ABNA swahili
  • HABARI KAMILI
  • HABARI MUHIMU
  • Iran
  • ASIA
  • ULAYA
  • AMERIKA
  • AFRIKA
  • PICHA
  • MAKALA
العربية English فارسی Türkçe اردو Español bahasa Indonesia हिन्दी français 汉语 русский Deutsch Melayu Hausa বাংলা Азәрбајҹан Азәрбајҹан әлифбасы Kiswahili မြန်မာဘာသာ bosanski português سورانی 日本語 Kurmancî Pilipinas Тоҷик italiano 한국어
×
filterHabari za leo
  • Sheikh Dkt. Alhad Mussa Salum: "Kuombea Dua Maiti ni Jambo Lililothibitika katika Qur’an na Sunna - Ukisema Maiti Hafaidika Kasome tena Hujui Kitu"

    Sheikh Dkt. Alhad Mussa Salum: "Kuombea Dua Maiti ni Jambo Lililothibitika katika Qur’an na Sunna - Ukisema Maiti Hafaidika Kasome tena Hujui Kitu"

    Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT), Sheikh Dkt. Alhad Mussa Salum, ametoa hotuba fupi katika hafla ya Dua ya kumuombea Marehemu Hafidh Amir Hassan, aliyekuwa Mume wa Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, akisisitiza umuhimu wa kuwaombea Dua waliotangulia mbele ya Haki.

    2026-09-16 00:32
  • Sheikh Dkt. Reihan Yasin Ahimiza Umoja na Ushirikiano wa Waislamu katika Maulid ya Mtume (s.a.w.w) Kigamboni +Video

    Sheikh Dkt. Reihan Yasin Ahimiza Umoja na Ushirikiano wa Waislamu katika Maulid ya Mtume (s.a.w.w) Kigamboni +Video

    Samahat Sheikh Dkt. Reihan Yasin amehimiza Waislamu kuendeleza umoja na ushirikiano uliooneshwa katika Maulid ya Mtume Muhammad (s.a.w.w) Iliyofanyika Kigamboni - Mwapemba, akisisitiza kuwa kumpenda na kumuenzi Mtume (s.a.w.w) kunapaswa kudhihirika kupitia Umoja na mshikamano baina ya Waislamu, kusaidiana na kuzingatia mafundisho yake Matukufu. Akirejea kauli ya مَا كانَ للهِ يَنمُو ومَا كانَ لغيرِ اللهِ يَذْهَبُ جُفَاءً — “Kile kinachofanywa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu hukua na kustawi, na kile kinachofanywa kwa ajili ya asiyekuwa Mwenyezi Mungu huondoka na kutoweka bila athari.” — alieleza matumaini yake kuwa moyo wa umoja na ushirikiano uliooneka mwaka huu, utaendelea kukua na kuimarika na kushuhudiwa zaidi mwakani Insha'Allah.

    2026-09-15 20:46
  • Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania Ashiriki Dua ya Kumuombea Marehemu Hafidh Ameir Hassan - Mtume wa Rais Dr.Samia Suluhu Hassan +Picha

    Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania Ashiriki Dua ya Kumuombea Marehemu Hafidh Ameir Hassan - Mtume wa Rais Dr.Samia Suluhu Hassan +Picha

    Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Dkt. Abubakar Zuber bin Ali, amewasili katika Msikiti wa Bakwata Kinondoni, Dar es Salaam, kwa ajili ya kushiriki dua ya kumuombea marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan, aliyekuwa mume wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

    2026-09-15 16:18
  • Shule ya Kiislamu Al-Hadi - Malawi Yaandaa Kikao cha Kiroho cha Usomaji wa Qur’an Tukufu +Picha

    Shule ya Kiislamu Al-Hadi - Malawi Yaandaa Kikao cha Kiroho cha Usomaji wa Qur’an Tukufu +Picha

    Sehemu ya Utamaduni na Malezi katika Shule ya Kiislamu ya Al-Hadi, yenye uwakilishi wa Al-Mustafa nchini Malawi, yaandaa hafla ya usomaji wa Qur’an kwa ushiriki wa wanafunzi na walimu.

    2026-09-15 15:09
  • Hafla Tukufu ya Maulid ya Mtume Muhammad (s.a.w.w) Yaunganisha Shia na Sunni - Madrasat Zainabiyya Kigamboni +Picha

    Hafla Tukufu ya Maulid ya Mtume Muhammad (s.a.w.w) Yaunganisha Shia na Sunni - Madrasat Zainabiyya Kigamboni +Picha

    Madrasa ya Zainabiyya Kigamboni - Mwapemba yaadhimisha kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (s.a.w.w) kwa kuwakutanisha Waumini wa Shia na Sunni, Masheikh, Walimu, wanafunzi, Wanawake, Wanaume, Vijana na Wazee kwa lengo la kuhuisha mafundisho ya thamani na tabia njema za Mtume (s.a.w.w). Mgeni Rasmi wa hafla hiyo alikuwa Hujjatul-Islam Samahat Sheikh Abdul Majid Nasir, ambaye katika hotuba yake aliwaasa Waumini na jamii kwa ujumla kutumia fursa za hafla za Maulid ya Mtume Muhammad (saww) kama majukwaa ya kujifunza na kutafakari mafundisho yanayopatikana katika maisha yake matukufu. Sheikh Abdul Majid Nasir alisisitiza umuhimu wa kuhuisha vikao vya kheri kama hivyo katika jamii, akieleza kuwa mafundisho na ujumbe wa Maulid haupaswi kubaki ndani ya Taasisi au ndani ya kuta za vituo vya Kiislamu pekee, bali unapaswa kuwafikia wanajamii walio nje ya taasisi hizo.

    2026-09-14 22:23
  • Mwenyekiti wa JMAT-Taifa Sheikh Prof. Alhad Mussa Salum Aongoza Viongozi wa JMAT Kumfariji Rais Samia Suluhu Hassan Kufuatia Msiba wa Mumewe

    Mwenyekiti wa JMAT-Taifa Sheikh Prof. Alhad Mussa Salum Aongoza Viongozi wa JMAT Kumfariji Rais Samia Suluhu Hassan Kufuatia Msiba wa Mumewe

    JMAT Taifa imetoa pole na faraja kwa Rais Samia Suluhu Hassan na familia yake kufuatia kifo cha mumewe, Marehemu Hafidh Ameir Hassan, huku viongozi hao wakisisitiza umuhimu wa amani na mshikamano katika kipindi hiki cha majonzi.

    2026-09-12 14:59
  • Mbunge Suleiman Jafo Ahudhuria Hadhara ya Maulid ya Kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (SAWW) Kariakoo +Picha

    Mbunge Suleiman Jafo Ahudhuria Hadhara ya Maulid ya Kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (SAWW) Kariakoo +Picha

    Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Mhe. Alhaj Suleiman Jafo, amehudhuria hadhara kubwa ya Maulid katika Madrasat Abbasiya, Kariakoo jijini Dar es Salaam, iliyowakutanisha viongozi wa dini, waumini na wananchi kwa ajili ya kuadhimisha mazazi matukufu ya Mtume Muhammad (SAWW) na kusisitiza maadili, upendo na mafundisho yake mema.

    2026-09-11 17:45
  • Hotuba ya Ijumaa |  Malawi: Sheikh Kachera Aeleza Njia za Kufikia Uongofu wa Mwenyezi Mungu +Picha

    Hotuba ya Ijumaa | Malawi: Sheikh Kachera Aeleza Njia za Kufikia Uongofu wa Mwenyezi Mungu +Picha

    Katika hotuba ya Ijumaa - nchini Malawi, Sheikh Abdulrahman Kachera ameeleza aina mbalimbali za uongofu na kusisitiza kuwa imani, kutafakari Qur’ani, kumfuata Mtume (saww) na Ahlul-Bayt (as), kutekeleza wajibu na kujiepusha na madhambi ni miongoni mwa njia za kufikia uongofu wa Mwenyezi Mungu.

    2026-09-11 16:30
  • Majlisi ya Fatiha na Kumbukumbu ya Sheikh Mkuu wa Kwanza wa Shia Tanzania Yafanyika Lindi

    Majlisi ya Fatiha na Kumbukumbu ya Sheikh Mkuu wa Kwanza wa Shia Tanzania Yafanyika Lindi

    Majlisi ya Fatiha na kumbukumbu ya Sheikh Marehemu Abdullah Seif Linganaweka, Sheikh Mkuu wa kwanza wa Jumuiya ya Shia Ithna Ashari Tanzania (T.I.C), imefanyika katika Kijiji cha Mnan'gole, Mkoa wa Lindi, kwa kuhudhuriwa na wanazuoni, viongozi na waumini, wakikumbuka mchango wake wa kidini na kielimu.

    2026-09-11 16:17
  • Sheikh Arif Surya: “Tusifuge watoto, tuwalee” — Atoa wito wa kuimarisha malezi na kuwaunga mkono walimu wa dini

    Sheikh Arif Surya: “Tusifuge watoto, tuwalee” — Atoa wito wa kuimarisha malezi na kuwaunga mkono walimu wa dini

    Sheikh Arif Surya, Mwenyekiti wa Umoja wa Maimamu na Walimu Tanzania (UMATA), ametoa wito kwa wazazi, walimu na viongozi wa dini kuimarisha malezi ya watoto kwa misingi ya Imani, maadili na mfano bora wa wazazi, akisisitiza kuwa mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia yanaanzia katika familia.

    2026-09-09 22:54
  • Cairo na Amman zinaunga mkono uamuzi wa London wa kukabiliana na makazi ya Kiyahudi

    Cairo na Amman zinaunga mkono uamuzi wa London wa kukabiliana na makazi ya Kiyahudi

    Misri na Jordan zililakaribisha hatua ya serikali ya Uingereza ya kupiga marufuku biashara na makazi yasiyo halali ya Israel; hatua iliyochukuliwa kwa lengo la kulinda suluhu ya mataifa mawili na kuzingatia sheria za kimataifa.

    2026-09-09 09:48
  • Sheikh Mkuu wa Jumuiya ya Shia Ithna Ashari Tanzania Katika Mapumziko Yanayoendana na Falsafa ya “Mwili Una Haki Juu ya Mtu, Ikiwemo Haki ya Kupumzika

    Sheikh Mkuu wa Jumuiya ya Shia Ithna Ashari Tanzania Katika Mapumziko Yanayoendana na Falsafa ya “Mwili Una Haki Juu ya Mtu, Ikiwemo Haki ya Kupumzika

    Kupumzika baada ya safari na shughuli nyingi ni sehemu ya kuhifadhi afya ya mwili na kurejesha nguvu kwa ajili ya kuendelea kutekeleza majukumu.

    2026-09-07 21:42
  • Kituo cha Kiislamu cha Al-Imam Al-Hadi (as) Nchini Malawi Chafungua Rasmi Mwaka Mpya wa Masomo 2026 - 2027 +Picha

    Kituo cha Kiislamu cha Al-Imam Al-Hadi (as) Nchini Malawi Chafungua Rasmi Mwaka Mpya wa Masomo 2026 - 2027 +Picha

    Kituo cha Kiislamu Al-Hadi, Tawi la Malawi, kimefanya kwa mafanikio hafla ya ufunguzi wa mwaka wa masomo 2026, huku wanafunzi na walimu wakihimizwa kuanza mwaka mpya kwa kujituma, nidhamu, kuhudhuria masomo kwa wakati na kuzingatia maadili ya Kiislamu.

    2026-09-07 13:47
  • Maulana Sheikh H. Jalala - Sheikh Mkuu wa T.I.C Taifa,  Ampongeza Dkt. Sibtain kwa Huduma za Kijamii Jijini Mwanza +Picha

    Maulana Sheikh H. Jalala - Sheikh Mkuu wa T.I.C Taifa, Ampongeza Dkt. Sibtain kwa Huduma za Kijamii Jijini Mwanza +Picha

    Maulana Sheikh Hemed Jalala Mwakindenge amempongeza Dkt. Alhaji Sibtain na The Desk and Chair Foundation kwa juhudi zao za kuwahudumia wananchi kupitia uchimbaji wa visima, utoaji wa madawati shuleni na kusaidia watu wenye ulemavu.

    2026-09-06 20:48
  • Uzinduzi wa Eneo la Pili la Chuo Kikuu cha Hikmat Afrika Mashariki Nchini Tanzania Waambatana na Maadhimisho ya Maulid ya Mtume (saww) +Picha

    Uzinduzi wa Eneo la Pili la Chuo Kikuu cha Hikmat Afrika Mashariki Nchini Tanzania Waambatana na Maadhimisho ya Maulid ya Mtume (saww) +Picha

    Uzinduzi wa eneo la pili la Chuo Kikuu cha Hikmat Afrika Mashariki nchini Tanzania umefanyika sambamba na maadhimisho ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (saww) na Imam Jaafar Sadiq (as), katika hafla iliyowakutanisha viongozi na wasomi wa Shia na Sunni pamoja na wawakilishi wa dini mbalimbali.

    2026-09-06 18:00
  • Mh.Habib Mbota, Diwani wa Chanika Afungua Matembezi na Sherehe za Maulid ya Mtume Muhammad (saww) Chanika, Handeni +Picha

    Mh.Habib Mbota, Diwani wa Chanika Afungua Matembezi na Sherehe za Maulid ya Mtume Muhammad (saww) Chanika, Handeni +Picha

    Diwani wa Kata ya Chanika, Tanga, Hon. Dr. Habibu Mbota, maarufu kama Mojakwamoja, amefungua rasmi matembezi na sherehe za Maulid ya Mtume Muhammad (saww) yaliyoandaliwa na Shamsul Huda Day katika eneo la Chanika, Handeni.

    2026-09-06 16:51
  • Maulana Sheikh H. Jalala Ahimiza Waislamu Kudumisha Vikao vya Maulidi, Dua na Dhikri - Jijini Mwanza +Picha

    Maulana Sheikh H. Jalala Ahimiza Waislamu Kudumisha Vikao vya Maulidi, Dua na Dhikri - Jijini Mwanza +Picha

    Sheikh Mkuu wa Jumuiya ya Shia Tanzania (TIC), Maulana Sheikh Hemed Jalala Mwakindenge, amewataka Waislamu kudumisha vikao vya Maulidi, dua na dhikri kama sehemu ya kumkumbuka Mtume Muhammad (s.a.w.w.), kujifunza maadili yake na kuimarisha imani katika jamii.

    2026-09-05 16:24
  • Sheikh Prof Alhad Mussa Salum: Mtume Muhammad (s.a.w.w) ana Huruma kwa Walimwengu Wote, Lakini kwa Waumini ana Ra’fah na Huruma +Picha

    Sheikh Prof Alhad Mussa Salum: Mtume Muhammad (s.a.w.w) ana Huruma kwa Walimwengu Wote, Lakini kwa Waumini ana Ra’fah na Huruma +Picha

    Sheikh Prof. Alhad Mussa Salum katika hotuba yake kuhusu kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (saww) alibainisha nukta muhimu kwamba: Mtume Muhammad (saww) ni rehema kwa walimwengu wote, lakini kwa Waumini ana kiwango cha pekee cha Ra’fah na Rahmah, kupitia huruma yake ya karibu, upole wake wa kina na kujali kwake kwa namna ya pekee kwa watu wa imani.

    2026-09-02 22:03
  • Waziri Mhe.Deus Sangu Akutana na Waislamu na Viongozi wa Kiislamu katika Maulid ya Mtume Muhammad (s.a.w.w) Kigogo Post, Dar -es- Salaam

    Waziri Mhe.Deus Sangu Akutana na Waislamu na Viongozi wa Kiislamu katika Maulid ya Mtume Muhammad (s.a.w.w) Kigogo Post, Dar -es- Salaam

    Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Mhe. Deus Sangu, ameshiriki katika hafla ya kumbukizi ya mazazi ya Mtume Muhammad (saww), iliyowakutanisha viongozi mbalimbali wa dini na serikali katika uwanja wa Kigogo Posti, Jijini Dar es Salaam.

    2026-09-02 21:29
  • Noor Centre Dar es Salaam Yaandaa Kikao Maalum cha Kujadili Utume wa Mtume (saw) Katika Dunia ya Kisasa

    Noor Centre Dar es Salaam Yaandaa Kikao Maalum cha Kujadili Utume wa Mtume (saw) Katika Dunia ya Kisasa

    Sheikh Ali Asad Esmail aongoza kikao maalum cha “Utume wa Mtume (saww) Katika Dunia ya Kisasa” kilichoandaliwa na Noor Centre Dar es Salaam, Tanzania.

    2026-09-01 20:21
  • T.I.C Yaandaa Zafa la Maulidi ya Mtume Muhammad (saww) Kigogo Post: “Amani, Upendo na Huruma Ndiyo Mafunzo ya Mtume Muhammad (s.a.w.w)” +Picha

    T.I.C Yaandaa Zafa la Maulidi ya Mtume Muhammad (saww) Kigogo Post: “Amani, Upendo na Huruma Ndiyo Mafunzo ya Mtume Muhammad (s.a.w.w)” +Picha

    Jumuiya ya Shia Ithna'ashariyyah Tanzania (T.I.C) imeandaa zafa maalumu ya kusherehekea Maulidi ya Mtume Muhammad (saww), iliyofanyika tarehe 30 Agosti 2026 katika eneo la Kigogo Post, Dar es Salaam, chini ya kaulimbiu ya “Amani, Upendo na Huruma” ikiwa ni miongoni mwa mafundisho muhimu ya Mtume Muhammad (saww).

    2026-09-01 19:41
  • Ayatollah Sayyid Mojtaba Khamenei Atoa Pongezi za Maulidi ya Mtume Muhammad (saw) na Imam Ja’far Sadiq (as)

    Ayatollah Sayyid Mojtaba Khamenei Atoa Pongezi za Maulidi ya Mtume Muhammad (saw) na Imam Ja’far Sadiq (as)

    Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei amewapongeza Waislamu kote duniani na taifa la Iran kwa maadhimisho ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (saw) na mjukuu wake, Imam Ja’far Sadiq (as), akisisitiza hadhi yao tukufu na nafasi yao katika kuiongoza na kuiunganisha Umma wa Kiislamu.

    2026-08-30 14:57
  • Al-Jamaal Islamic Foundation Yampa Pongezi Sheikh Prof. Alhad Mussa Salum kwa Kuchaguliwa Tena Kuongoza JMAT-TAIFA

    Al-Jamaal Islamic Foundation Yampa Pongezi Sheikh Prof. Alhad Mussa Salum kwa Kuchaguliwa Tena Kuongoza JMAT-TAIFA

    Taasisi ya Al-Jamaal Islamic Foundation imempongeza Rais wake, Sheikh Prof. Alhad Mussa Salum, kwa kuchaguliwa tena kwa kishindo kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT) kwa kipindi kingine cha miaka 10, huku ikimuombea mafanikio katika kuendeleza juhudi za kuimarisha maridhiano, amani na umoja nchini Tanzania.

    2026-08-29 23:32
  • Nyayo za Tel Aviv katika migogoro ya ndani ya Sudan

    Nyayo za Tel Aviv katika migogoro ya ndani ya Sudan

    Kuchapishwa kwa ripoti kunathibitisha kuingilia kwa utawala wa Kizayuni katika migogoro ya ndani ya Sudan na kuunga mkono wanamgambo wa «Kikosi cha Mwitikio wa Haraka».

    2026-08-29 16:47
  • Sheikh Prof. Alhad Mussa Salum Apewa Hati ya Ushindi, Aaminiwa Tena Kuongoza JMAT-Taifa

    Sheikh Prof. Alhad Mussa Salum Apewa Hati ya Ushindi, Aaminiwa Tena Kuongoza JMAT-Taifa

    Sheikh Prof. Alhad Mussa Salum ameibuka mshindi katika uchaguzi wa JMAT Taifa na kukabidhiwa rasmi Hati ya Ushindi mjini Dodoma - Tanzania, akipewa dhamana ya kuendelea kuongoza Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT) kwa kipindi kingine.

    2026-08-28 22:34
  • Wananchi Wajitokeza kwa Wingi Kupata Huduma za Afya ya Macho Manazi Mmoja +Picha

    Wananchi Wajitokeza kwa Wingi Kupata Huduma za Afya ya Macho Manazi Mmoja +Picha

    Programu ya huduma za afya ya macho Manazi Mmoja, Dar es Salaam, imehudhuriwa na wananchi wengi kutoka maeneo mbalimbali ya jiji, huku huduma za uchunguzi wa macho na utoaji wa miwani bure zikitolewa kwa waliohitaji baada ya vipimo.

    2026-08-16 01:58
  • Wanafunzi - Banati wa Shule ya Hazrat Zainab (as) Dar es Salaam Huianza Siku Yao kwa Qur’an Tukufu, Dua na Ziyara +Picha

    Wanafunzi - Banati wa Shule ya Hazrat Zainab (as) Dar es Salaam Huianza Siku Yao kwa Qur’an Tukufu, Dua na Ziyara +Picha

    Wanafunzi wa Kike wa Shule ya Hazrat Zainab (as), Kigamboni, Dar es Salaam, huianza siku yao kwa programu ya asubuhi ya kiroho inayojumuisha kisomo cha Qur’an Tukufu, dua na ziyara, huku wakisisitiza nafasi ya Qur’an katika uongofu, nuru na baraka za maisha ya Waumini.

    2026-08-10 21:43
  • Umuhimu wa Dua katika Maisha ya Muumini Wasisitizwa katika Shule ya Imam Zain al-Abidin (as) Burundi +Picha

    Umuhimu wa Dua katika Maisha ya Muumini Wasisitizwa katika Shule ya Imam Zain al-Abidin (as) Burundi +Picha

    Wanafunzi wa Shule ya Imam Zain al-Abidin (as) nchini Burundi washiriki katika programu ya “Asubuhi ya Kiroho” kwa kusoma Dua ya Jumatatu, huku wakisisitiza umuhimu wa dua katika kuimarisha imani, kumtegemea Mwenyezi Mungu na kujenga maisha yenye maadili na utulivu wa kiroho.

    2026-08-10 21:08
  • Yemen: Jeshi la Yemen Ladai Limewasambaratisha Maafisa wa Saudi Arabia na Makundi Yake ya Kijeshi

    Yemen: Jeshi la Yemen Ladai Limewasambaratisha Maafisa wa Saudi Arabia na Makundi Yake ya Kijeshi

    Chanzo cha ngazi ya juu nchini Yemen kimesema kuwa mashambulizi ya vikosi vya Yemen dhidi ya maeneo ya Al-Mokha na Ma’rib yamelenga mikusanyiko ya maafisa wa Saudi Arabia pamoja na maghala ya silaha, huku kikisisitiza kuwa harakati zote za kijeshi za Saudi Arabia zinaendelea kufuatiliwa kwa karibu.

    2026-08-09 22:10
  • Wanafunzi wa Hawzat Zahra (sa) Washiriki katika Maombolezo ya Mtume Muhammad (saw) Jijini Dar es Salaam +Picha

    Wanafunzi wa Hawzat Zahra (sa) Washiriki katika Maombolezo ya Mtume Muhammad (saw) Jijini Dar es Salaam +Picha

    Wanafunzi wa Hawzat Zahra (sa), chini ya usimamizi wa Jamiat Al-Mustafa (s) Tanzania, wameshiriki katika Majlisi ya maombolezo ya kumbukumbu ya kufariki dunia kwa Mtume Muhammad (saw), iliyofanyika katika Msikiti wa Ali Amir al-Mu’minin (as), eneo la Magomeni, Dar es Salaam.

    2026-08-09 12:42
  • Kabla
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • Baada
Sauti ya Mashia wasio na Vyombo vya Habari.
Desktop version Mobile version

Nukuu ya "Maudhui" inaruhusiwa bila kutaja chanzo

Nastooh Saba Newsroom