21 Februari 2026 - 21:20
Je, wasichana waliobalehe hivi karibuni au watu wanaopata ugumu mkubwa kufunga wanaweza kuacha kufunga?

Msichana aliyebalehe hivi karibuni au mtu yeyote anayepata ugumu wa kufunga haruhusiwi kuacha kufunga moja kwa moja kwa sababu ya hofu au dhana tu ya ugumu. Anapaswa kuweka nia ya kufunga mwanzoni mwa siku. Ikiwa wakati wa kufunga atapata taabu au mashaka makubwa yasiyovumilika, ndipo anarusiwa kufungua. Siku aliyofungua atalazimika kuilipa (qaḍā’) baada ya Ramadhani.

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Ikiwa uwezo wa mtu aliyewajibika kufunga ni wa kiwango ambacho kwa sababu ya udhaifu wa mwili au urefu wa siku, kufunga - hata kwa kupunguza shughuli na kuzingatia lishe - kunasababisha ugumu mkubwa usiovumilika, basi kwa tahadhari ya wajibu (iḥtiyāṭ wājib) anatakiwa kuweka nia ya kufunga; lakini akifikia hali ya mashaka au taabu kali sana, anaweza kufungua (kula/kunywa) na baadaye atalipa (qaḍā’) ya siku hiyo.

Pia, ikiwa ugumu huo mkubwa unatokana na shughuli kama kazi, masomo au kujisomea, kwa mujibu wa fatwa anatakiwa kufunga; na akifikia mashaka makubwa sana, anaweza kufungua na atalipa siku hiyo baadaye.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha