Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul Bayt (AS) -ABNA- Ayatollah Ramezani, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (AS), alisafiri kwenda Côte d'Ivoire (Ivory Coast), nchi iliyopo upande wa Afrika Magharibi, kwa mwaliko wa viongozi wa kidini wa Côte d'Ivoire (Ivory Coast).
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (AS) alipowasili uwanja wa ndege wa Côte d'Ivoire, alifanya mkutano mfupi na Bogere Mambe, Waziri wa nchi hiyo.
Mkutano wa Ayatollah Ramadhani na Waziri Mkuu wa Côte d'Ivoire
Katika mkutano huu, Amir Hossein Nikbin, Balozi wa Iran nchini Côte d'Ivoire, alifafanua malengo ya safari ya Ayatollah Ramezani katika nchi hiyo kwa Waziri Mkuu wa Côte d'Ivoire.
Inafahamika kwamba mikutano na wanazuoni, wataalamu, wasomi na vijana wa Côte d'Ivoire ni mojawapo ya mipango ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul Bayt (AS) katika ziara yake nchini humo.
Your Comment