-
Kocha Mkuu wa Mpira wa Miguu wa Misri: Yeyote asiyeelewa mateso ya Palestina si binadamu!
Hossam Hassan, kocha mkuu wa timu ya taifa ya Misri, katika mkutano na waandishi wa habari kabla ya mechi dhidi ya Argentina, alionyesha tena kuunga mkono Palestina.
-
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran: Kuwawajibisha Wauaji wa Kigaidi Kutafanyika kwa Mkakati wa Busara
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mohammad Reza Aref, amesema kuwa madai ya wananchi ya kuwawajibisha waliotekeleza mashambulizi ya kigaidi ni haki ya kisheria na yatatekelezwa kwa busara na mkakati wa kimkakati.
-
Hawza ya Hazrat Zainab (as) Kigamboni Yaandaa Khatmu ya Qur'an Tukufu kwa Ajili ya Shahidi Sayyid Ali Khamenei na Mashahidi wote wa Vita vya Ramadhan
Wanafunzi wa Hawza ya Hazrat Zainab (as) Kigamboni, wameshiriki katika Khatmu ya Qur'an Tukufu kwa ajili ya kuwaombea Mashahidi wa vita vya Ramadhan, akiwemo Ayatollah Sayyid Ali Hussein Khamenei.
-
Wanafunzi na Walimu wa Al-Mustafa Zanzibar Wafanya Khatmu ya Qur'an kwa ajili ya Roho za Mashahidi
Kikao maalumu cha khatma ya Qur'ani Tukufu kimefanyika katika Ofisi ya Al-Mustafa Zanzibar kwa ushiriki wa walimu na wanafunzi, kwa ajili ya kumuombea rehema Kiongozi Shahidi wa Umma wa Kiislamu, Ayatollah Sayyid Ali Khamenei, pamoja na Mashahidi wote wa Vita vya Ramadhani.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Kongo: Imam Khamenei alikuwa msukumo kwa mataifa yaliyodhulumiwa duniani
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kongo (Kongo-Brazzaville), akimtukuza mtu wa Ayatollah Sayyid Ali Khamenei, kiongozi shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, alimtaja kuwa ni msukumo kwa mataifa yaliyodhulumiwa duniani na akasisitiza kwamba kiongozi shahidi alikuwa ishara ya kusimama imara na upinzani katika uwanja wa kimataifa.
-
Kocha mkuu wa Misri alitoa ushindi dhidi ya Australia kwa Palestina
Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Misri baada ya ushindi wa timu yake dhidi ya Australia alitokwa na machozi na akasema: Watu wa Palestina hawakukata tamaa katika kuunga mkono, na mimi natoa ushindi huu kwao.
-
Rais wa Kuba: Lengo la kizuizi cha Marekani ni kujenga machafuko ya kijamii
Rais wa Kuba, akichambua kuendelea kwa vikwazo na kizuizi cha kiuchumi cha Marekani, alitangaza kwamba Havana itaibua tena suala la kufutwa kwa vikwazo hivi katika Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa.
-
Sheikh Mkuu wa TIC Ashiriki Matembezi ya Amani ya Kumuomboleza Imam Hussein (a.s) Temeke - Dar-es-salaam +Picha
Maulana Sheikh Hemed Jalala Mwakindenge ameungana na waumini na viongozi mbalimbali wa kidini katika matembezi ya amani yaliyofanyika Temeke, Dar es Salaam, kwa ajili ya kuenzi shahada ya Imam Hussein (a.s) na kusisitiza ujumbe wa haki, amani, umoja na utu kwa wanadamu wote.
-
Mamilioni ya Waombolezaji Washiriki Maandamano ya Ashura katika Zaidi ya Miji 60 nchini Nigeria
Mamilioni ya Waislamu wa Kishia na wapenzi wa Ahlul-Bayt (as) walishiriki maandamano na majlisi za kuomboleza siku ya Ashura katika mji mkuu wa Nigeria, Abuja, pamoja na zaidi ya miji 60 nchini humo, wakisisitiza kuendeleza ujumbe wa Karbala na utamaduni wa kusimama dhidi ya dhulma.
-
Muharram 1448H: Wanafunzi Mabinti wa Jamiatul Mustafa Washiriki Majlisi ya Maombolezo katika Msikiti wa Amirul Muuminin (AS), Magomeni
Wanafunzi 144 wa Jamiatul Mustafa, wakiongozana na msimamizi wao, walishiriki majlisi ya maombolezo ya Muharram katika Msikiti wa Amirul Muuminin (AS) uliopo Mgomeni, Dar es Salaam. Majlisi hiyo ilijumuisha muhadhara wa Sheikh Hujjatul Islam wal-Muslimin Aydarus, kisomo cha Qur'ani Tukufu na maombolezo ya Imam Hussein (AS), ikiwa ni sehemu ya kuhuisha ujumbe wa Karbala wa haki, uadilifu na kujitolea katika njia ya Mwenyezi Mungu.
-
Wanafunzi wa Kike wa Madrasa ya Hazrat Zaynab (a.s.) Wafanya Safari ya Mapumziko na Burudani Fun City Dar es Salaam +Picha
Wanafunzi wa kike wa Madrasa ya Hazrat Zaynab (a.s.), Kigamboni, Dar es Salaam, walifanya safari ya siku moja ya mapumziko katika kituo cha burudani cha Fun City tarehe 15 Juni 2026, ambapo walishiriki michezo mbalimbali, kula pamoja na kuswali Swala za Adhuhuri na Alasiri, kwa lengo la kurefresh akili, kuimarisha mshikamano na kujenga afya ya kiakili na kimwili.
-
Ubalozi wa Iran nchini Kenya: Kilichoharibiwa Pekee ni Sifa ya Jeshi la Marekani
Ubalozi wa Iran nchini Kenya umesema madai ya Marekani kuhusu kuzuia makombora yote ya Iran hayana msingi, ukidai kuwa mashambulizi ya Iran yaliharibu rada mbili muhimu za kijeshi za Marekani na kuathiri zaidi sifa ya jeshi la Marekani kuliko uwezo wa Iran.
-
Ijumaa | Sheikh Dkt. Swaleh Maulid Azungumzia Nafasi ya Mwanamke katika Uislamu, Ibada, na Ujenzi wa Jamii
Katika Swala ya Dhuhrain iliyoswaliwa katika Shule ya Wasichana ya Hazrat Zainab (sa) - Kigamboni, Dar-es-salaam, Sheikh Dkt. Swaleh Maulid alisisitiza kuwa mwanamke katika Uislamu ana nafasi ya ibada, uwajibikaji na mchango mkubwa katika kujenga jamii yenye maadili na maadili mema.
-
Sheikh Khalifa Khamis: Dunia Sasa Yakiri Iran ni Taifa Kuu
Sheikh Khalifa Khamis amesema dunia sasa imeitambua Iran kama taifa kubwa, akisisitiza kuwa Imam Khomeini (ra) aliupa Uislamu nguvu katika nyanja za kidini, kisiasa na kijeshi.
-
Sheikh Pro.Alhad Mussa Salum: Serikali Hupambana na Kuchukua Hatua dhidi ya Wanaotishia Maslahi Yake, Sio kwa Msingi wa Dini
Sheikh Prof.Alhad Mussa Salum: "Nchi ya Tanzania ni nchi ya Amani na sisi sote ni Watanzania, tunaishi kwa Upendo na Amani na watu wote. Uislamu ni Amani na unatufundisha kuishi kwa wema na watu wote."
-
Wamorocco kutangaza mshikamano wao na watu wa Palestina katika kumbukumbu ya 'Naksa'
Makumi ya raia wa Morocco siku ya Ijumaa walifanya maandamano mbele ya jengo la bunge la nchi yao huko Rabat, mji mkuu wa Morocco, kama ishara ya mshikamano na watu wa Palestina.
-
ABNA Yampongeza Sheikh Prof. Alhad Mussa Salum kwa Uongozi Wake wa Kuimarisha Amani na Maridhiano Nchini Tanzania
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt News Agency (ABNA) limetoa pongezi kwa Sheikh Prof. Alhad Mussa Salum kwa mchango wake katika kukuza maridhiano ya kijamii, kuimarisha umoja wa kitaifa na kudumisha amani, akiwa kielelezo cha uongozi wenye hekima na busara, katika siku muhimu ya kuzaliwa kwake.
-
Mali Yatangaza Zawadi ya Mamilioni ya Dola kwa Taarifa za Viongozi wa Kigaidi wa JNIM
Serikali ya kijeshi ya Mali imetenga dola milioni 3.5 kwa taarifa zitakazowezesha kukamatwa au kuuawa kwa kiongozi wa JNIM, Iyad Ag Ghaly, na dola milioni 2.5 kwa taarifa kuhusu naibu wake, Amadou Kouffa.
-
Barrick Gold Yalipa Faranga za CFA Bilioni 275 kwa Mali Baada ya Mvutano wa Muda Mrefu
Kampuni ya uchimbaji madini ya Barrick Gold imelipa Faranga za CFA bilioni 275 kwa Serikali ya Mali ikiwa ni sehemu ya fedha zilizokuwa zikidaiwa na mamlaka za nchi hiyo, hatua inayotajwa kuwa matokeo ya msimamo mkali wa Bamako katika kusimamia rasilimali zake za taifa.
-
Sheikh wa Mkoa wa Tabora (T I.C) Ahudhuria Baraza la Eid Lililoandaliwa na Wanawake wa Kiislamu wa BAKWATA +Picha
Sheikh wa Mkoa wa Tabora (T.I.C), Sheikh Swahibu Shabani, amehudhuria Baraza la Eid lililoandaliwa na Jumuiya ya Wanawake wa BAKWATA Tabora, akisisitiza umuhimu wa umoja na ushirikiano miongoni mwa Waislamu.
-
Burkina Faso Yakanusha Taarifa za Machafuko; Serikali Yatetea Muswada wa Kudhibiti Maeneo ya Ibada
Serikali ya Burkina Faso imetetea hatua ya kumkamata mwanazuoni wa Kiislamu Dk. Mohamed Kindou kufuatia hotuba yake kuhusu muswada wa maeneo ya ibada, huku ikisisitiza kuwa hakuna uasi dhidi ya Rais Ibrahim Traoré na kwamba wananchi bado wanaunga mkono uongozi wake.
-
Sheikh Prof. Alhad Mussa Salum Atoa Nasaha za Eid al-Adha na Hijja: Ibada Ifanywe kwa Ikhlasi na Si Kujionesha Mitandaoni
Sheikh Profesa Alhad Mussa Salum amesisitiza umuhimu wa uelewa sahihi wa ibada za Eid al-Adha na Hijja. Ameeleza kuwa kondoo ni mnyama bora zaidi kwa kuchinjwa katika Eid al-Adha endapo anapatikana, na hata nyama yake ni bora zaidi Bali Kondoo Ndiye asili ya ibada hiyo. Kuhusu Hijja, amebainisha kuwa ni ibada ya kuitikia wito wa Mwenyezi Mungu kupitia Nabii Ibrahim (as), na huleta utakaso wa dhambi kwa mja. Ameonya baadhi ya mahujaji kukosa maandalizi ya kiroho na kurejea katika dhambi baada ya Hijja. Ameikosoa tabia ya kutumia ibada ya Hijja kwa kujionesha mitandaoni kupitia Picha za “selfie”, akisisitiza kuwa ibada ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu pekee. Amemalizia kwa kusisitiza msingi wa ikhlasi na kuepuka riyaa katika ibada zote.
-
Hafla ya Ugawaji Zawadi kwa Washindi wa Mashindano ya Uandishi wa Muhtasari "Summary Writing" Yafanyika Kigamboni - Dar-es-salaam
Katika hafla iliyofanyika katika shule ya wasichana ya Kigamboni, washindi wa mashindano ya kuandika muhtasari kuhusu “Shahada ya Ayatollah Sayyid Ali Khamenei (ra)” walikabidhiwa zawadi maalum katika mwendelezo wa masomo ya Qur’an chini ya usimamizi wa Bi. Fatma Ma‘suma, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha elimu, ubunifu na ushindani wenye tija kwa wanafunzi.
-
Msaada wa mwanafikra wa Algeria kwa Iran; Wafuasi wa utamaduni wa Alawi wanasimama dhidi ya udhalimu
Yahya Abu Zakaria aliandika: Wote waliopata dini yao kutoka kwa zuriya safi na utamaduni wa Alawi wanasimama dhidi ya udhalimu, Amerika na Israel. Siri ya jambo hii ni nini?
-
Wafuasi wa Ahlul-Bayt (as) Mjini Nakuru - Kenya Waliupokea Mwezi wa Ibada na Toba - Mwezi Mtukufu wa Ramadhan kwa Imani, Umoja na Mshikamano
Waislamu wa Nakuru, wafuasi wa Ahlul-Bayt, walikusanyika katika Ijumaa ya kwanza ya Ramadhan kwa upendo na mshikamano, wakisherehekea kuingia Mwezi wa: Toba, Rehema na Kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu kupitia ibada mbalimbali.
-
EAC Yafanya Mazungumzo ya Kuondoa Vizuizi vya Biashara na Kuongeza Ukuaji wa Kanda
EAC imezindua kikao cha kiwango cha juu Kigali, Rwanda, kukabiliana na vizuizi vya biashara vya ndani, kuboresha utekelezaji wa Umoja wa Forodha na Soko la Pamoja, na kuongeza ukuaji wa kibiashara wa kikanda, huku wanasiasa na sekta binafsi wakisisitiza uungwaji mkono wa hatua za haraka na uratibu bora.
-
Faida za Mwezi Mtukufu wa Ramadhan | Faida za Kimwili, Kiroho na Kijamii +Video
Mwezi Mtukufu wa Ramadhan unaleta faida nyingi kwa Waislamu: kimwili, kwa kuimarisha afya, kupunguza sumu mwilini na kuendeleza nidhamu ya mwili; kiroho, kwa kuimarisha imani, kujenga taqwa na kukuza tafakari na uhusiano na Mwenyezi Mungu; na kijamii, kwa kuimarisha mshikamano, kuongeza huruma kwa maskini na kukuza maadili mema miongoni mwa jamii.
-
Darsa ya Ramadhan | Al-Haj Dkt. Saleh Maulid Asisitiza Imani na Matendo Mema Katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhan
Alhaj Dkt. Saleh Maulid, akizungumza baada ya Sala ya Dhuhri katika Chuo cha Kisayansi cha Al-Mustafa International Foundation- Tanzania, alisisitiza umuhimu wa imani na matendo mema katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhan, akibainisha kwamba matendo mema kama usomaji wa Qur’an, sala za usiku, utoaji wa sadaka na kusaidia maskini huimarisha Taq'wa, subira, shukrani na malezi ya kiroho miongoni mwa Waumini.
-
Kumfuata Mtume(s) kama Kielelezo Bora | Wanafunzi wa Hawzat Hazrat Zainab(sa) Tanzania Waadhimisha Ramadhan kwa Ratiba Maalum ya Usomaji wa Qur’an
Wakiongozwa na azma ya kumfuata Mtume (saww) kama kielelezo bora cha maisha ya Kiislamu, wanafunzi wa Hawzat Hazrat Zainab (sa) Kigamboni wameanzisha ratiba maalum ya kila siku ya usomaji wa Qur’an Tukufu katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhan, kwa lengo la kuimarisha malezi yao ya kiimani na kunufaika kikamilifu na baraka za Mwezi huo Mtukufu, ikiwemo faida za kimwili, kiroho na kijamii.
-
Jamiatul Mustafa - Dar-es-salaam | Funga za Viungo Zasisitizwa kama Njia ya Kufikia Taq'wa katika Kongamano la Kielimu +Picha
Akitoa mada katika kongamano la kielimu lililofanyika katika Chuo cha Jamiatul Mustafa (s) Jijini Dar es Salaam - Tanzania, Sheikh Dr.Raihan alisisitiza kuwa funga za viungo ni njia muhimu ya kufikia taqwa, kuimarisha nidhamu ya nafsi na kukuza maadili ya kijamii miongoni mwa waumini.