Haki
-
Msemaji wa Jeshi la Iran: Vyombo vya Majini Vinavyotumika Dhidi ya Wananchi wa Iran Haviwezi Kupita Katika Bahari ya Hormuz
“Udhibiti wa Bahari ya Hormuz uko mikononi mwa Majeshi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Vifaa vinavyotumika dhidi ya wananchi wa Iran haviwezi kupita katika Bahari ya Hormuz.”
-
Ubalozi wa Iran Vienna: Iran Itaendelea Kusimama Imara na Kudumu Milele
Ubalozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Austria umesisitiza kuwa historia inaonyesha uimara wa wananchi wa Iran dhidi ya wavamizi, ukieleza kuwa maadui wa haki na wahalifu wanaotafutwa kimataifa hawatapata chochote isipokuwa fedheha na aibu.
-
Sayyid Mustafa Khamenei: Subira haiipingani na kulipiza haki wala kukabiliana na waovu
Sayyid Mustafa Khamenei amesema kuwa subira ya kweli si udhaifu wala kusalimu amri, bali ni kusimama imara katika njia ya haki huku ukiendelea kukabiliana na waovu na kutafuta haki dhidi ya waliohusika na uhalifu mkubwa.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Kulipiza kisasi hakutategemea uwepo wangu au wa viongozi wengine
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa kuwawajibisha waliohusika na mauaji ya Kiongozi Shahidi ni jambo ambalo litaendelea bila kutegemea uwepo wake binafsi au wa viongozi wengine, akisisitiza kuwa watu huru duniani watatekeleza wajibu wao kwa wakati wake.
-
Jeshi la Wanamaji la Walinzi wa Mapinduzi: Wageni Hawana Haki katika Mlango wa Hormuz
Jeshi la Wanamaji la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC Navy) limesema kuwa mataifa ya kigeni hayana haki yoyote katika eneo la Iran na Mlango wa Hormuz, likionya kuwa hatua za kijeshi za Marekani zinatishia usalama wa njia hiyo muhimu ya kimataifa.
-
Hali ya Majonzi Yatanda Tehran sambamba na kuanza kwa Shughuli za Kumuaga Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu
Hali ya majonzi na huzuni kubwa imeendelea kutawala katika mji wa Tehran kuelekea shughuli za mwisho za kumuaga Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Shahidi Ayatollah Sayyid Ali Khamenei(Ra), huku umma wa Kiislamu ukiendelea kutoa heshima zake kwa Kiongozi huyu Mwema na mtetezi wa Haki za Wapalestina na Haki za wanyonge popote walipo Ulimwenguni.
-
Mkuu wa Mahakama ya Iran: Madai ya Marekani ya Kutetea Haki za Binadamu ni ya Kichekesho
Mkuu wa Idara ya Mahakama ya Iran, Hujjatul-Islam Gholam-Hossein Mohseni Ejei, amesema kuwa madai ya Marekani kuhusu kuunga mkono haki za binadamu ni ya kichekesho, akituhumu Washington kutumia propaganda za vyombo vya habari kuficha uhalifu wake na kupotosha ukweli.
-
Wito wa Hekima na Umoja Watolewa kwa Umma wa Kiislamu, Uislamu Wahimizwa Kujengwa juu ya Elimu na Uadilifu
Wito wa kuimarisha hekima, uadilifu na umoja ndani ya Umma wa Kiislamu umetolewa, ukisisitiza kuwa tofauti za kimtazamo na kimadhehebu hazipaswi kuwa chanzo cha chuki bali fursa ya majadiliano ya kielimu na kuheshimiana.
-
Majlisi ya Maombolezo ya Muharram Yafanyika Jamiat Al-Mustafa, Dar es Salaam
Majlisi ya maombolezo ya mwezi wa Muharram imefanyika katika Jamiat Al-Mustafa, Dar es Salaam, Tanzania, ambapo mhadhiri alikuwa Sheikh Taqee Zacharia Athumani, akizungumzia sababu za kuhuishwa kwa kumbukumbu ya Karbala kila mwaka.
-
Tehran Yajibu Vikali Ufaransa: Yazitaja Kauli za Paris Kuhusu Haki za Binadamu kuwa Unafiki wa Kisiasa
Tehran yaitaja kauli za Ufaransa kuhusu Iran kuwa unafiki wa kisiasa, ikisisitiza matumizi ya haki za binadamu kama chombo cha shinikizo la kimataifa.
-
Sheikh Isa Qassim: Ujumbe wa A'shura Ni Kusimama Dhidi ya Batili na Kushikamana na Haki
Sheikh Isa Qassim, kiongozi wa kiroho wa Mashia wa Bahrain, amesisitiza kuwa ujumbe wa Ashura ni kusimama dhidi ya batili na kushikamana na haki, akibainisha kuwa tukio la Imam Hussein (a.s.) linabeba maadili ya heshima, ikhlasi na uthabiti, pamoja na wito wa kuimarisha umoja na mshikamano.
-
John bin Huway (r.a): Mtumwa Mweusi Aliyeandika Historia ya Uaminifu kwa Imam Hussein (a.s)
Miongoni mwa mashujaa waliotukuka katika tukio la Karbala yupo John bin Huway (r.a.), ambaye historia yake inaonyesha wazi kwamba mbele ya Mwenyezi Mungu heshima ya mtu haipimwi kwa rangi, kabila wala hadhi ya kijamii, bali kwa imani, uchamungu na uaminifu kwa haki.
-
Balozi wa Iran katika Umoja wa Mataifa: Hatutawahi Kusalimu Amri kwa Vitisho wala Mashinikizo
Balozi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haitawahi kusalimu amri mbele ya vitisho, mashinikizo au vitendo vya kutisha kutoka nje, akisisitiza kuwa taifa hilo litaendelea kulinda uhuru na haki zake kwa uthabiti.
-
Iran Yalaani Azimio la Baraza la Magavana la IAEA, Yasisitiza Itajibu na Kulinda Haki Zake
Ujumbe wa Iran mjini Vienna umesema kuwa azimio la Baraza la Magavana la IAEA dhidi ya Iran ni la kisiasa na lisilo la kitaalamu, ukisisitiza kuwa Tehran itajibu hatua hiyo ili kulinda haki zake zisizoweza kuondolewa.
-
Tehran Yalaani Uchokozi wa Kijeshi wa Marekani Dhidi ya Iran, Yasisitiza Haki ya Kujilinda
Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imelaani vikali kile ilichokiita “uchokozi wa kijeshi” wa Marekani dhidi ya nchi hiyo, ikisisitiza kuwa Iran haitasita kutumia haki yake ya kujilinda dhidi ya mashambulizi yoyote yanayoilenga.
-
Haki na Uadilifu wa Kifamilia katika Mizani ya Riwaya; Tathmini Upya ya Mipaka ya Ndoa ya Muda (Mut’a)
Ndoa ya muda (Mut’a) ambayo Mtume (s.a.w.w) aliihalalisha na Qur’ani ikaithibitisha, kwa msingi wa fiqhi ya Shia ni halali kisheria. Hata hivyo, riwaya zimeweka miongozo ya kimaadili na kijamii inayosisitiza tahadhari katika baadhi ya mazingira.
-
Abbas Araghchi: Makubaliano yako karibu iwapo diplomasia itapewa kipaumbele
Abbas Araghchi amesema kuwa makubaliano kati ya Iran na Marekani yako ndani ya mfukoni iwapo diplomasia itapewa kipaumbele, akisisitiza kuwa Iran haitafuti silaha za nyuklia lakini haitarudi nyuma katika haki yake ya teknolojia ya amani ya nyuklia.
-
Televisheni ya Urusi: Maelezo ya kifurushi cha mapendekezo ya Urusi kwa Iran na Marekani
Urusi imependekeza mpango wa makubaliano kati ya Iran na Marekani. Kampuni ya Urusi Rosatom isimamie urutubishaji wa urani nchini Iran kwa matumizi ya kiraia. Iran ibaki na haki ya kurutubisha urani kwa kiwango cha karibu 3.6%. Iran itoe dhamana ya kutotumia makombora yake kwa mashambulizi ya mapema dhidi ya Marekani au Israel. Lengo ni kufikia makubaliano yanayokubalika kwa pande zote.
-
Tarehe 13 Rajab: Maadhimisho ya Kuzaliwa kwa Kiongozi Mkuu wa Umma, Imam Ali (a.s)
Tarehe 13 ya mwezi wa Rajab ni siku ya kuzaliwa kwa Imam Ali (a.s), kiongozi mkuu baada ya Mtume Muhammad (s.a.w.w), ambaye ni mtu pekee aliyezaliwa ndani ya Al-Kaaba Tukufu na anayetambuliwa kwa elimu, uadilifu, ujasiri na maadili mema kwa wanadamu wote.
-
Araqchi: Marekani Haitaki Diplomasia ya Kweli, Bali Kulazimisha Iran Kunyimwa Haki Zake
Araqchi: "Diplomasia ya kweli haiwezi kujengwa juu ya mashinikizo na masharti ya upande mmoja. Kuitaka Iran iachane na haki zake halali si mazungumzo, bali ni jaribio la kulazimisha,”
-
Sheikh Ahmad Haji Atoa Mafunzo Muhimu ya Kujenga Utu na Kukemea Dhulma katika Jamii | "Dhulma huondoa Baraka na Kuleta Majuto"
"Unaweza kumdhulumu mtu na ukalala usingizi mzito, lakini yule uliyemdhulumu halali kamwe. Anakumbuka dhulma yako kila siku na humlalamikia Mwenyezi Mungu dhidi yako. Na ikumbukwe kuwa macho ya Mwenyezi Mungu hayalali,” amesema Sheikh Ahmad Haji, akisisitiza hatari ya dua ya aliyedhulumiwa.
-
Mwakilishi wa Ayatullah Sistani:
Licha ya juhudi zote, bado haki ya kueleza na kuonesha kikamilifu ukubwa wa Arbaeen haijatimizwa
Mwakilishi mwenye mamlaka kamili wa Ayatollah Sistani nchini Iran amesema kuwa Arbaeen ni fursa kubwa sana kwa wasimamizi na wenye dhamana wa tukio hili la kimataifa, na hawapaswi kupuuzia au kughafilika na thawabu na malipo makubwa yanayopatikana kutokana nalo.
-
Marafiki wa Ukweli Wako Wengi Zaidi Upande wa Pili | Kifo cha Kishahidi kwao hakileti upweke kwao Bali ni Daraja la kukutana na Msafara wa Waumini
"Katika ugeni hakuna hofu ya upweke; marafiki wapendwa wako wengi zaidi upande ule mwingine.” Kwa maana kwamba: Shahidi anapovuka kutoka dunia hii, haogopi kutengwa, kwa sababu anatambua wazi kuwa upande wa pili kuna kundi kubwa la wacha-Mungu, wakweli, watu wema, na mashahidi waliomtangulia, walio tayari kumpokea katika safu yao.
-
Jibu la Ayatollah Al-Udhma Sistani Kuhusu Kufuata Maimam wa Sala ya Jamaa Wanaopokea Malipo (Mishahara) za Kiserikali
Ayatollah Al-udhma Al-Sistani, kiongozi mkuu wa Shi’a, katika jibu lake kwa swali kuhusu kufuata maimamu wa sala ya jamaa (imam wa jamaa) wanaopokea haki (ya mishahara) kutoka serikali za Kiislamu, alishauri waumini wasisali nyuma yao, ili nafasi za kidini zilindwe dhidi ya uingiliaji wowote unaowezekana wa serikali.
-
Sheikh Naim Qassem: Kujisalimisha si chaguo; Hezbollah ina haki ya kulipiza kisasi kwa shambulio la Dahiyeh
Katibu Mkuu wa Hezbollah, Sheikh Naim Qassem, ameonya kwamba kundi la mapambano lina haki ya kulipiza kisasi kutokana na kuuawa kwa kamanda mwandamizi Haitham Al-Tabtabai, na akasisitiza kuwa kujisalimisha si chaguo kabisa.
-
Mahakama Kuu Yaweza Kuongeza Ufanisi wa Mfumo wa Kiislamu Kupitia Utekelezaji wa Haki
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya AhlulBayt (a.s), akiwa mbele ya wakurugenzi na wafanyakazi wa Mahakama ya Mkoa wa Gilan, amesema kuwa utekelezaji sahihi wa haki na usawa katika taasisi zote za serikali unaweza kuongeza ufanisi wa Jamhuri ya Kiislamu na kuthibitisha madai yake ya msingi kuhusu haki katika utawala.
-
Hotuba ya 22 ya Nahjul-Balagha: Njia za Kihistoria za Kurejesha Batili!
Katika sehemu hii ya hotuba, Imam Ali (a.s) anasisitiza kwamba vyombo vya habari na mbinu za kisaikolojia ni silaha kuu za Shetani na wafuasi wake katika kujaribu kurejesha dhulma na uongo katika jamii.
-
Sheikh Naim Qasim: Baada ya Mashambulizi ya Adui, Hezbollah Ilisimama Imara na Imekuwa Imara Zaidi / Wakati wa Vita Sikukubali Kwenda Iran
Katibu Mkuu wa Hezbollah ya Lebanon, Sheikh Naim Qasim, amesisitiza kwamba ingawa kuna uwezekano wa kutokea kwa vita kati ya Lebanon na Israel, jambo hilo halijathibitishwa, lakini upinzani (muqawama) uko tayari kulilinda taifa la Lebanon hata kama litakabiliwa na hali ya upungufu wa vifaa. Hezbollah Imeimarika Zaidi Baada ya Mashambulizi ya adui.
-
Ayatullah Javadi Amoli alisema:
“Iwapo kitovu cha mgawanyiko kitaundwa kati ya taifa na serikali, msingi wa mfumo utadhurika”
Mmoja wa maraji wa juu wa Washia alisema: “Iwapo kitovu cha mgawanyiko kitaibuka kati ya serikali na taifa, msingi wa mfumo utadhurika. Iwapo kiongozi atakuwa na wavurugiko kati ya matakwa yake ya kimaakili na tamaa za nafsi, ataondoka mbali na haki.”
-
Rais wa Baraza la Maulamaa wa Kishia Pakistan:
Uislamu ni mtangulizi wa haki sawa, uadilifu wa kiuchumi na utawala wa haki
Rais wa Baraza la Maulamaa wa Kishia Pakistan amesema kuwa: Uislamu ni mfumo kamili wa maisha ambao ni mtangulizi wa haki sawa, uadilifu wa kiuchumi na utawala wa haki, na mfano bora zaidi wa hayo ni mfumo wa haki wa Imam Ali (a.s) ambao utabaki kuwa kielelezo cha uadilifu na usawa daima.