Utawala
-
Aoun Aomba Shinikizo la Kimataifa dhidi ya Israel Kutekeleza Makubaliano na Kuondoka Lebanon
Rais wa Lebanon Joseph Aoun amemtaka Papa Leo XIV kusaidia kuongeza shinikizo la kimataifa kwa utawala wa Israel ili utekeleze “Makubaliano ya Mfumo”, usitishe mashambulizi na kuondoka kikamilifu katika maeneo ya Lebanon inayoyakalia.
-
Qaani: Utawala wa Kizayuni unasumbuliwa na “saratani ya kijamii”, kuanguka kutoka ndani ni hatima yake
Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) - ABNA - Kamanda wa Kikosi cha Quds, Brigedia Jenerali Ismail Qaani, amesema kuwa utawala wa Israel unasumbuliwa na kile alichokiita “saratani ya kijamii”, akisisitiza kuwa hatima yake ni kuanguka kutoka ndani.
-
Waziri Mkuu wa Malaysia: Kusimama imara kwa Iran dhidi ya uchokozi kunastahili pongezi
Waziri Mkuu wa Malaysia amelaani uchokozi wa kijeshi wa Marekani na utawala wa Kizayuni dhidi ya Iran, akisema kuwa msimamo, azma na uvumilivu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kukabiliana na mashambulizi hayo unastahili pongezi.
-
Iran: Taarifa ya Ufaransa na washirika wake wa Magharibi kuhusu haki za binadamu ni unafiki na kujipotosha
Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imelaani taarifa ya pamoja ya Ufaransa na baadhi ya nchi za Magharibi dhidi ya Iran, ikisema nchi hizo zinapaswa kuwajibika kwa ukiukaji wa haki za binadamu na sheria za kimataifa katika maeneo mbalimbali duniani.
-
Waziri wa Mambo ya Nje Iran: Marekani na Israel Ndio Chanzo cha Kukosekana kwa Usalama katika Mlango wa Hormuz
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amesema Marekani na utawala wa Israel ndio wahusika wakuu wanaopaswa kulaumiwa kwa ukosefu wa usalama na kukosekana kwa utulivu katika Mlango wa Hormuz, njia muhimu zaidi ya kimataifa ya usafirishaji wa nishati.
-
Brigedia Jenerali Hassan Zadeh: Marekani na utawala wa Kizayuni wameshindwa kufikia malengo yao dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
Kamanda wa Kikosi cha Muhammad Rasulullah (s) cha Tehran amesema kuwa kushindwa kwa Marekani na utawala wa Kizayuni kumedhihirisha uwezo mkubwa wa Iran, huku nguvu ya wananchi na utayari wa vikosi vya uhamasishaji ukiifanya Iran kuwa miongoni mwa nguvu kuu katika eneo na duniani.
-
Mhadhiri wa Sala ya Ijumaa Tehran: Makombora na Diplomasia Vimeimarisha Mizani ya Nguvu kwa Manufaa ya Iran
Mhadhiri / Khatibu wa Sala ya Ijumaa mjini Tehran amesema uwezo wa makombora ya Iran pamoja na diplomasia madhubuti ndivyo vilivyoimarisha mizani ya nguvu kwa manufaa ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, huku akisisitiza umuhimu wa kulinda mshikamano wa kitaifa na kuimarisha imani ya wananchi.
-
Kaimu Waziri wa Ulinzi wa Iran: Nchi za Kiislamu Lazima Zizuie Israel Kuchochea Mvutano Mashariki ya Kati
Waziri wa Ulinzi wa Iran (akikaimu), Brigedia Jenerali Majid Ibn al-Ridha, amesisitiza umuhimu wa kuanzishwa kwa mfumo wa pamoja wa kiusalama kati ya nchi za Kiislamu ili kuzuia utawala wa Israel kuchochea mivutano katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Qalibaf: Kulipiza kisasi kwa Kiongozi wa Mapinduzi ni kuwaweka huru Waislamu kutoka katika dhulma za Marekani na utawala wa Kizayuni
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema kuwa njia ya kuenzi urithi wa Kiongozi Shahidi wa Umma wa Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, ni kuendelea kuiunga mkono Kambi ya Muqawama, hususan Lebanon, na kupambana na ubeberu wa Marekani na utawala wa Kizayuni.
-
Mahakama ya Damascus Yaanza Kesi dhidi ya Aliyekuwa Mufti wa Syria, Ahmad Hassoun, kwa Tuhuma za Kuhamasisha Uhalifu wa Kivita
Mahakama ya Jinai ya Nne mjini Damascus imeanza kusikiliza kesi dhidi ya aliyekuwa Mufti wa Jamhuri ya Syria, Ahmad Hassoun, anayekabiliwa na tuhuma za kuchochea mauaji, kuhalalisha uhalifu wa kivita na kutoa uungwaji mkono wa kidini na kisiasa kwa utawala wa zamani wa Bashar al-Asad na washirika wake.
-
Umoja wa Ulaya Washindwa Kufikia Makubaliano Kuhusu Kumuwekea Vikwazo Itamar Ben-Gvir
Msemaji wa masuala ya nje wa Tume ya Ulaya amesema kuwa nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya hazikufikia mwafaka kuhusu pendekezo la kumuwekea vikwazo Waziri wa Usalama wa Ndani wa Israel, Itamar Ben-Gvir, huku zikilaani kauli zake za uchochezi dhidi ya Lebanon.
-
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi la Iran Latangaza Kufungwa kwa Mlango wa Bahari wa Hormuz
Jeshi la Wanamaji la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC Navy) limetangaza kuwa Mlango wa Bahari wa Hormuz umefungwa kwa meli zote na kuonya kuwa chombo chochote kitakachoukaribia kitakuwa kinahatarisha usalama wake.
-
Qalibaf: Vikosi vya Israel Vinapaswa Kujiondoa Kusini mwa Lebanon
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesisitiza kuwa vikosi vya Israel vinapaswa kujiondoa kusini mwa Lebanon ili wananchi warejee makwao kwa heshima, huku Spika wa Bunge la Lebanon, Nabih Berri, akiishukuru Iran kwa mchango wake katika juhudi za kusitisha vita.
-
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya (S) Yaionya Israel: Mashambulizi dhidi ya Lebanon Yakendelea, Iran Itajibu kwa Nguvu
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya (S) yameionya Israel kwamba ikiwa itaendelea na mashambulizi dhidi ya kusini mwa Lebanon na kukiuka makubaliano ya usitishaji mapigano, itakabiliwa na jibu kali kutoka kwa Vikosi vya Wanajeshi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Mamilioni ya Wairaq Kuitikia Wito wa Kushiriki Mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi
Takribani Wairaq milioni moja wanatarajiwa kushiriki mazishi ya kiongozi shahidi wa Mapinduzi, huku zaidi ya nusu milioni wakitarajiwa kuingia Iran kupitia mpaka wa Mehran kuelekea Tehran, Qum na Mashhad kwa ajili ya maombolezo.
-
Iran: "Vitendo vya Israel Vimegeuka Fursa ya Kuimarisha Mhimili wa Muqawama"
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema vitendo vya Israel havikuvuruga maslahi ya Iran na Lebanon, bali vimeimarisha mshikamano na kuongeza nguvu za Mhimili wa Muqawama katika kukabiliana na Israel.
-
Qalibaf: Muqawama wa Lebanon na Diplomasia ya Iran Vinahakikisha Uhuru na Uadilifu wa Ardhi ya Lebanon
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema jihadi ya Muqawama wa Kiislamu nchini Lebanon pamoja na diplomasia madhubuti ya Iran vinahakikisha mamlaka na uadilifu wa ardhi ya Lebanon, akisisitiza kuwa maadui hawataweza kamwe kuitenga au kuisambaratisha nguzo yoyote ya Muqawama.
-
Waziri wa Utamaduni wa Iran: Mshikamano kati ya Iran na Lebanon ni Hitaji la Kimkakati la Kujilinda
Waziri wa Utamaduni na Mwongozo wa Kiislamu wa Iran amesema kuwa Iran na Lebanon wanakabiliwa na adui mmoja wa pamoja, na kwamba kuimarisha mshikamano kati ya mataifa hayo mawili si suala la hisia za kibinadamu pekee, bali ni hitaji la kimkakati katika kujilinda dhidi ya vitisho vya pamoja.
-
Qalibaf: Marekani Italazimika Kubeba Gharama ya Uhalifu wa Utawala wa Kizayuni nchini Lebanon
Kwa Mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) – ABNA – Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, ametoa onyo kali kwa Marekani kufuatia mashambulizi makali yanayoendelea kufanywa na utawala wa Kizayuni nchini Lebanon, akisema kuwa Washington italazimika kubeba gharama ya uhalifu huo. Kwa mujibu wa Shirika la Habari la IRNA, Qalibaf aliandika katika ukurasa wake kwenye mtandao wa X siku ya Jumatatu kwamba kuzingirwa kwa njia za baharini na kuongezeka kwa vitendo vinavyotajwa kuwa uhalifu wa kivita dhidi ya wananchi wa Lebanon ni ushahidi wa wazi kwamba Marekani haijaheshimu makubaliano ya kusitisha mapigano. Spika huyo wa Bunge la Iran alisisitiza kuwa kila hatua inayochukuliwa katika medani ya kisiasa na kijeshi ina gharama zake, akionya kuwa wale wanaounga mkono au kufumbia macho mashambulizi hayo hawataepuka kuwajibika kwa matokeo yake. Qalibaf aliongeza kuwa kuendelea kwa mashambulizi dhidi ya Lebanon kunathibitisha ushiriki wa Marekani katika kutoa uungaji mkono wa kisiasa na kijeshi kwa utawala wa Kizayuni, jambo ambalo, kwa mujibu wake, linachangia kuongezeka kwa mzozo na mateso ya raia wasio na hatia. Kauli hiyo imekuja wakati mashambulizi ya Israel dhidi ya maeneo mbalimbali ya Lebanon yakiendelea kuzua wasiwasi mkubwa wa kimataifa kuhusu usalama wa raia na hatari ya kupanuka kwa mzozo katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Iran Yajibu Shambulio la Marekani, Yalenga Kituo cha anga Kilichotumika Kushambulia Kisiwa cha Sirik
IRGC imesema imeharibu kituo cha anga kilichotumika katika shambulio dhidi ya mnara wa mawasiliano wa Kisiwa cha Sirik na kuonya kwamba mashambulizi yoyote yatakayojirudia yatakabiliwa na jibu kali zaidi.
-
Iran: Mfumo wa Sasa wa Utawala wa Dunia Unakabiliwa na Mgogoro wa Imani na Uhalali
Balozi wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema jamii ya kimataifa inashuhudia kuongezeka kwa migogoro, ukosefu wa usawa na kudhoofika kwa diplomasia, huku akisisitiza umuhimu wa kuheshimu sheria za kimataifa na kuimarisha ushirikiano wa kweli wa kimataifa.
-
Ayatllah Hosseini Gorgani amesisitiza kuwa:
Fiqh ya Usimamizi Ina Historia Ndefu | Utendaji wa vitendo unaoendana na Qur’an ni muhimu katika utawala na usimamizi wa umma
Mwalimu wa Dars-e-Kharij katika Hawza Ilmiyya ya Qom amesema kuwa kuunda serikali na utawala na manabii wa Mungu si jambo jipya, na Qur’an kwa uwazi inataja mtindo wa utawala wa baadhi ya manabii.
-
Waziri wa Ulinzi wa Pakistan, Khawaja Muhammad Asif: "Pakistan haitasita kufanya mashambulizi ya anga ndani ya Afghanistan ikiwa itahitajika"
Khawaja Asif, Waziri wa Ulinzi wa Pakistan, ameeleza kuwa Islamabad haitakosa kufanyia mashambulizi ya anga ndani ya Afghanistan ikiwa itaona ni lazima, chini ya utawala wa Taliban. Alidai kwamba makundi ya silaha yanayofanya operesheni kutoka ardhi ya Afghanistan yanaingiliana katika mashambulizi dhidi ya Pakistan.
-
Jumuiya ya Kiislamu Bangladesh: Waislamu Bilioni Mbili Wako Pamoja na Iran kwa Roho na Mali
Jumuiya ya Kiislamu ya Bangladesh imetoa tamko rasmi ikitangaza uungaji mkono wake kamili kwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, na kuonya kuwa shambulio lolote la kijeshi dhidi ya Iran litakabiliwa na mwitikio mpana wa Waislamu duniani. Katika tamko hilo imesema: “Ingawa viongozi wa baadhi ya nchi za Kiislamu wanategemea Marekani na Israel, lakini Waislamu bilioni mbili duniani wamesimama pamoja na Palestina. Ikiwa uvamizi wa kijeshi utafanywa dhidi ya Iran, Waislamu kote duniani wataingia uwanjani kwa mali na nafsi zao; na kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, utawala ghasibu wa Kizayuni wa Israel utaanguka hivi karibuni.”
-
Makubaliano ya Al-Julani na Wazayuni chini ya kivuli cha Washington
Pendekezo jipya la Washington la Ushirikiano wa Kijamii Kati ya Syria na Utawala wa Kizayuni. Pendekezo jipya la Marekani la ushirikiano wa usalama kati ya Syria na utawala wa Israel linaonekana kama hatua mpya kuelekea kuhalalisha na kudumisha ukoloni, likifanyika chini ya usimamizi wa moja kwa moja wa Marekani.
-
Katika ujumbe kwa Mkutano wa Mwaka wa Umoja wa Vyama vya Wanafunzi wa Kiislamu barani Ulaya; Kiongozi wa Mapinduzi:
Hitaji kuu la dunia leo ni mfumo wa haki wa kitaifa na kimataifa wa Kiislamu / Shambulio la Marekani lilishindwa mbele ya ujasiri wa vijana wa Iran
Ayatollah Khamenei, katika ujumbe wake kwa Mkutano wa 59 wa Mwaka wa Umoja wa Vyama vya Wanafunzi wa Kiislamu barani Ulaya, amesisitiza kuwa sababu kuu ya msukosuko na wasiwasi wa madhalimu wafisadi si suala la nyuklia, bali ni kuinuliwa kwa bendera ya kupinga mfumo usio wa haki na utawala wa mabavu wa mfumo wa ubeberu duniani, pamoja na mwelekeo wa Iran ya Kiislamu kuelekea kujenga mfumo wa haki wa kitaifa na kimataifa wa Kiislamu.
-
Kufichuliwa kwa muundo wa siri wa utawala wa Kizayuni kwa ajili ya kukwepa uwajibikaji / Haki iko chini ya upanga wa fedha na nguvu ya utawala
Tovuti ya Kifaransa Mediapart, kwa ushirikiano na vyombo vingine nane vya habari vya Ulaya, kupitia mradi unaoitwa “Faili za Utawala wa Kizayuni”, imefichua kuundwa kwa kitengo cha siri ndani ya Wizara ya Sheria ya utawala huo.
-
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Minnesota Afichua “Mkakati wa Kipuuzi” wa Marekani dhidi ya Iran
Anakanusha madai ya Tom Barrack kuhusu kuachwa kwa sera ya kuuangusha utawala wa Iran.
-
Sheikh Naim Qassem:
Lebanon inapaswa kukabiliana kikamilifu na uvamizi wa kibeberu wa utawala wa Kizayuni | Mashahidi walijitolea kwa roho, mali na kila walichokuwa nacho
Lebanon inakabiliwa na uvamizi hatari wa Kizayuni: Akirejea mashambulizi ya mara kwa mara ya Israel kusini mwa Lebanon, alisema: “Lebanon inakabiliwa na uvamizi wa hatari na wa kupanua mipaka wa utawala wa Kizayuni. Lazima tukabiliane nao kwa kila njia na mbinu. Adui huyu haheshimu makubaliano yoyote.”
-
Umoja wa Waislamu na kuunga mkono Iran kama mstari wa mbele wa kulinda Quds ni jambo la lazima
Mwanafikra mashuhuri wa Algeria amesisitiza kuwa umoja wa Waislamu, kuacha misimamo ya chuki za kimadhehebu na kuunga mkono Iran kama ngome ya mbele ya kulinda Quds (Msikiti wa Al-Aqsa) na Umma wa Kiislamu ni jambo la lazima, na kwamba mataifa pamoja na wanazuoni wa Kiislamu wanapaswa kusimama bega kwa bega na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika nyanja za vyombo vya habari, siasa, utamaduni na usalama.