalizi ya Maridhiano Day 2026
Kamati ya Maandalizi ya Maridhiano Day 2026 imetoa tuzo za heshima kwa viongozi wa Mkoa wa Mwanza pamoja na Jeshi la Polisi, kama ishara ya kutambua mchango wao katika kudumisha amani, mshikamano na utulivu wa kijamii. Tuzo hizo zilitolewa katika hatua inayolenga kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi za serikali, vyombo vya ulinzi na jamii kwa ujumla kuelekea maandalizi ya tukio hilo muhimu la Maridhiano Day 2026.
-
Bilal Tanga: Ujenzi wa Jengo la Ghorofa Tisa Kutoa Suluhisho la Changamoto ya Nafasi kwa Hawza
Taasisi ya Bilal Tanga inaendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuimarisha shughuli za tabligh na elimu ya juu ya Hawza, ikiwa ni sehemu ya dhamira yake ya kuinua elimu ya Kiislamu na kuwahudumia waumini. Katika muktadha huo, ujenzi wa jengo jipya la ghorofa tisa umebeba matumaini makubwa ya kutatua changamoto ya upungufu wa nafasi na kuboresha mazingira ya masomo na dawah.
-
Kufichuliwa kwa mpango wa utawala wa Kizayuni kwa Somaliland
Televisheni ya utawala wa Kizayuni imeashiria nia na madhumuni ya utawala huo kutokana na hatua ya hivi karibuni yenye utata ya kuitambua Somaliland.
-
Shughuli za Uenezi wa Elimu na Maarifa ya Dini Zinazofanywa na Mabanati Wanaosoma Madrasat Hazrat Zainab (SA) Wakati wa Likizo
Picha hizi ni kielelezo cha wazi na dhahiri cha matunda ya juhudi zinazofanywa katika kueneza elimu na maarifa kupitia Madrasat Zainab (SA), inayosimamiwa na Rais wake, Dkt. Ali Taqavi. Tunamuomba Mwenyezi Mungu amlinde, ampe nguvu, afya njema na tawfiq ya kudumu katika kuitumikia Uislamu na Waislamu.
-
Heshima na Unyenyekevu wa Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Mwinyi kwa Wazee | Sala ya Ijumaa - Masjid Abdallah Rashid - Zanzibar
Rais Dkt. Mwinyi pia ameswali Sala ya Ijumaa katika Msikiti wa 'Abdallah Rashid', ikiwa ni hatua inayotekeleza utaratibu wake wa kawaida wa kusali katika Misikiti mbalimbali nchini, kwa lengo la kuimarisha mshikamano wa kijamii na kudumisha mahusiano ya karibu kati ya Viongozi na Waumini.
-
Mufti Mkuu wa Tanzania:
"Qur’an Tukufu Inahimiza Amani Kama Msingi wa Maisha ya Mwanadamu | Tunajifunza Amani Kutoka Katika Kisa cha Nabii Ibrahim (as)
Katika kufafanua hoja yake, Mufti Mkuu wa Tanzania ametaja kisa cha wageni wa Nabii Ibrahim (as) kama kinavyosimuliwa ndani ya Qur’an Tukufu. Amesema kuwa wageni hao walipoingia nyumbani kwa Nabii Ibrahim (as), walimpa maamkizi ya amani, naye akajibu kwa maamkizi yale yale ya amani.
-
Mufti Mkuu wa Tanzania: Mashekhe Msihofu Kutukanwa, Ni Njia ya Thawabu Siku ya Qiyama +Picha
Mheshimiwa Mufti aliwahimiza wanazuoni waendelee kusimamia haki, kuhubiri dini kwa hekima na subira, na kutoacha jukumu lao la kuuelimisha umma licha ya changamoto zinazowakabili.
-
Mkurugenzi wa Khatamul Anbiyaa Institution Arusha Aungana na Wakristo Kuadhimisha Krismasi kwa Misaada ya Kibinadamu +Picha
Waumini wa Kikristo na wanajamii walioshiriki katika hafla hiyo wamepongeza hatua hiyo, wakieleza kuwa ni mfano bora wa kuishi pamoja kwa amani na kuimarisha uhusiano mwema kati ya jamii za kidini nchini Tanzania.
-
Burkina Faso, Mali na Niger Zazindua Operesheni ya Pamoja ya Kijeshi Dhidi ya Makundi ya Kijihadi
Kiongozi wa mpito wa Burkina Faso, Ibrahim Traoré, ametangaza kuanza kwa hatua mpya za kijeshi katika eneo la Sahel baada ya nchi yake, kwa kushirikiana na Mali na Niger, kuzindua operesheni ya pamoja inayolenga kukabiliana na makundi ya kijihadi yanayohusishwa na Al-Qaeda na ISIS. Hatua hiyo inakuja katika muktadha wa kuimarishwa kwa muungano wa kijeshi wa nchi hizo tatu, huku zikisisitiza mshikamano wa kiusalama na mwelekeo mpya wa ushirikiano wa kikanda kufuatia kujiondoa kwao katika ECOWAS na kuvunja ushirikiano wa awali na Ufaransa na Marekani.
-
Waziri Mkuu Dr. Mwigulu Nchemba: Mgawanyiko na Vita vya Ndani Havina Mshindi, Amani Ndiyo Ushindi wa Taifa
Kupitia salamu zake za Krismas - Waziri Mkuu ameutanabahisha Umma wa Watanzania dhidi ya Mgawanyiko na kusisitiza umuhimu wa Amani.
-
Salamu za Krismasi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan
Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan: "Ninawatakia kheri ya Sikukuu ya Krismasi Wakristo na Watanzania wote. Mnaposafiri na kujumuika na ndugu, jamaa na marafiki katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu, tusherehekee sikukuu hii kwa furaha, amani na upendo."
-
Sheikh Hemed Jalala Mwakindenge - Atoa Salam za Krismas kwa Wakristo wote Nchini Tanzania +Picha
Sheikh Hemed Jalala Mwakindenge - Amehitimisha kwa kutoa wito kwa Watanzania wote kutumia sikukuu za kidini kama nyakati za kutafakari, kuimarisha mahusiano ya kijamii, na kuendeleza utamaduni wa amani na upendo unaolinda umoja wa Taifa.
-
Sheikh Dr.Alhad Mussa Salum | Cheti cha Heshima Kwa Waziri Mkuu Mstaafu Mh.Kassim Majaliwa ni Taswira Halisi ya "Falsafa ya Upendo na Umoja wa Kudumu"
Kulinda na kuendeleza upendo na umoja ni jukumu la kila mwanajamii - kwa maneno, kwa matendo na kwa maamuzi - ili kujenga mustakabali wenye matumaini, mshikamano na heshima kwa utu wa binadamu.
-
Faida na Thawabu za Kufanya Umrah Mufradah kwa Mujibu wa Mafunzo ya Ahlul-Bayt (a.s) +Picha
Tunamuomba Mwenyezi Mungu azikubali ibada za Masheikh wetu, awajaalie Umrah yao iwe Umrah yenye kukubalika (Umrah Maqbulah), na arejeshe thawabu zake kwa Ummah wote wa Kiislamu.
-
"Falsafa ya Amani na Haki" Kutoka Katika Mafunzo ya Sheikh Dkt.Alhad Mussa Salum - Mwenyekiti JMAT-TAIFA +Picha
Amani haiwezi kudumu bila haki, na haki haiwezi kupatikana kupitia vurugu wala ghasia.Haki ya kweli hujengwa kwa misingi ya uelewano na kuheshimiana, si kwa kulazimishana. Katika kudai haki, ni muhimu kutumia Amani kama nyenzo kuu ya mawasiliano na maridhiano.