9 Julai 2026 - 16:01
Qalibaf: Mazishi ya Kihistoria ya Kiongozi Shahidi nchini Iraq Yalikuwa Tamko la Kulipiza Damu Yake

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema mazishi ya kihistoria ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu aliyeuawa shahidi nchini Iraq hayakuwa tukio la maombolezo pekee, bali yalikuwa tamko la kuendeleza njia yake na kulipiza damu yake.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) –ABNA– Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema kuwa mazishi makubwa ya kihistoria ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu aliyeuawa shahidi nchini Iraq hayakuwa hafla ya kuaga na kuomboleza pekee, bali yalikuwa tamko la wazi la kuunga mkono misimamo na njia yake, pamoja na azma ya kulipiza damu yake.

Katika ujumbe wa shukrani alioutuma kwa wananchi wa Iraq siku ya Alhamisi, Qalibaf alisema mamilioni ya waombolezaji waliokusanyika katika miji mitakatifu ya Najaf na Karbala walitoa ujumbe wa mshikamano kwa kusaini kwa vitendo tamko la kuendeleza njia ya kiongozi huyo na kuimarisha Muqawama (Mhimili wa Upinzani).

Qalibaf alieleza kuwa marehemu alitumia maisha yake yote kuimarisha umoja wa Waislamu, kulinda heshima ya Umma wa Kiislamu, kutetea haki na ukweli, pamoja na kusimama bega kwa bega na wanyonge dhidi ya kile alichokiita ubeberu unaoongozwa na Marekani na kupambana na Uzayuni.

Aidha, alisema mazishi hayo yalibeba ujumbe wa wazi kwamba Mhimili wa Upinzani hauwezi kushindwa wala kuvunjwa, na kwamba watu huru wa dunia – Waislamu, Wakristo, Mashia, Masunni, Waarabu, Wakurdi na Waturkmen – wanaendelea kuwa na mshikamano katika kutetea haki.
Qalibaf aliwashukuru Marjaa wa dini, wanazuoni wa Kishia na Kisunni, viongozi wa Kikristo, wasimamizi wa maeneo matakatifu ya Najaf na

Karbala, viongozi wa makabila, waandaaji wa mawakibu, serikali na bunge la Iraq, vikosi vya usalama, jeshi, Hashd al-Shaabi na wananchi wote wa Iraq kwa kuandaa mazishi aliyoyataja kuwa ya kihistoria na ya kukumbukwa milele, huku akiiombea Iraq na wananchi wake amani, heshima na uthabiti.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha