Mshikamano
-
Mwenyekiti wa Baraza la Sera za Maimamu wa Ijumaa nchini:
"Swala ya Ijumaa ni nguzo ya Umoja wa Kitaifa - Lazima iwafikie watu wa makundi yote"
Mwenyekiti wa Baraza la Sera za Maimamu wa Ijumaa nchini: "Swala ya Ijumaa inapaswa kuwa ya watu wote na kuakisi umoja wa kitaifa."Akiangazia umuhimu wa nafasi ya wananchi na ushirikishi mpana katika Swala ya Ijumaa, mwenyekiti huyo alisema: “Makamati ya Swala ya Ijumaa yanapaswa kwa ubunifu na upangaji madhubuti, kuweka mazingira yanayowezesha ushiriki wa watu wa makundi yote ya jamii — kuanzia wanafunzi wa vyuo vikuu, walimu na wasomi, hadi wafanyakazi wa viwandani na wakulima.” Aliongeza kuwa kwa njia hii, ibada hii ya kiroho na kisiasa itakuwa ni taswira kamili ya mshikamano na umoja wa kitaifa.
-
Dkt. Pezeshkian: Umoja na Mshikamano Nguvu Yetu Dhidi ya Maadui
Alionya dhidi ya kuvunjika kwa mshikamano wa taifa na urafiki wa majirani, akibainisha kuwa hayo ni malengo ya Marekani na Israel ya kuleta mgawanyiko miongoni mwa Waislamu na nchi za jirani.
-
Mazuwwari wa Afghanistan: Warithi wa Karbala, Sio Vipande vya Mchezo wa Chesi
Ukosoaji wa Matusi ya Gazeti la Ettelaat-e-Rooz dhidi ya Waislamu wa Kishia wa Afghanistan
Katikati ya wimbi la maandiko yenye upendeleo ambayo, kwa kisingizio cha utafiti, yanadhalilisha imani na uelewa wa Waislamu wa Kishia wa Afghanistan, ni lazima kukumbusha ukweli: ukweli wa uhusiano wa kihistoria na wa kina kati ya mataifa mawili ya Iran na Afghanistan, ambao katika nyanja za mapambano, ulinzi na mshikamano, daima wamesimama bega kwa bega — na lengo la pamoja la maadui wao limekuwa kuvunja mshikamano huu.
-
Washairi wa Kimataifa Waungana na Washairi wa Iran Kuadhimisha Mashahidi katika Usiku wa Mashairi ulioitwa: “Wasafiri wa Alfajiri”
Katika hafla hii, washairi walitumia lugha ya fasaha na yenye kugusa hisia kueleza hadhi ya mashahidi, wakisoma mashairi yenye maudhui ya hisia, ujasiri na ucha Mungu, ambayo yalionyesha sio tu upendo wa kibinadamu bali pia dhamira ya kijamii, mwamko wa kiutamaduni na mshikamano wa kitaifa.
-
Zanzibar | Rais Mwinyi Atoa Wito wa Kuendelea Kuliombea Taifa Amani
Alisema: “Kila ninapopata nafasi ya kuzungumza na Wananchi, nitaendelea kusisitiza juu ya umuhimu wa amani na utulivu kwa sababu ndiyo njia pekee ya kuhakikisha tunapata maendeleo.”
-
Idadi ya waliouawa Gaza imefikia watu 54,880 | Hali ni mbaya sana na watu wengi wanahitaji msaada wa kibinadamu
Hali ya Gaza inaendelea kuwa mbaya kutokana na mashambulizi ya hivi karibuni ya utawala wa Kizayuni. Wizara ya Afya ya Palestina imetangaza kuwa ndani ya saa 24 zilizopita watu 108 wamepoteza maisha na wengine 393 wamejeruhiwa. Jumla ya waliofariki tangu kuanza kwa mashambulizi haya imezidi kufikia watu 54,000. Hali hii inahitaji mshikamano wa kimataifa ili kusitisha ukatili huu na kuanzisha mazungumzo ya amani.
-
Shahriari: Vitabu Vipya vya Jumuiya ya Kimataifa ya Taqrib ya Madhehebu za Kiislamu, vinaangazia Umoja na Ustaarabu Mpya wa Kiislamu
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Taqrib baina ya Madhehebu ya Kiislamu, Dkt. Hamid Shahriari, alieleza kuwa: “Kwa bahati nzuri, kwa kuweka vitabu katika mfumo wa kielektroniki kupitia tovuti ya maonyesho ya vitabu, mazingira mazuri yameandaliwa kwa ajili ya kutoa huduma kwa wadau na wageni wanaopendelea kufanya manunuzi yao kwa njia za kidijitali.”
-
Mkutano na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Dkt. Batlida Burian, pamoja na baadhi ya Masheikh wa Kishia na Kisunni.
"Tanga ni mfano wa kuigwa kwa utulivu wa kidini. Tuendelee kudumisha hali hii na kushirikiana kwa ajili ya maendeleo ya jamii yetu."
-
Kuimarishwa kwa uhusiano wa kibiashara kati ya Iran na Afrika / Isfahan kuwa mwenyeji wa Mkutano wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Iran na Afrika
Waziri wa Viwanda wa Mali, katika hafla ya kufunga Mkutano wa Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Iran na Afrika, alisisitiza umuhimu wa kuimarisha uhusiano wa kibiashara na uwekezaji wa pamoja katika nyanja mbalimbali. Alieleza matumaini kwamba mkutano huu utasababisha mshikamano na maingiliano yenye tija kati ya pande hizo mbili, na akatambua kuwa sekta binafsi ina nafasi muhimu katika mchakato huu.
-
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Umoja wa Madhehebu ya Kiislamu:
Udhalilishaji wa hivi karibuni wa mambo matukufu ya Waislamu wa Kisunni una nyanja tata zaidi
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kudumisha Umoja wa Madhehebu ya Kiislamu akilaani udhalilishaji wa mambo matukufu ya Waislamu wa Kisunni alisema: Udhalilishaji wa hivi karibuni una nyanja tata zaidi, na inatarajiwa kutoka kwa viongozi wa masuala haya kuchukua hatua za kuzuia kurudiwa kwa maafa kama haya.
-
Serikali ya Muda ya Afghanistan Yatoa Pole kwa Watu wa Iran Kufuatia Mlupuko wa Bandar Abbas
Baada ya mlipuko uliotokea jana katika Bandari ya Shahid Rajaei iliyopo katika Mji wa Bandar Abbas, Serikali ya Muda ya Afghanistan, sambamba na mataifa mengi duniani, imetoa pole kwa watu na Serikali ya Iran.
-
Dr. Ali Taqavi, Mwakilishi wa Jamiat Al-Mustafa (s)Tanzania, akiambatana na Sheikh Dr. Alhad Mussa Salum watembelea uwanja wa Michezo Zanzibar + Picha
Uislamu umesisitiza Umoja wa Kiislamu, na madhehebu yote ya Kiislamu yanaunganishwa na Umoja wa Kiislamu, na Kibla cha Waislamu wote ni kimoja, na Qur'an ndio Kitabu chao na Muongozo wao.
-
Mwenyekiti wa Baraza la Ulamaa wa Pakistan: Mahali pa mwisho pa mradi wa "Israeli Kubwa" ni Makka na Madina
Mkuu wa Baraza la Ulamaa wa Pakistan alionya kwamba mradi wa "Israeli Kubwa" unatafuta udhibiti wa mwisho juu ya Madina na Makka.
-
Fat'wa Mpya: Kuitetea Palestina na Jihad dhidi ya Utawala wa Kizayuni ni Wajibu Ayn (jambo la faradhi kwa kila Mtu)
Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu Ulimwenguni umetoa Fat'wa kuhusu Wajibu wa Jihadi katika kuunga mkono Ghaza na kusisitiza kuwa, Jihadi dhidi ya utawala wa Kizayuni na mamluki na askari wake wanaohusika na mauaji ya halaiki ya watu wa Ghaza katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina ni wajibu mutlaki (unaomgusa kila mtu).