Imam Ali(as)
-
Hadithi za Mtume(saww) ndaniya Nahjul-Balagha zinaonyesha jinsi Imam Ali(as) alivyoendeleza njia ya Mtume(saww) katika Uongozi,UadiIifu Ibada na Siasa
Mtume Muhammad (s.a.w.w): “ Yeyote atakayenisingizia mimi uongo kwa makusudi basi ajiandalie makazi yake kuwa ni motoni.”
-
Dalili ya wazi na kubwa Kuhusu Kupigana kwa Malaika Pembeni ya Ali (as)
kwa Hakika Amirul-Mu'minin Ali (a.s) hakuwa anarudi kutoka vitani mpaka apate ushindi kwa msaada wa Mwenyezi Mungu. Na ni fadhila iliyo kubwa kiasi gani kuwa Malaika Jibril (as) anapigana upande wa kulia wake, na Mikail (as) upande wa kushoto wake.
-
Ugumu uliopo katika kuwatangaza Kizazi Kitukufu cha Mtume Muhammad (saww) ambao ni Mawalii wa Mwenyezi Mungu (s.w.t) | Watu hawawajui Ahlu-Bayt (as)!
Leo hii, jambo la kuwatangaza Ahlul-Bayt (a.s) ambao ndio tumeusiwa na Mtume wetu Muhammad (s.a.w.w) tushikamane nao baada yake na kuwafuata wakiwa wakiwa kama Kizito cha Pili baada ya Qur'an Tukufu, ni jambo gumu kulingana na jamii ya watu tunayokabiliana nayo.
-
Mwanaume Mkristo aliyesilimu kwa sababu ya tabia nzuri ya Ali (AS)
Je, Hadhrat Ali (AS) alifanya nini wakati Mwanaume mmoja Mkristo aliposilimu? Kwa heshima ya kusilimu kwake, alimpa ngao yake (inayovaliwa vitani) na kumpa nafasi katika Serikali.
-
Wosia Kwa Historia na Wanadamu Wote
Wosia wa Hadhrat Ali (amani iwe juu yake), ni moja ya maandiko muhimu ya Kiislamu yaliyosheheni mafunzo ya kimaadili (kiakhlaq), kijamii na kisiasa, na sio tu kwa ajili ya watoto na masahaba zake, bali pia ni nuru kwa watu wote wanaotafuta ukweli (uhakika) na uadilifu.
-
Asilimia 30 ya ongezeko la idadi ya Mazuwwari kwenye Madhabahu (Haram) ya Imam Ali (AS) katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani
Idadi ya Mazuwwari wa Madhabahu ya Imam Ali (AS) iliweka rekodi katika siku ya 21 ya Ramadhani, na mwaka huu, mahujaji milioni moja na 500,000 zaidi wametembelea (wamezuru) Madhabahu ya Alawi kuliko mwaka jana.
-
Sababu ya Ushujaa na Ujasiri wa Ali bin Abi Talib (a.s)
Sheikh Said Othman: "Imam Ali (a.s) anakumbukwa na Ulimwengu wote wa Kiislamu kuwa yeye ni Shujaa wa Kiislamu, aliyeupigania Uislamu, na kuuhami Uislamu kwa ushujaa wake na ujasiri wake, daima aliutetea uhai wa Uislamu na aliuheshimisha Uislamu kupitia Upanga wake, kama ambavyo Ummul - Muuminina Khadija (s.a) aliuhamia na kuuheshimisha Uislamu kupitia Mali yake".
-
Ayatollah Ramezani: Kutokushindwa ndio msingi wa utawala wa Alawi; Imam Ali (amani iwe juu yake) ni kielelezo cha Ulimwengu wa Mwanadamu
Katibu Mkuu wa Baraza la Kidunia la Ahlul-Bayt (a.s.) katika hafla ya kuhuisha Usiku wa 21 wa Ramadhani, akiashiria kwamba kutokukubali ndio msingi wa utawala wa Alawi, alisema: Imam Ali (a.s) ni kielelezo cha ulimwengu wa Wanadamu.
-
Imam Ali (a.s) Katika Kurasa za Historia:
Elimu na Maarifa, Ibada na Ucha Mungu, Ujasiri na Ushujaa, na Upole na Huruma ya Imam Ali (a.s)
Imam Ali (a.s) alipigwa upanga na mtu aliyejulikana kwa jina la Abdur Rahman bin Muljim Muradi (laana iwe juu yake milele). Imam Ali (a.s) alikufa Shahidi siku tatu baadaye katika usiku wa 21 wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Imam Ali bin Abi Talib (a.s) ni shakhsia wa pili mkubwa katika Uislamu baada ya Mtukufu Mtume Muhammad (s.a.w.w), na anaelezwa katika historia ya Uislamu kuwa alikuwa jasiri na shujaa wa kupigiwa mfano, mwenye imani thabiti, mwenye akhlaki njema, mwenye elimu na uadilifu usio na kifani.
-
Wasifu wa Amirul Momineen (AS) unapaswa kuunganisha mwili wa Umma wa Kiislamu
Katika hotuba yake kwa mnasaba wa kuuawa shahidi Imam Ali, Waziri Mkuu wa Iraq alitaja fadhila za Imam Ali (a.s).
-
Wa Kwanza Kuitwa Amirul-Muuminina:
Mwenyezi Mungu (s.w.t) Alimpa Ali bin Abi Talib Lakabu ya “Amirul Muuminina”
Ukufungua kurasa za Historia ya Maisha yake safi ya Imam Ali bin Abi Talb (a.s), utamkuta kwamba yeye ni wa mwanzo katika kila kitu, kisha wengine wanafuata nyuma yake katika kitu hicho.
-
Kauli mbiu: Amani ya Palestina ni Amani ya Tanzania;
Majlis ya Siku ya Kupigwa Upanga Imam Ali (a.s), imefanyika katika Hawza ya Imam Sadiq (a.s), Kigogo, Dar-es-Salam, Tanzania
Maulana Sheikh Hemed Jalala: "Adui Ibn Muljim (laana iwe juu yake), aliyempiga Imam Ali (a.s) kwa upanga wenye sumu kali, alijua kuwa hawezi kupambana na Imam Ali (a.s) akiwa nje ya Msikiti, hivyo akaona mbinu aliyokuwa nayo ni kumuwinda akiwa katika ibada (swala), kwani awapo katika swala huwa mwili wake na hisia zake zinatoweka Duniani, na anazungumza na Mola wake Mtukufu kama vile hayupo Duniani".
-
Sehemu ya Fadhila za Kipekee za Imam Ali (a.s):
Imam Ali (a.s) ni Mtu wa Kwanza kuzaliwa ndani ya Msikiti na Kuuliwa ndani ya Msikiti
Imam Ali (a.s), Maisha yake yote yalikuwa ni Maisha ya kuweka uthabiti na kuimarisha nguzo na misingi ya Uislamu, pia kujitolea muhanga kwa kitu ghali na chenye thamani kubwa, ili kuhakikisha neno la Mwenyezi Mungu linakuwa juu, na neno la makafiri linakuwa chini.