Imam Ali(as)
-
Imam Ali (a.s) na Siri za Ukuruba Wake kwa Mtume Mm Muhammad (s.a.w.w)
Imam Ali (a.s) si tu sahaba wa karibu wa Mtume (s.a.w), bali ni zao la malezi ya moja kwa moja ya Mtume, shahidi wa mwanzo wa wahyi, na mhimili wa maadili ya Kiislamu. Upendo na ufuasi wake unabaki kuwa kipimo muhimu cha uaminifu wa kweli kwa Uislamu na Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w).
-
Mhadhiri wa Masomo ya Ngazi ya Juu katika Hawza ya Qom asisitiza:
Lengo kuu la utawala wa Amirul-Mu’minin (a.s) ni kuwaongoza wanadamu / mpaka kati ya uhuru wa kujieleza na vitendo dhidi ya usalama wa umma
Mheshimiwa Sayyid Mujtaba Nourmofidi, Rais wa Taasisi ya Utafiti wa Fiqhi ya Kisasa, alipohudhuria Shirika la Habari la ABNA, alichambua mada ya: “Fiqhi ya kisiasa katika kuweka mipaka kati ya uhuru wa kujieleza na ukosoaji halali, dhidi ya uasi na vitendo vinavyohatarisha usalama wa umma katika utawala wa Imam Ali (a.s)”.
-
Ni vipi Fatima Zahra (a.s) Alikuwa Mpenzi na Mpendwa Zaidi Katika Maisha ya Ali (a.s)?
Katika baadhi ya nyakati, mtu humtambulisha nafsi yake kwa kutaja nasaba yake na watu wakubwa. Hivyo ndivyo alivyofanya Amirul-Mu'minin Ali (a.s) katika mojawapo ya khutba zake baada ya kurejea kutoka vita vya Nahrawan. Ali (a.s) alisema: “Mimi ni mume wa Bibi Batul, Bibi wa wanawake wa ulimwengu, Fatima aliye mchamungu, msafi, mtukufu, mwongofu, mpendwa wa Mpenzi wa Allah, bora wa mabinti wake na mchanga wa roho ya Mtume wa Allah (s.a.w.).” Kutaja kwa Imam Ali (a.s) daraja la juu la Bibi Zahra (a.s) baada ya kujinasabisha na mwanamke huyu mtukufu ni kusisitiza nafasi kuu ya bibi huyu mbele ya mtu mkubwa kama Ali (a.s).
-
Maadhimisho ya Kifo cha Bibi Fatima Umm ul-Banin (a.s)
Bibi Ummul-Baneen aliwapenda Ahlul-Bayt wa Mtume kuliko alivyowapenda wanawe mwenyewe. Alipopata habari za huzuni za Karbala, hakumuuliza kwanza kuhusu wanawe wanne, bali alisema: “Nijulisheni kuhusu Hussein.”
-
Mafunzo kutoka katika Maisha ya Bibi Fatima Zahra (a.s) kwa Ajili ya Kujenga Utulivu katika Familia +
Hadithi ya Mgawanyo wa Majukumu kati ya Imam Ali (a.s) na Bibi Fatima Zahra (s.a) Hadithi inayosimulia jinsi Mtume Mtukufu (s.a.w.w) alivyogawa majukumu ya kifamilia kati ya Imam Ali (a.s) na Bibi Fatima (a.s) ni mfano wa hekima katika ujenzi wa familia ya Kiislamu.
-
Tone kutoka Nahjul-Balagha 27 | Kuheshimu Hadhi ya Imamu ni Nini?
Matokeo ya utiifu ni nini?. Amirul-Mu’minin Ali bin Abi Talib (AS) katika khutba ya 156 anasema: «إِنْ أَطَعْتُمُونِی فَإِنِّی حَامِلُکُمْ إِنْ شَاءَ اللَّهُ عَلَی سَبِیلِ الْجَنَّةِ» Yaani: “Mkinitii mimi – mimi kama Imamu– bila shaka nitawaongoza katika njia ya Peponi"
-
Uzinduzi wa Mfumo wa Kielelezo cha Kujadiliana na Tafsiri za Qur’ani / Ayatollah Makarem:Teknolojia Mpya Iwe Kwenye Huduma ya Qur’ani na AhlulBayt(as)
Ayatollah Makarem Shirazi, mmoja wa maraja’ wa kiislamu, akisisitiza umuhimu wa kueneza habari za mafanikio ya kisayansi, alisema: “Moja ya mahitaji muhimu ya leo ni kuwafahamisha watu. Kuna shughuli nyingi zenye thamani zinafanyika, lakini taarifa zake ni chache. Vyombo vya habari, redio, televisheni na mashirika ya habari vinapaswa kusambaza maendeleo haya ili wananchi waone kiwango cha maendeleo ya teknolojia mpya katika sekta ya elimu ya dini.”
-
-
Uchambuzi na Tathmini ya Thawabu za Ajabu na za Kipekee kwa Matendo Rahisi
Kuwepo kwa thawabu kubwa kwa baadhi ya matendo rahisi ni jambo lisilopingika, kwa sababu mizani ya Mwenyezi Mungu katika kutoa malipo haifanani na mizani ya kidunia.
-
Hotuba ya 22 ya Nahjul-Balagha: Njia za Kihistoria za Kurejesha Batili!
Katika sehemu hii ya hotuba, Imam Ali (a.s) anasisitiza kwamba vyombo vya habari na mbinu za kisaikolojia ni silaha kuu za Shetani na wafuasi wake katika kujaribu kurejesha dhulma na uongo katika jamii.
-
Ushahidi wa Kifo cha Kishahidi cha Bibi Fatimah az-Zahra (a.s) | Mtizamo wa Shia na Sunni juu ya Kifo Hicho
Ushahidi wa Riwaya za Kisunni: Shia pia wametaja kuwa baadhi ya maelezo kuhusu tukio la shambulio la nyumba ya Bibi Fatimah (a.s.) na Imam Ali (a.s.) yanapatikana hata katika baadhi ya vitabu vya Kisunni, na wamekusanya riwaya zaidi ya 84 kutoka kwa wanazuoni wa Kisunni kuhusu tukio hilo (kama ilivyokusanywa katika al-Hujūm ʿalā Bayt Fāṭimah (a.s).
-
Rais wa Baraza la Maulamaa wa Kishia Pakistan:
Uislamu ni mtangulizi wa haki sawa, uadilifu wa kiuchumi na utawala wa haki
Rais wa Baraza la Maulamaa wa Kishia Pakistan amesema kuwa: Uislamu ni mfumo kamili wa maisha ambao ni mtangulizi wa haki sawa, uadilifu wa kiuchumi na utawala wa haki, na mfano bora zaidi wa hayo ni mfumo wa haki wa Imam Ali (a.s) ambao utabaki kuwa kielelezo cha uadilifu na usawa daima.
-
Irada ya Mwanadamu; Ufunguzi wa Mafanikio na Furaha katika Mafundisho ya Qur’ani na Hadithi
Mtazamo wa Qur'an kuhusu Irada: Qur’ani Tukufu inamueleza mwanadamu kuwa kiumbe mwenye uhuru wa kuchagua na mwenye kuwajibika: “Hakika Mwenyezi Mungu habadilishi yaliyoko kwa watu mpaka wabadilishe yaliyoko katika nafsi zao.” (Sura ya Ra’d, aya 11).
-
"Mwizi, huiba riziki yake mwenyewe!"
Riziki Halali Katika Mafundisho ya Kiislamu - Kulingana na Hadithi za Mtume na Maimamu wa Ahlul-Bayt (as) | Kulingana na mafundisho ya Kiislamu, kila mtu ana sehemu maalum ya riziki halali aliyopangiwa. Kupata riziki kupitia njia haramu hakuongezi sehemu hiyo, bali hupunguza riziki ya halali na huleta madhara na athari mbaya katika maisha.
-
Mawakibu (1,800) za waombolezaji yalifurika katika Haram Tukufu ya Imam Ali (a.s) kwa Mnasaba wa kumbukumbu ya kufariki kwa Mtukufu Mtume Muhammad (s)
Haram Tukufu ya Imam Ali (a.s) Yapokea Makundi 1800 ya Waombolezaji Kutoka Ndani na Nje ya Iraq kwa Kumbukumbu ya Kifo cha Mtume Muhammad (s.a.w.w).
-
Barua ya 18 ya Nahjul Balagha / Onyo kwa Viongozi wote wa Serikali ya Kiislamu
Barua ya kumi na nane (18) ya Nahjul Balagha, ingawa imeandikwa kwa jina la Abdullah bin Abbas, gavana wa Basra wakati huo, lakini inapaswa kuchukuliwa kama onyo kwa viongozi wote wa serikali katika historia yote. Onyo hili linapaswa kuwa mwongozo wa kila mtu anayepewa nafasi au jukumu katika taasisi mbalimbali za mfumo wa Kiislamu.
-
"Wema Hauozi, Dhambi Haisahauliki, Allah Hafi, Utalipwa kama Ulivyotenda" | Ni Maneno Mazito kutoka katika Vyanzo vya Kiislamu
Maneno haya ni wito wa kutuweka kwenye mstari wa Ucha Mungu, uwajibikaji wa nafsi, na kujiepusha na dhambi kwa kutambua kuwa hakuna kisichojulikana mbele ya Mwenyezi Mungu (swt).
-
Maana ya Ghadir Khum na Umuhimu wa Siku ya Ghadir Khum katika Uislamu
Ghadir Khum ni tukio la kihistoria lenye uzito mkubwa kwa Waislamu, hasa kwa wale wanaotilia mkazo nafasi ya Ahlul Bayt (a.s) katika uongozi wa umma. Ni siku ya kutafakari juu ya uongozi wa haki, kutambua mafundisho ya Mtume (s.a.w.w), na kuhuisha uhusiano wa kidini kwa msingi wa upendo, uadilifu, na utiifu kwa uongozi wa kweli wa Kiislamu.
-
"Maarifa ya Nahjul Balagha (3) / Dua za Imam Ali (a.s)"
Hata ingawa seti ya dua zinazosimuliwa kutoka kwa Imam Ali (a.s) inafikia takriban dua 700, lakini kwa kuzingatia msisitizo wa Sayyid Razi katika kuchagua baadhi ya maneno ya Imam Ali (a.s) katika kitabu cha Nahjul Balagha, kuna takriban dua 50 zinazohusishwa na Amir al-Mu'minin (a.s) ambazo zinahusisha mada mbalimbali.
-
Faida ya kuingiza furaha katika moyo wa mtu mwenye matatizo
"Huna hasara yoyote hata chembe mbele ya Mwenyezi Mungu endapo utamsapoti Mwalimu kwa kumlipia mtoto wake ada ya shule na kumuepushia tatizo la mtoto wake kufukuzwa shule kwa ajili ya ada (school fees), au ukamlipia Mwalimu kodi ya nyumba"
-
Hadithi za Mtume(saww) ndaniya Nahjul-Balagha zinaonyesha jinsi Imam Ali(as) alivyoendeleza njia ya Mtume(saww) katika Uongozi,UadiIifu Ibada na Siasa
Mtume Muhammad (s.a.w.w): “ Yeyote atakayenisingizia mimi uongo kwa makusudi basi ajiandalie makazi yake kuwa ni motoni.”
-
Dalili ya wazi na kubwa Kuhusu Kupigana kwa Malaika Pembeni ya Ali (as)
kwa Hakika Amirul-Mu'minin Ali (a.s) hakuwa anarudi kutoka vitani mpaka apate ushindi kwa msaada wa Mwenyezi Mungu. Na ni fadhila iliyo kubwa kiasi gani kuwa Malaika Jibril (as) anapigana upande wa kulia wake, na Mikail (as) upande wa kushoto wake.
-
Ugumu uliopo katika kuwatangaza Kizazi Kitukufu cha Mtume Muhammad (saww) ambao ni Mawalii wa Mwenyezi Mungu (s.w.t) | Watu hawawajui Ahlu-Bayt (as)!
Leo hii, jambo la kuwatangaza Ahlul-Bayt (a.s) ambao ndio tumeusiwa na Mtume wetu Muhammad (s.a.w.w) tushikamane nao baada yake na kuwafuata wakiwa wakiwa kama Kizito cha Pili baada ya Qur'an Tukufu, ni jambo gumu kulingana na jamii ya watu tunayokabiliana nayo.
-
Mwanaume Mkristo aliyesilimu kwa sababu ya tabia nzuri ya Ali (AS)
Je, Hadhrat Ali (AS) alifanya nini wakati Mwanaume mmoja Mkristo aliposilimu? Kwa heshima ya kusilimu kwake, alimpa ngao yake (inayovaliwa vitani) na kumpa nafasi katika Serikali.
-
Wosia Kwa Historia na Wanadamu Wote
Wosia wa Hadhrat Ali (amani iwe juu yake), ni moja ya maandiko muhimu ya Kiislamu yaliyosheheni mafunzo ya kimaadili (kiakhlaq), kijamii na kisiasa, na sio tu kwa ajili ya watoto na masahaba zake, bali pia ni nuru kwa watu wote wanaotafuta ukweli (uhakika) na uadilifu.
-
Asilimia 30 ya ongezeko la idadi ya Mazuwwari kwenye Madhabahu (Haram) ya Imam Ali (AS) katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani
Idadi ya Mazuwwari wa Madhabahu ya Imam Ali (AS) iliweka rekodi katika siku ya 21 ya Ramadhani, na mwaka huu, mahujaji milioni moja na 500,000 zaidi wametembelea (wamezuru) Madhabahu ya Alawi kuliko mwaka jana.
-
Sababu ya Ushujaa na Ujasiri wa Ali bin Abi Talib (a.s)
Sheikh Said Othman: "Imam Ali (a.s) anakumbukwa na Ulimwengu wote wa Kiislamu kuwa yeye ni Shujaa wa Kiislamu, aliyeupigania Uislamu, na kuuhami Uislamu kwa ushujaa wake na ujasiri wake, daima aliutetea uhai wa Uislamu na aliuheshimisha Uislamu kupitia Upanga wake, kama ambavyo Ummul - Muuminina Khadija (s.a) aliuhamia na kuuheshimisha Uislamu kupitia Mali yake".
-
Ayatollah Ramezani: Kutokushindwa ndio msingi wa utawala wa Alawi; Imam Ali (amani iwe juu yake) ni kielelezo cha Ulimwengu wa Mwanadamu
Katibu Mkuu wa Baraza la Kidunia la Ahlul-Bayt (a.s.) katika hafla ya kuhuisha Usiku wa 21 wa Ramadhani, akiashiria kwamba kutokukubali ndio msingi wa utawala wa Alawi, alisema: Imam Ali (a.s) ni kielelezo cha ulimwengu wa Wanadamu.
-
Imam Ali (a.s) Katika Kurasa za Historia:
Elimu na Maarifa, Ibada na Ucha Mungu, Ujasiri na Ushujaa, na Upole na Huruma ya Imam Ali (a.s)
Imam Ali (a.s) alipigwa upanga na mtu aliyejulikana kwa jina la Abdur Rahman bin Muljim Muradi (laana iwe juu yake milele). Imam Ali (a.s) alikufa Shahidi siku tatu baadaye katika usiku wa 21 wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Imam Ali bin Abi Talib (a.s) ni shakhsia wa pili mkubwa katika Uislamu baada ya Mtukufu Mtume Muhammad (s.a.w.w), na anaelezwa katika historia ya Uislamu kuwa alikuwa jasiri na shujaa wa kupigiwa mfano, mwenye imani thabiti, mwenye akhlaki njema, mwenye elimu na uadilifu usio na kifani.
-
Wasifu wa Amirul Momineen (AS) unapaswa kuunganisha mwili wa Umma wa Kiislamu
Katika hotuba yake kwa mnasaba wa kuuawa shahidi Imam Ali, Waziri Mkuu wa Iraq alitaja fadhila za Imam Ali (a.s).