Kwa Mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (AS) –ABNA– Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Abbas Araghchi, amekutana na mabalozi kadhaa wa nchi za Amerika ya Kusini wanaowakilisha mataifa yao mjini Tehran, pembeni mwa mkutano wa mabalozi na wakuu wa ujumbe wa nchi za kigeni walioidhinishwa nchini Iran.
Kwa mujibu wa Shirika la Habari la IRNA, mkutano huo ulipambwa na ishara ya urafiki ambapo mabalozi wa Uruguay na Brazil, sambamba na shamrashamra za mashindano ya Kombe la Dunia la Mpira wa Miguu, walimkabidhi Waziri Araghchi jezi za timu za taifa za nchi zao kama zawadi.
Katika mazungumzo hayo, Waziri Araghchi alisisitiza kuwa kuna fursa na uwezo mkubwa wa kuimarisha ushirikiano kati ya Iran na mataifa ya Amerika ya Kusini, akieleza umuhimu wa kupanua na kuimarisha uhusiano huo katika nyanja mbalimbali kwa manufaa ya pande zote.
Your Comment