19 Julai 2026 - 17:22
Msemaji wa Serikali ya Iran: Mkakati Wetu Unategemea Uwezo wa Ndani na Uungwaji Mkono wa Wananchi

Msemaji wa Serikali ya Iran, Fatemeh Mohajerani, amesema kuwa Mkakati wa Serikali unategemea Uwezo wa Ndani na Uungwaji Mkono wa Wananchi, akisisitiza kuwa Umoja wa Kitaifa wa Wananchi wa Iran utaiwezesha Nchi hiyo kupata Ushindi dhidi ya Maadui wanaolenga Maisha ya Watu, Shule na Hospitali.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Msemaji wa Serikali ya Iran, Fatemeh Mohajerani, amesisitiza kuwa Mkakati wa Serikali ya Iran umejikita katika kutegemea Uwezo wa Ndani wa Nchi pamoja na Uungwaji Mkono wa Wananchi.
 

Umoja wa Kitaifa Chanzo cha Ushindi Dhidi ya Maadui
Mohajerani amesema kuwa Mkakati huo unalenga kuwawezesha Wananchi wa Iran, kupitia Umoja wao wa Kitaifa, kupata Ushindi madhubuti dhidi ya Maadui ambao wameyalenga Maisha ya Watu, Shule na Hospitali.
 

Wananchi wa Bushehr Walinzi wa Utambulisho na Uhuru wa Iran

Akizungumza wakati wa Ziara yake katika Mji wa Bushehr, Kusini mwa Iran, na kukagua Maeneo yaliyoathiriwa na Mashambulizi ya hivi karibuni ya Marekani, Mohajerani amesema kuwa Wananchi wa Iran, hususan Wakazi Mashujaa wa Bushehr, ni Walinzi wa Utambulisho na Uhuru wa Nchi yao.

Kuijenga Iran kwa Juhudi na Azma
Msemaji huyo wa Serikali ameongeza kuwa Wananchi wa Iran, kupitia Azma na Juhudi zao, wataendelea kuilinda Nchi yao na kuijenga kwa namna bora zaidi.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha