Afghanistan
-
Zaidi ya Wanawake na Wasichana 1,000 Wafariki Katika Tetemeko la Ardhi Mashariki mwa Afghanistan
UN: Wanawake na Wasichana 1,025 Wamefariki Katika Tetemeko la Ardhi Mashariki mwa Afghanistan. Ofisi ya Kuratibu Misaada ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa (OCHA) nchini Afghanistan imetangaza kuwa: Jumla ya wanawake na wasichana 1,025 wamepoteza maisha kutokana na tetemeko la ardhi lililotokea katika maeneo ya mashariki mwa Afghanistan. Taarifa hiyo inasisitiza ukubwa wa athari za kibinadamu, hasa kwa wanawake na watoto, katika tukio hili la maafa ya asili.
-
Hamas Yatuma Salamu za Pole kwa Watu wa Afghanistan Kufuatia Tetemeko la Ardhi
Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imetoa salamu za rambirambi kufuatia tetemeko la ardhi lililosababisha vifo katika mkoa wa Kunar, nchini Afghanistan, na kueleza masikitiko yake makubwa kwa maelfu ya raia waliopoteza maisha au kujeruhiwa.
-
Salam za Rambirambi za Baraza la Maulamaa na Wenye Mamlaka wa Madhhebu ya Shia nchini Afghanistan Kufuatia Tetemeko la Ardhi Mashariki mwa Afghanistan
Baraza la Maulamaa na Watu Wenye Mamlaka wa Madhehebu ya Shia nchini Afghanistan, kupitia taarifa rasmi, limeeleza masikitiko na mshikamano wao na familia za waathirika wa tetemeko la ardhi lililotokea hivi karibuni katika mkoa wa Kunar, mashariki mwa Afghanistan, huku likisisitiza umoja wa kitaifa na hitajio la msaada wa haraka kwa waathirika.
-
Tetemeko la ardhi nchini Afghanistan limeua zaidi ya watu 1,200
Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 6.2 katika kipimo cha Richter liliikumba mkoa wa Kunar mashariki mwa Afghanistan, na hadi sasa limesababisha vifo vya zaidi ya watu 1,200.
-
Ujerumani Yapokea Kundi la Kwanza la Wakimbizi wa Kiafghan Baada ya Miaka Mitatu ya Kusubiri
Baada ya miezi kadhaa ya kusubiri na shinikizo kutoka kwa mahakama, Ujerumani hatimaye imepokea kundi la kwanza la wakimbizi wa Afghanistan waliokimbia utawala wa Taliban.
-
Ripoti ya Umoja wa Mataifa: Asilimia 92 ya Watu wa Afghanistan Wanataka Elimu kwa Wasichana Kuendelezwa
Wakati Serikali ya Taliban inaendeleza sera za kuzuia elimu kwa wasichana, ripoti ya Umoja wa Mataifa inaonyesha wazi kuwa watu wa Afghanistan – wanawake kwa wanaume, wa mjini kwa vijijini – wanataka mabadiliko. Wanataka elimu kwa wasichana, fursa za kazi kwa wanawake, na mustakabali bora kwa jamii nzima.
-
Masomo kwa Wasichana Hayana Nafasi katika Mkakati wa Miaka 5 wa Taliban
Msemaji wa Taliban, alipoulizwa na mmoja wa waandishi wa habari kuhusu nafasi ya elimu na masomo ya wasichana katika mkakati huu wa miaka mitano, alisema kuwa suala hilo ni jambo la “kijuujuu” mbele ya mada kuu ya kikao hicho, na akakataa kulijibu.
-
Araqchi: Taliban Haijaheshimu Haki za Waislamu wa Kishia wa Afghanistan
Ikumbukwe kuwa, baada ya kurejea madarakani, Taliban ilifuta rasmi Sheria ya Hali ya Kiraia ya Waislamu wa Kishia, na kuondoa vitabu vyote vya Fiqh ya Ja’fari kutoka vyuo vikuu, shule na maktaba za serikali. Kundi hilo limekuwa likisisitiza kwamba sheria za Afghanistan lazima zitekelezwe kwa mujibu wa Fiqh ya Kihanifi pekee.
-
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa China na Pakistan Wawasili Kabul, Afghanistan
Waziri wa Mambo ya Nje wa China alipokelewa na Amir Khan Muttaqi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Kaimu ya Afghanistan, na kufanya naye mazungumzo. Wakati huo huo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Pakistan alipokelewa na Hanafi Wardak, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Taliban.
-
Mkutano wa Haji Muhammad Muhaqiq na Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Iraq
Mchana wa Jumamosi tarehe 25 Mordad 1404 (sawa na Agosti 16, 2025), Haji Muhammad Muhaqiq, kiongozi wa Chama cha Umoja wa Kiislamu wa Watu wa Afghanistan, alikutana na Dk. Humam al-Hammoudi, Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Iraq, na kufanya mazungumzo naye.
-
Ahadi Mpya za Taliban / Ufunguzi wa Shule za Wasichana Wategemea "Kibali cha Kisharia"
Zabihullah Mujahid, msemaji wa serikali ya Taliban, ametangaza kuwa mchakato wa kupata “kibali sahihi cha kisharia” kwa ajili ya kufunguliwa tena shule na vyuo vikuu vya wasichana bado unaendelea. Hii ni baada ya zaidi ya miaka minne ya kunyimwa wanawake na wasichana haki ya msingi ya elimu.
-
Waumini wa Kabul Waadhimisha Arubaini ya Imam Hussein (a.s) Wakihoji Vikwazo vya Safari za Mahujaji (Mazuwwari) wa Afghanistan
Sambamba na kuwadia kwa siku ya Arubaini ya Imam Hussein (a.s), hafla ya kuadhimisha siku hii ilifanyika katika Kituo cha Fiqhi cha Maasemamu Watakatifu (a.s) upande wa magharibi mwa jiji la Kabul. Washiriki, sambamba na kufanya maombolezo kwa ajili ya Imam Hussein (a.s), walitoa malalamiko makali dhidi ya ukosefu wa uratibu wa kisiasa na kisheria ambao mwaka huu uliwazuia waumini wengi wa Afghanistan kusafiri kwa wingi kwenda Karbala.
-
Umoja wa Mataifa:Katika kuelekea miaka 4 ya utawala wa Taliban, wanawake wa Afghanistan wanakabiliwa na mgogoro mkubwa wa haki za wanawake Duniani
Kitengo cha wanawake cha Umoja wa Mataifa, katika kuelekea kumbukumbu ya miaka minne tangu Taliban ichukue madaraka nchini Afghanistan, kimetoa taarifa ikikosoa vikali mwenendo wa kundi hilo kuhusu wanawake wa Afghanistan.
-
Mazuwwari wa Afghanistan: Warithi wa Karbala, Sio Vipande vya Mchezo wa Chesi
Ukosoaji wa Matusi ya Gazeti la Ettelaat-e-Rooz dhidi ya Waislamu wa Kishia wa Afghanistan
Katikati ya wimbi la maandiko yenye upendeleo ambayo, kwa kisingizio cha utafiti, yanadhalilisha imani na uelewa wa Waislamu wa Kishia wa Afghanistan, ni lazima kukumbusha ukweli: ukweli wa uhusiano wa kihistoria na wa kina kati ya mataifa mawili ya Iran na Afghanistan, ambao katika nyanja za mapambano, ulinzi na mshikamano, daima wamesimama bega kwa bega — na lengo la pamoja la maadui wao limekuwa kuvunja mshikamano huu.
-
Baada ya kusaini makubaliano makubwa zaidi ya nishati katika historia yake - Je, Afghanistan inakaribia kujitegemea?
Kabul imeanza safari ya kuzalisha megawati 10,000 za umeme baada ya kusaini makubaliano makubwa zaidi ya nishati katika historia yake, mpango unaoweza kuibadilisha kutoka nchi inayoagiza umeme hadi kuwa muuzaji wa nishati katika ukanda.
-
Funzo Kuu la Arbaeen ni Msimamo Imara, Subira, na Mapambano: Ayatollah Ramazani
Mkutano wa awali wa wavuti (webinar) ulioandaliwa na Idara ya Masuala ya Kimataifa ya Jumuiya ya Kimataifa ya AhlulBayt (a.s.) kuhusu mada “Kutathmini Ujumbe wa Kimataifa wa Arbaeen ya Imam Hussain (a.s): Kutoka Wilayat hadi Wajibu” umefanyika.
-
Kudhibiti Moto wa Misitu na Kutojali kwa Gavana wa Bamiyan Kuhusu Uhamishaji wa Lazima wa Waislamu wa Kishia nchini Afghanistan
Wakati serikali ya muda ya Taliban imetangaza kuwa Gavana wa Mkoa wa Bamiyan, Mawlawi Abdullah Sarhadi, alifika haraka eneo la tukio na kuongoza operesheni ya kuzima moto wa misitu kama ishara ya kujali mazingira, ripoti nyingine zimeripoti uhamishaji wa lazima wa makumi ya familia za Kishia na jamii ya Wahazara kwa amri ya kiongozi huyo huyo wa Taliban – jambo lililosababisha hasira na taharuki kubwa miongoni mwa wananchi na wanaharakati wa kiraia.
-
Watu milioni 10 nchini Afghanistan wanakosa maji safi ya kunywa
Katika taarifa yake ya hivi punde kuhusu tatizo la maji nchini Afghanistan, UNAMA ilisema kuwa zaidi ya watu milioni 10, karibu theluthi moja ya wakazi wa Afghanistan, hawana maji safi ya kunywa na wanatumia vyanzo vya maji visivyo safi.
-
Mauaji ya Mwanazuoni wa Kishia katika jimbo la Badakhshan nchini Afghanistan
Hojjat al-Islam wal- Muslimin, Sayyid Kazem Amiri, Profesa wa Seminari ya Imam Sadiq (AS) ameuawa katika mji wa Kashem, Mkoa wa Badakhshan, Afghanistan.
-
Mlipuko Mkubwa Watokea Katika Mji wa Bamiyan, Afghanistan
Taarifa kuhusu majeruhi au vifo: Hadi sasa, hakuna taarifa rasmi kuhusu kiwango cha majeruhi au uharibifu wa mali, na mamlaka ya polisi ya Taliban mjini Bamiyan haijatoa tamko lolote rasmi kuhusiana na tukio hili.
-
UNICEF: Takriban watoto milioni 4 wa Afghanistan hawana fursa ya kupata elimu
UNICEF imetangaza hivi karibuni kuwa takriban watoto milioni 4 nchini Afghanistan hawapati elimu kutokana na uhaba wa shule, huduma za afya, na walimu wenye sifa.
-
Kuendelea kuwepo kwa Marekani nchini Afghanistan kinyume na misimamo rasmi ya pande husika / Ujasusi na vitisho vya Marekani kwa nchi za eneo
Ingawa Marekani kwa dhihiri imeondoa majeshi yake kutoka Afghanistan, ripoti na kauli za Donald Trump zinaonyesha kuwa msingi mmoja wa kimkakati bado uko chini ya udhibiti wa Marekani nchini humo. Washington inatumia kambi hii kufanikisha malengo kama vile ufuatiliaji wa taarifa za kijasusi kuhusu Iran, China na Urusi, pamoja na kuhifadhi ushawishi wake katika Asia ya Kati.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Taliban akiwa Tehran: Haki ya maji ya Iran imekuwa ikitiririka kwa mwezi mmoja sasa
Amir Khan Muttaqi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Muda ya Afghanistan, amesema saa chache zilizopita katika “Jukwaa la Mazungumzo ya Tehran” kwamba: “Kwa mwezi mmoja sasa, haki ya maji ya Iran kutoka Afghanistan imekuwa ikielekezwa kuelekea Sistan na Baluchestan.”
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Afghanistan na Iran wamekutana na kufanya mazungumzo Mjini Tehran
Waziri wa Mambo ya Nje wa serikali ya muda ya Afghanistan, ambaye yuko Iran kwa ajili ya kushiriki katika Jukwaa la Mazungumzo ya Tehran, amekutana na Sayyid. Araghchi na kufanya mazungumzo kuhusu ushirikiano wa pande mbili, masuala ya kiusalama, hali ya wakimbizi na haki ya maji ya Iran.
-
"Wadau wa sekta ya utamaduni wa Afghanistan watilia mkazo juu ya ukarabati wa "Gonbad-e-Begum" / 'Kubba ya Malkia' katika Mkoa wa Ghazni"
"Baadhi ya wadau wa sekta ya utamaduni wa Afghanistan wametilia mkazo umuhimu wa ukarabati na urejeshwaji wa jengo la kihistoria la 'Kubba ya Malkia' katika Mkoa wa Ghazni."
-
Serikali ya Muda ya Afghanistan Yatoa Pole kwa Watu wa Iran Kufuatia Mlupuko wa Bandar Abbas
Baada ya mlipuko uliotokea jana katika Bandari ya Shahid Rajaei iliyopo katika Mji wa Bandar Abbas, Serikali ya Muda ya Afghanistan, sambamba na mataifa mengi duniani, imetoa pole kwa watu na Serikali ya Iran.
-
Mchakato wa kuwatimua wahamiaji wa Afghanistan walioko Pakistan unaanza leo hii
Vyombo vya Habari vya Pakistan vimeripoti kuwa mchakato wa kuwatimua wahamiaji wa Afghanistan bila hati za ukazi wa kisheria kutoka nchi hii umepangwa kuanza leo Jumanne (Aprili 1).
-
Maafisa wa Umoja wa Mataifa: Wasichana wa Afghanistan Wanapaswa Kurejea Shuleni
Mkurugenzi mtendaji wa Idara ya Umoja wa Mataifa ya Wanawake, akizungumzia kuendelea kupigwa marufuku kwa elimu ya wasichana wa Afghanistan, amesema kuwa wasichana katika nchi hii wanapaswa kurejea shuleni haraka iwezekanavyo.
-
Human Rights Watch: Afghanistan si salama kwa wahamiaji waliofukuzwa kutoka Pakistan
Human Rights Watch, katika ripoti yake ya hivi punde kuhusu wahamiaji wa Afghanistan nchini Pakistan, ilionyesha wasiwasi wake kuhusu kufukuzwa kwa lazima kwa wahamiaji hao.
-
Tangazo la Urusi la kuwa tayari kupatanisha Pakistan na Afghanistan
Wakati mvutano kati ya Pakistan na Afghanistan ukiendelea, Balozi wa Urusi nchini Pakistan alitangaza utayari wa nchi yake kutatua mivutano hii.