Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Vyanzo vya kiusalama vya Taliban vimetangaza kuwa Jenerali Ikramuddin Saree, aliyekuwa mwanajeshi wa zamani wa Afghanistan, aliuawa Jijini Tehran kwa amri ya Shirika la Ujasusi la Pakistan (ISI). Kwa mujibu wa taarifa hizo, ISI ilikuwa ikimfuatilia jenerali huyo kwa muda mrefu na katika siku za hivi karibuni ilitekeleza mauaji hayo kupitia makundi yake ya wakala.
Pakistan inadaiwa kulenga kuvuruga uhusiano kati ya Kabul na Tehran, huku tukio hili la mauaji likitajwa kuwa jaribio la kuchafua mahusiano hayo katika mazingira nyeti ya sasa. Inaripotiwa kuwa Jenerali Ikramuddin Saree aliuawa kwa kupigwa risasi na watu wenye silaha katikati ya jiji la Tehran takribani wiki moja iliyopita, na tukio hilo bado linaendelea kuvuta hisia za wengi.
Your Comment