-
Msaada wa mwanafikra wa Algeria kwa Iran; Wafuasi wa utamaduni wa Alawi wanasimama dhidi ya udhalimu
Yahya Abu Zakaria aliandika: Wote waliopata dini yao kutoka kwa zuriya safi na utamaduni wa Alawi wanasimama dhidi ya udhalimu, Amerika na Israel. Siri ya jambo hii ni nini?
-
Wafuasi wa Ahlul-Bayt (as) Mjini Nakuru - Kenya Waliupokea Mwezi wa Ibada na Toba - Mwezi Mtukufu wa Ramadhan kwa Imani, Umoja na Mshikamano
Waislamu wa Nakuru, wafuasi wa Ahlul-Bayt, walikusanyika katika Ijumaa ya kwanza ya Ramadhan kwa upendo na mshikamano, wakisherehekea kuingia Mwezi wa: Toba, Rehema na Kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu kupitia ibada mbalimbali.
-
EAC Yafanya Mazungumzo ya Kuondoa Vizuizi vya Biashara na Kuongeza Ukuaji wa Kanda
EAC imezindua kikao cha kiwango cha juu Kigali, Rwanda, kukabiliana na vizuizi vya biashara vya ndani, kuboresha utekelezaji wa Umoja wa Forodha na Soko la Pamoja, na kuongeza ukuaji wa kibiashara wa kikanda, huku wanasiasa na sekta binafsi wakisisitiza uungwaji mkono wa hatua za haraka na uratibu bora.
-
Faida za Mwezi Mtukufu wa Ramadhan | Faida za Kimwili, Kiroho na Kijamii +Video
Mwezi Mtukufu wa Ramadhan unaleta faida nyingi kwa Waislamu: kimwili, kwa kuimarisha afya, kupunguza sumu mwilini na kuendeleza nidhamu ya mwili; kiroho, kwa kuimarisha imani, kujenga taqwa na kukuza tafakari na uhusiano na Mwenyezi Mungu; na kijamii, kwa kuimarisha mshikamano, kuongeza huruma kwa maskini na kukuza maadili mema miongoni mwa jamii.
-
Darsa ya Ramadhan | Al-Haj Dkt. Saleh Maulid Asisitiza Imani na Matendo Mema Katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhan
Alhaj Dkt. Saleh Maulid, akizungumza baada ya Sala ya Dhuhri katika Chuo cha Kisayansi cha Al-Mustafa International Foundation- Tanzania, alisisitiza umuhimu wa imani na matendo mema katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhan, akibainisha kwamba matendo mema kama usomaji wa Qur’an, sala za usiku, utoaji wa sadaka na kusaidia maskini huimarisha Taq'wa, subira, shukrani na malezi ya kiroho miongoni mwa Waumini.
-
Kumfuata Mtume(s) kama Kielelezo Bora | Wanafunzi wa Hawzat Hazrat Zainab(sa) Tanzania Waadhimisha Ramadhan kwa Ratiba Maalum ya Usomaji wa Qur’an
Wakiongozwa na azma ya kumfuata Mtume (saww) kama kielelezo bora cha maisha ya Kiislamu, wanafunzi wa Hawzat Hazrat Zainab (sa) Kigamboni wameanzisha ratiba maalum ya kila siku ya usomaji wa Qur’an Tukufu katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhan, kwa lengo la kuimarisha malezi yao ya kiimani na kunufaika kikamilifu na baraka za Mwezi huo Mtukufu, ikiwemo faida za kimwili, kiroho na kijamii.
-
Jamiatul Mustafa - Dar-es-salaam | Funga za Viungo Zasisitizwa kama Njia ya Kufikia Taq'wa katika Kongamano la Kielimu +Picha
Akitoa mada katika kongamano la kielimu lililofanyika katika Chuo cha Jamiatul Mustafa (s) Jijini Dar es Salaam - Tanzania, Sheikh Dr.Raihan alisisitiza kuwa funga za viungo ni njia muhimu ya kufikia taqwa, kuimarisha nidhamu ya nafsi na kukuza maadili ya kijamii miongoni mwa waumini.
-
Simulizi ya Mabadiliko ya maisha ya Muimba Mziki na Rapa kutoka Madagascar baada ya kuhudhuria katika Majlisi ya Maombolezo ya Imam Hussein(a.s)+Video
Rapa mmoja kutoka Madagascar ameeleza kusilimu kwake baada ya kuhudhuria Majlisi ya Maombolezo ya Imam Hussein ibn Ali (as), akigusiwa na uzoefu wa kiroho wa hafla hiyo.
-
Kikao cha Kiakhlaq cha Wanafunzi na Rais wa Jamiat Al-Mustafa Tanzania, Dk. Ali Taqavi +Picha
Siku ya Jumatano, 18 Februari 2026, Dk. Ali Taqavi, Rais wa Chuo cha Al-Mustafa International Foundation- nchini Tanzania, alifanya mkutano na wanafunzi wa taasisi hiyo. Katika kikao hicho, alisisitiza umuhimu wa elimu yenye maadili na uwajibikaji, akahimiza kuimarishwa kwa mazingira ya masomo na mawasiliano ya karibu kati ya uongozi na wanafunzi.
-
Sheikh Dr.Alhad Mussa Salum: Swaumu ya Ramadhan si adhabu, bali ni Tiba ya Kiroho na Kimwili
Sheikh Dr. Alhad Mussa Salum anafafanua kuwa swaumu ya mwezi mtukufu wa Ramadhan si adhabu, bali ni ibada iliyojaa huruma ya Mwenyezi Mungu. Kufunga kunalenga kutuponya kiroho na kimwili, kuimarisha nafsi, na kutufundisha subira, kama ambavyo Daktari (Tabibu) humlazimisha mgonjwa kunywa dawa chungu, lakini sio kwa lengo la kumuadhibu, bali ili apone. Swaumu ni fursa ya kujenga uhusiano thabiti baina ya Mja na Mola wake (swt) na kupata manufaa mapana katika maisha yetu.
-
Ubalozi wa Iran Nchini Tanzania Waadhimisha Miaka 47 ya Mapinduzi ya Kiislamu +Video
Ubalozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Nchini Tanzania umeadhimisha miaka 47 ya ushindi wa Iranian Revolution, huku Balozi Mohammad Javad Hemmatpanah akisisitiza kuimarika kwa uhusiano wa kihistoria kati ya Iran na Tanzania na kuahidi kupanua ushirikiano katika biashara, teknolojia na maendeleo.
-
Malawi | Mjadala wa Kielimu kuhusu Mkombozi wa Ulimwengu katika Mtazamo wa Dini Mbalimbali +Video
Wanazuoni wa Kikristo na Kiislamu nchini Malawi wamekutana katika mjadala wa kielimu kujadili dhana ya Mkombozi wa Ulimwengu kwa mujibu wa mitazamo ya dini zao. Katika mjadala huo, washiriki walieleza kuwa dini zote zinabeba tumaini la kuja kwa Kiongozi wa haki atakayerejesha amani, uadilifu na maadili katika jamii. Kwa mujibu wa itikadi ya Kiislamu, Mkombozi huyo ni Imam Mahdi (atfs), anayengojewa kudhihiri kwa amri ya Mwenyezi Mungu ili kuujaza ulimwengu kwa haki na uadilifu kama ulivyojaa dhulma. Mjadala huo umeelezwa kuwa hatua muhimu katika kuimarisha mazungumzo ya kidini, mshikamano na uelewano miongoni mwa waumini wa dini mbalimbali.
-
Vijana 250 Washiriki Semina ya Wajibu Katika Kipindi cha Ghaibah Kubwa +Dodoma
Semina hiyo iliyoandaliwa na wanafunzi wa Kishia wa vyuo vikuu mjini Dodoma kwa ushirikiano na Bilal Muslim Mission of Tanzania ilijikita katika kuwakumbusha vijana wajibu wao wa kiimani, kimaadili na kijamii katika kipindi cha Ghaibah ya Imam Mahdi (a.t.f.s), huku takribani vijana 250 wakishiriki.
-
Sheikh Dr.Alhad Mussa Salum aimarisha Falsafa ya Udugu wa Kibinadamu Katika Kongamano la Kielimu Tanzania +Picha
Kikao cha 5 cha Kielimu kilichojadili mada ya “Mkombozi Katika Mitazamo ya Dini Mbalimbali: Tumaini la Viumbe Wote” kilifanyika tarehe 13 Februari 2026, kikiandaliwa na Jamiat Al-Mustafa International Foundation – Tanzania. Kongamano liliwakutanisha wanazuoni na wawakilishi wa dini mbalimbali kwa lengo la kuimarisha mshikamano, maridhiano na amani. Sheikh Dr. Alhad Mussa Salum, Mwenyekiti wa JMAT-TAIFA, alisisitiza kupinga ukabila, ubinafsi na umimi, na kuhimiza mazungumzo ya heshima kati ya dini. Alieleza kuwa dini zote zinapaswa kutambua udugu wa kibinadamu na kushirikiana kwa manufaa ya mustakabali mwema wa wanadamu. Pia aligusia dhana ya Mkombozi, akieleza nafasi ya Imam Mahdi (as) na Mtume Muhammad (saww) kama muombezi mkuu Siku ya Kiyama.
-
Mkutano wa Mshikamano na Wapalestina Mbele ya Bunge la Moroko
Jioni ya Ijumaa, mji mkuu wa Morocco, Rabat, ulishuhudia mkutano wa kuonesha mshikamano na watu wa Palestina huko Gaza na kudai kuingizwa kwa misaada ya kibinadamu katika eneo hili linalozingirwa na utawala wa Kizayuni.
-
Maadhimisho ya Kuzaliwa kwa Imam Mahdi (AS): Vijana Wakumbushwa Wajibu wa Kuijenga Jamii ya Uadilifu katika Kipindi cha Ghaiba
Katika mnasaba wa maadhimisho ya Kuzaliwa kwa Imam Mahdi (AS), Waislamu wa Shia na Sunni walikusanyika kujadili kuhusu Mwokozi wa Ulimwengu na wajibu wa Waumini katika kipindi cha Ghaiba. Khatibu Sheikh Suleimani Abdully aliwakumbusha vijana juu ya umuhimu wa kumcha Mwenyezi Mungu, kushukuru neema Zake na kujenga tabia njema ili kuandaa jamii yenye utu, uadilifu na iliyoepukana na dhulma na ufisadi.
-
Maulana Sheikh Hemed Jalala: "Uislamu ni Ushindi, Izza na Umoja wa Umma"
Sheikh Hemed Jalala: Uislamu wa kweli ulioshikamana na thaqafa ya Karbala unamtambua adui, na unapambana na dhulma ya adui, na kusimamia haki na uadilifu. Uislamu una nguvu kwa sababu una uongozi, wanazuoni na marjaa wanaoupa Umma mwelekeo hata katika nyakati ngumu.
-
Rais Samia Ampokea Rais Museveni Ikulu Dar es Salaam kwa Ziara ya Kikazi ya Siku Moja +Picha
Ziara hiyo inalenga kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia, kiuchumi na kijamii kati ya Tanzania na Uganda.
-
Sheikh Ibrahim Zakzaky (H) Ahudhuria na Kuongea na Maelfu wa Waumini Katika Maadhimisho ya Nisfu Sha’aban Abuja, Nigeria
Kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, Kiongozi wa Harakati za Kiislamu Nigeria, Seikh Ibrahim Zakzaky (H), amehudhuria Maadhimisho ya Nisfu Sha’aban (Nusu ya Mwezi wa Sha'ban) jijini Abuja kwa mara ya pekee mwaka huu, yakilenga kusherehekea mazazi ya Imam Mahdi (a.j.t.f.s) pamoja na kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa kwa Sheikh Zakzaky ambayo huangukia tarehe 15 Sha’aban.
-
Ziara ya Mwenyekiti wa JMAT-TAIFA Sheikh Dkt.Al-Had Mussa Salum Nchini Misri Yaleta Mafanikio kwa Maendeleo ya Vijana
Ziara ya Sheikh Dkt. Alhad Mussa Salum nchini Misri imefungua ukurasa mpya wa ushirikiano wa kimataifa katika elimu, ajira na maendeleo ya vijana kupitia JMAT.
-
Tanzania Yakamata Pakiti 20 za Skanka Zenye Kilogramu 20 Kwenye Bus la Kimataifa, Temeke - Dar-es-salaam
Mamlaka ya DCEA imekamatwa pakiti 20 za skanka zenye uzito wa kilo 20.03 zilizofichwa kwenye balo la mitumba ndani ya bus la Scania la King Masai Tours, lenye namba za usajili AAM 297 CA, likisafiri kati ya Nampula, Msumbiji na Dar es Salaam. Watuhumiwa waliokamatwa ni Amasha Iddi Mrisho (40) kutoka Dar es Salaam na Seleman Juma Ally (32) raia wa Msumbiji. Uchunguzi na kesi za kiutumishi zinaendelea.
-
Malawi | Baraza la Kumbukumbu ya Kufariki kwa Hadhrat Ibrahim (a.s), Mwana wa Mtume Muhammad (s.a.w.w) +Picha
Baraza la kumbukumbu ya kufariki kwa Hadhrat Ibrahim (a.s), mwana wa Mtume (saww), limefanyika Alhamisi, 08/01/2026, katika Shule ya Imam Al-Hadi(as). Baraza hili lilihudhuriwa na wanafunzi na walimu, na Sheikh Abdulrahman Kachera alihutubia katika mnasaba huu. Katika hotuba yake, alisisitiza upendo kwa Ahlul-Bayt (as) uliosisitizwa na Qur'an Tukufu iliposema: (قُل لَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ أَجْرًا إِلَّا الْمَوَدَّةَ فِي الْقُرْبَىٰ), historia ya watoto wa Mtume (saww), ndoa ya Hadhrat Ma'riya al-Qibtiyya, na kufariki kwa Hadhrat Ibrahim (a.s) akiwa mtoto kiumri. Wahudhuriaji walikumbuka tukio hilo kwa huzuni na kuimarisha dhamira ya kufuata maadili na mafundisho ya Ahlul-Bayt (a.s).
-
Maulidi ya Imam Ali (a.s.) Yaadhimishwa katika Madrasa ya Imam Ali (a.s) Vikindu - Tanzania + (Video - Picha)
Baraza la Maulid lilianza kwa kisomo kitukufu cha Aya za Qur’ani Tukufu, kikifuatiwa na maneno ya utangulizi yaliyobainisha umuhimu wa tukio hili tukufu na nafasi ya pekee ya Imam Ali (a.s.) katika Uislamu, kama mfano wa haki, ucha-Mungu, ushujaa na elimu.
-
Waziri Mkuu Dkt.Mwigulu Nchemba Afungua Skuli ya Sekondari Chukwani Zanzibar Katika Maadhimisho ya Miaka 62 ya Mapinduzi +Picha
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba, amefungua rasmi Skuli ya Sekondari Chukwani Zanzibar iliyogharimu shilingi bilioni 6.1, katika maadhimisho ya miaka 62 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, akisisitiza umuhimu wa uwekezaji katika elimu kwa maendeleo ya taifa.
-
Rais Samia Afanya Mazungumzo na Viongozi wa Wizara ya Ulinzi na JKT Zanzibar
Mazungumzo hayo yamezingatia masuala mbalimbali ya usalama, ulinzi wa taifa, na maendeleo ya majeshi, huku akisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya majeshi na wananchi katika kuhakikisha amani na utulivu wa taifa.
-
Ujumbe wa rambirambi wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (a.s) Kufuatia Kifo cha Mwanachuoni wa Afrika Mashariki Sheikh Ali Mayunga
Marehemu alikuwa na mchango mkubwa katika nyanja za kielimu, ikiwemo nafasi yake kama Katibu wa Baraza la Wanazuoni wa Ahlul-Bayt (a.s), na alikuwa miongoni mwa waliotafsiri Qur’an Tukufu kwa lugha ya Kiswahili iliyoitwa Tafsiri Al-Mubin.
-
Ayatollah Dkt. Abbasi, kupitia ujumbe wake, amempa pole Hujjatul-Islam wal-Muslimin Sayyid Aref Naqavi kufuatia kufariki dunia kwa mke wake mpendwa
Ayatollah Dkt. Abbasi ametoa ujumbe wa rambirambi kwa Hujjatul-Islam wal-Muslimin Sayyid Aref Naqavi kufuatia kufariki dunia kwa mke wake, akimuomba Mwenyezi Mungu amrehemu marehemu na awajaalie wafiwa subira na malipo mema.
-
Sa‘yi kati ya Safa na Marwa: Alama ya Imani na Nguzo Muhimu ya Hija na Umra
Aya hii tukufu inathibitisha kuwa sa‘yi baina ya Safa na Marwa ni sehemu muhimu ya ibada ya Hija na Umra, na kwamba hakuna dhambi wala lawama katika kuitekeleza. Kinyume chake, ni ibada iliyoidhinishwa na Qur’ani na kusisitizwa na Sunna ya Mtume ﷺ, na aya imekuja mahsusi kuondoa shaka na uzito uliokuwepo katika nyoyo za watu kuhusu ibada hii.
-
Viongozi wa Serikali na Jeshi la Polisi Jijini Mwanza Watunukiwa Tuzo za Amani Kupitia Kamati ya Maandalizi ya Maridhiano Day 2026
Kamati ya Maandalizi ya Maridhiano Day 2026 imetoa tuzo za heshima kwa viongozi wa Mkoa wa Mwanza pamoja na Jeshi la Polisi, kama ishara ya kutambua mchango wao katika kudumisha amani, mshikamano na utulivu wa kijamii. Tuzo hizo zilitolewa katika hatua inayolenga kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi za serikali, vyombo vya ulinzi na jamii kwa ujumla kuelekea maandalizi ya tukio hilo muhimu la Maridhiano Day 2026.
-
Bilal Tanga: Ujenzi wa Jengo la Ghorofa Tisa Kutoa Suluhisho la Changamoto ya Nafasi kwa Hawza
Taasisi ya Bilal Tanga inaendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuimarisha shughuli za tabligh na elimu ya juu ya Hawza, ikiwa ni sehemu ya dhamira yake ya kuinua elimu ya Kiislamu na kuwahudumia waumini. Katika muktadha huo, ujenzi wa jengo jipya la ghorofa tisa umebeba matumaini makubwa ya kutatua changamoto ya upungufu wa nafasi na kuboresha mazingira ya masomo na dawah.