Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ametangaza kuwa mazungumzo na Marekani mjini Geneva yatarejelewa kwa kuzingatia makubaliano ya duru zilizopita, akisisitiza kwamba Tehran ina dhamira ya dhati ya kufikia makubaliano ya haki katika muda mfupi iwezekanavyo.
Iran imesisitiza kuwa kamwe haijawahi kutafuta silaha za nyuklia, lakini haitarudi nyuma katika haki yake ya kunufaika na teknolojia ya nyuklia kwa matumizi ya amani.
Araghchi ameeleza hatua hii kuwa ni “fursa ya kihistoria” ya kuondoa wasiwasi wa pande zote, akisisitiza kuwa kufikiwa kwa makubaliano kunawezekana tu kwa kuipa diplomasia kipaumbele.
Your Comment