Mohammad Ali Jamoul, Kamanda wa kikosi cha Makombora cha Harakati ya Hizbullah, ameuawa Kigaidi kufuatia shambulio la ndege isiyo na rubani (drone) lililofanywa na utawala haram wa Kizayuni (Israel). Shambulio hili linaonekana kuwa sehemu ya mfululizo wa mashambulizi ya Israel dhidi ya viongozi na miundombinu ya Hizbullah.
Waziri wa Mambo ya Nje wa UAE Abdullah Bin Zayed amejadili uhusiano wa pande mbili katika mkutano wake na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kizayuni Gideon Sa'er huko Abu Dhabi. Katika kikao hicho amesisitiza juhudi za kidiplomasia za kufikia usitishaji vita huko Ghaza, lakini mkutano huu ulifanyika katika hali ambayo utawala wa Kizayuni unaendelea kuua na kufanya mauaji ya kimbari huko Ghaza.