-
Moja ya Matukio Muhimu Katika Ratiba za Mwezi wa Muharram Katika Masjidul Ghadir ni Hafla ya Kupandisha Bendera ya Imam Hussein (as) + Picha
Kupandishwa kwa Bendera hiyo ni ishara ya msimamo wa milele wa haki dhidi ya dhulma, na ni mwaliko kwa Waumini kujiandaa kuhudhuria katika Majalisi, kushiriki katika kuandaa Mashairi, na khutba mbalimbali zinazobainisha ujumbe wa Karbala na mafundisho ya Imam Husein (a.s).
-
Majlis za Maombolezo ya Shahada ya Imam Hussein(as) kwa Kina Mama wa Kiislamu nchini Tanzania zinaendelea kufikisha Ujumbe wa Imam Hussein (as) +Picha
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Majlis ya Imam Husein (as) ikiendeshwa makhsusi kwa Kinamama inaendelea kila siku ikiongozwa na Ustadhati Zainab Ndete.Waumini mbalimbali Wanawake wa Kiislamu wanajitokekeza kutoka maeneo mbalimbali na kukusanyika kwa Pamoja kwa ajili ya kupata Darsa mbalimbali zilizomo ndani ya Mapinduzi Matukufu ya Kiislamu ya Karbala, yaliyosimamiwa kikamilifu na Imam Hussein (as) Katika Ardhi ya Karbala.
-
Uanzishwaji wa Mawkib ya Aba Abdillah Al-Hussein(as) - Ulongoni B, Dar es Salaam, Tanzania ikiendeshwa na Husseiniyyah ya Hazrat Qamar Bani Hashim(as)
Mawkib hii, huduma mbalimbali za kijamii zinatolewa kwa Wananchi wa maeneo hayo, sambamba na kusambaza ujumbe wa Aba Abdillah Al-Hussein (as) wa kuhuisha maadili na misingi ya Kiislamu; kuhimiza kusema ukweli na haki, pamoja na kueneza uadilifu kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya Binadamu.
-
Madrasat Hazarat Zainab (sa) - Kigamboni ni kielelezo cha Nafasi ya Wanawake Katika Kuhifadhi Utamaduni wa Muharram
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Majalisi na vikao mbalimbali vya kuhuisha Shahada ya Imam Hussein (as) vinaendelea katika Madrasa ya Kidini ya Wasichana wa Kiisalamu inayoitwa: Madrasat Hazrat Zainab (sa) - Kigamboni, Dar-es-Salam - Tanzania.
-
Mimbari ya Imam Hussein (as) - Nchini Malawi | "Tofauti kati ya Mtu anayemjua Imam Hussein (AS) na Asiyemjua Imam Hussein (as)"
Sheikh Abdul Rahman Kachere: "Mtu anayemfahamu Imam Hussein (AS) daima ni jasiri katika kukabiliana na dhulma".Kumjua vizuri Imam Hussein (as) kutawafanya watu wa mataifa mbalimbali kumpinga adui na dhalimu, na kutambua njama za adui na dhalimu dhidi ya mataifa yao, na kuwa tayari kupambana kwa ajili ya kuinusuru Haki, kwa ajili ya kuondoa uistikbari, dhulma na unyonyaji wa mfumo mpya wa ukoloni unaoitwa: Ukoloni mambo leo.
-
Bilal Moshi | Waumini wengi wa Kiislamu wanaendelea kuifuatilia Misheni ya Imam Hussein(as)na kutofautisha baina ya Haki na Batili ya Yazid Bin Muawia
Shirika la Habari la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Majlisi ya Imam Hussein (as) imefanyika katika kituo cha Bilal Muslim Mission of Tanzania - Moshi Mjini. Waumini mbalimbali wanajitokeza kwa wingi kila siku kushiriki katika Majalis za Aba Abdillah Al-Hussein zinazofanyika katika vituo mbalimbali vya Bilal Muslim Mission of Tanzania. Ujumbe wa Imam Hussein (as) na Mapinduzi yake ya Karbala vinazidi kueleweka zaidi kwa umma wa kiislamu na kuhuishwa zaidi kila mwaka na sasa waumini wengi wanaijua na kuendelea kuijua misheni ya Imam Hussein (as) na Falsafa yake.
-
Nafasi ya Mwanamke katika Harakati ya Mabadiliko ya Imam Hussein (a.s) | Madrasat Hazrat Zainab (sa) - Kigamboni - Dar-es-salaam + Picha
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Majlisi ya Siku ya 6 ya Maombolezo ya Shahadat ya Imam Hussein (as) imefanyika katika Madrasat ya Wasichana wa Kiislamu ya Hazrat Zainab (sa), iliyopo Kigamboni Jijini Dar-es-salaam. Ushiriki Mzuri wa Mabanati wa Kiislamu katika kuhuisha Ujumbe wa Mapinduzi ya Imam Hussein (as), ni katika muendelezo wa ukweli ule halisi kwamba Mwanamke wa Kiislamu alikuwa mshirika wa msingi katika kuendeleza na kuhifadhi mafanikio ya harakati ya Imam Hussein (a.s). Kwa maana kwamba: Uwepo wa Wanawake katika tukio la Karbala haukuwa wa bahati (au wa kubahatisha) au jambo la ghafla, bali ulikuwa sehemu ya mpango wa kimkakati uliopangwa na Imam Hussein (a.s) mwenyewe - ili kuonyesha ulimwengu kuwa Mwanamke ana nafasi ya kuchukua maamuzi muhimu na kuyatetea kwa ujasiri mkubwa.
-
Muendelezo wa Majlisi za Imam Hussein(as) - Madrasat Hazrat Zainab(sa) Kigamboni - Dar-es-Salaam | Mada: "Masomo Tunayojifunza Kutoka Karbala"
Khatiba wa Majlis hii, (Fatima Mauga) alizungumzia mada muhimu iliyoitwa: "Masomo tunayojifunza kutoka Karbala". Katika mada hiyo, alijikita zaidi katika kufafanua na kudadavua nukta muhimu inayomhusu Mwanamke wa Kiislamu, ambayo aliipatia anuani isemayo: "Tunajifunza nini sisi kama Wanawake wa Kiislamu kutokana na yale maarifa tuliyojifunza, na upi wajibu wetu kwa wakati huu wa sasa?".
-
Maulana Sayyid Arif Naqvi: "Tumjue zaidi Imam Hussein (as) Kupitia Usomaji, Tafakuri, na Kuhudhuria Majlisi za Muharram" + Picha
Majlisi hii muhimu ilihudhuriwa na Waumini takriban 300 kutoka maeneo mbalimbali, waliokusanyika kwa pamoja kwa ajili ya kuadhimisha na kutafakari juu ya msimamo wa Imam Hussein (as) na ujumbe wake wa haki, uadilifu, na kujitolea kwa ajili ya kuihami na kuidumisha Dini Tukufu ya Mwenyezi Mungu (s.w.t).
-
Ripoti ya Picha | Marasimu (Hafla) ya Maombolezo ya Usiku wa nne wa Muharram katika Haram ya Sayyid Alauddin Hussein (AS)
Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Ahlul Bayt (AS) - ABNA - Marasimu ya maombolezo ya Mazuwwari katika Haram Tukufu ya Sayyid Alauddin Hussein (AS) ilifanyika usiku wa nne wa Muharram. Zifuatazo ni picha kadhaa za tukio za Majlisi hiyo.
-
Mbauda - Arusha, Tanzania | Waumini wa Kiislamu wakiwa katika Majlis ya Maombolezi ya Shahada ya Imam Hussein (as) + Picha
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Majalisi za Maombolezo ya Shahada ya Aba Abdillah Al-Hussein (as) na Mashahidi wa Karbala zinaendelea kila siku Jijini Arusha katika vituo mbalimbali vya Taasisi ya Khatamul-Anbiyaa, na waumini wengi kutoka maeneo mbalimbali ya Jiji la Arusha wanahudhuria katika Husseiniyyah na Misikitini kwa ajili ya kusikiliza masomo maridhawa yaliyopo katika harakati ya Mapinduzi Adhimu ya Kiislamu ya Imam Hussein (as).
-
Mfululizo wa Majlisi za Muharram Zinaendelea katika Chuo cha Al-Mustafa (s), Dar es Salaam | Mafunzo Kuhusu John, Sahaba Mtiifu wa Imam Hussein(as)
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) - ABNA- Majalis za Maombolezo ya Mwezi wa Muharram katika Chuo cha Jamiat Al-Mustafa International Foundation - Dar es Salaam, Tanzania zinaendelea kwa kila Siku, na Leo hii ilikuwa ni Sehemu ya Mfululizo wa Vikao hivyo vya Mwezi wa Muharram, ambapo mada muhimu imetolewa kuhusiana na: "Utambulisho wa John, Shahidi wa Karbala". Mada hii imebainishwa kupitia Khatibu wetu wa leo: Sheikh Abubakar Matulia na ametoa ufafanuzi wa kina zaidi kuhusiana na Maisha ya John, Sahaba wa Imam Hussein (as) aliyepigana vita vya Karbala sambamba na Mashahidi wa Karbala, akiwa ni mtu wa Jamii ya Kiafrika.
-
Arusha Mjini | Majalis za Maombolezo ya Muharram Katika kuenzi Mapinduzi ya Karbala zinaendelea Jijini Arusha
Kwa Mujibu wa Ripoti ya Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Vikao mbalimbali vya kuhuishwa kumbukumbu ya Karbala na Mapinduzi Matukufu ya Imam Hussein (as) zinaendelea katika Mji wa Arusha. Kila Siku ambapo Waumini kutoka maeneo mbalimbali wanakusanyika na kuhudhuria kwa wengi katika maeneo ya Husseiniyyah na Misikitini kwa ajili ya Kusikiliza Historia halisi ya Imam Hussein (as) na Mapinduzi adhimu aliyoyafanya katika kupinga dhulma na kuhuisha Haki na Uadilifu na kurudisha Heshima ya Uislamu na Waislamu bali Wanadamu wote, mambo ambayo adui wa Uislamu Yazidi bin Muawia alilenga kutafyekelea mbali na kueneza ufisadi Mkubwa uliokithiri ardhini.
-
Malawi | Majlisi za Muharram na Maombolezo ya Shahadat ya Imam Hussein (as) zikiendelea chini ya Usimamizi wa Jamiat Al-Mustafa (s) - Malawi
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Vikao (Majalis) mbalimbali za Maombolezo ya Shahadat ya Imam Hussein (as) Katika Mwezi huu Mtukufu wa Muharram - 1447 Hijria, zinaendelea kila Siku Nchini Malawi chini ya Usimamizi wa Jamiat Al-Mustafa (s) - Malawi. Waislamu Kote Duniani hususan Wapenzi wa Haki na wachukiao dhulma, wanaendelea kumuezi na kumkumbuka Imam Hussein (as), Mjukuu wa Mtume (saww), na kuisha Malengo Matukufu ya Mapinduzi yake aliyoyafanya katika Ardhi ya Karbala.
-
Majlisi za Maombolezo ya Muharram - Zinaendelea Mkoani Kigoma, Tanzania
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) - ABNA- Katika Picha ni Majlisi ya Pili ya Maombolezo ya Shahadat ya Imam Hussein (as) na Mashahidi wa Karbala, iliyofanyika Mkoani Kigoma, Tanzania, Khatibu akiwa ni Samahat Sheikh Shaban Mussa.
-
Sala ya Ijumaa, Jamiat Al-Mustafa (s)- Dar-es-salaam, Tanzania | "Jinsi ya kuishi Katika Mwezi wa Muharram Kulingana na Matukio Muhimu ya Mwezi huu"
Mada hii kwa hakika ni yenye umuhimu mkubwa kwani inawasaidia Waislamu kufahamu jinsi ya kuishi kwa kuzingatia mafunzo ya A'shura, kama vile: Ustahamilivu, kuinusuru haki, na kupigania ukweli na uadilifu hata kama ni kwa gharama ya kuyatoa muhanga maisha yako kwa ajili ya Uislamu.
-
Majlisi ya Muharram - Madrasat Hazrat Zaynab (SA): "Muslim bin Aqil (RA) na mchango wake muhimu katika historia ya Uislamu" + Picha
Majlisi hii imeandaliwa na kuratibiwa na Madrasat ya Mabinti ya Hazrat Zainab (sa) iliyopo Kigamboni, Jijini Dar-es-salaam. Hii inaonyesha umuhimu wa pekee wa Wanawake wa Kiislamu katika kuandaa na kushiriki kwenye shughuli za kidini na kitamaduni.
-
Majlis ya Muharram - Jamiat Al-Mustafa - Dar-es-salaam | Mada ya Leo: "Umuhimu wa Muslim bin Aqil (RA) na tukio la kihistoria la Karbala" + Picha
Khatibu, Sheikh Khalfan Katundu, katika Khutba yake ametanabahisha kuwa matukio kama vile tukio la "Muslim bin Aqil (RA)" yana umuhimu mkubwa kwa jamii zote za Kiislamu. Kwa mfano, vijana wa Kiislamu nchini Tanzania wanaweza kuelimishwa kuhusu thamani ya ushujaa, utoaji sadaka na kujitolea kijamii na kidini, na kuwa na Mapenzi makubwa kwa Haki na Uadilifu kupitia Hadithi na Hikaya za Matukio mbalimbali ya Karbala.
-
Pezeshkian: Shambulio kwenye taasisi za nyuklia ni kielelezo tosha kuwa Marekani ni msababishaji mkuu wa hatua za uhasama za Kizayuni dhidi ya Iran
Jibu kali la Iran lilikuwa ujumbe wa wazi kwa wahalifu wa Kizayuni. Marekani, baada ya majibu makali na ya kuadabisha kutoka kwa vikosi vya ulinzi vya nchi yetu, na kuona udhaifu na ulegeaji wa wazi wa utawala wa Kizayuni, hawakuweza kuvumilia ispokuwa kutojitokeza na kuamua kujitumbukiza rasmi kwenye dimbwi la uhasama."
-
Kwa mara ya kwanza, Iran imeshambulia Utawala wa Israel kwa kutumia kombora hatari la Khaibar lenye kutumia Lenzi + Video
Shirikja la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) - ABNA- Jeshi la IRGC limethibitishia kuwa limetumia makombora yenye kutumia teknolojia ya lenzi, aina ya Khaibar, asubuhi ya leo (22 - 06- 2025). Makombora hayo hatari yenye uawezo wa kubeba ndani yake rekoti zaidi ya 26, yameyatwanga maeneo mbalimbali na muhimu ndani ya Israel.
-
Hapa ni Israel sio Ghaza! | Tizama Makombora ya Iran leo hii asubuhi yalivyoichakaza Israel na kuigeuza kichwa chini miguu juu + Video
Shirika la Habari la Kimatifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Leo hii asubuhi, Jamhuri ya kiislamu ya Iran ilifanya shambulizi kali la makombora katika maeneo mbalimbali ya Palestina yanayokaliwa kimabavu na Utawala Haram wa Israel. Picha zinaonyesha jinsi maeneo yaliyolengwa katika shabaha jinsi yalivyosambaratishwa kikamilifu. Jeshi la Iran limetoa taarifa kuwa limelenga maeneo ya kijeshi na kiistratejia ndani kabisa ya Israel na Makombora yote yamepiga shabaha zake kwa mafanikio makubwa.
-
Haram ya Imam Hussein (as) yapambwa kwa vitambaa vyeusi sambamba na kukaribia Mwezi wa Huzuni wa Muharram + Picha
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Haram Tukufu ya Imam Hussein (as) Nchini Iraq, imepambwa rasmi kwa vitambaa vyeusi katika kujiandaa kuadhimisha Siku za Maombolezo na Majonzi za ndani ya Mwezi wa Huzuni wa Muharram.
-
Jenerali Naeini: Makombora ya IRGC yaligonga pointi 14 za kijeshi za Kizayuni jana usiku + Picha
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Msemaji na Naibu Mkuu wa Mahusiano ya Umma wa IRGC: Matokeo ya Mashambulizi ya Makombora ya Iran kwenye maeneo ya Palestina yanayokaliwa kimabavu na Utawala haram wa Israel, katika Mashambulizi ya wimbi la 18, yalilenga kwa mafanikio maeneo 14 ya kijeshi ya kimkakati huko Haifa na Tel Aviv.
-
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini | "Tunasimama bega kwa bega na Iran"
Amesisitiza kuwa: Serikali na wananchi wa Afrika Kusini wanalaani vitendo vya kinyama vya utawala wa kibaguzi wa Israel dhidi ya wananchi wa eneo la kikanda hususan watu wa Palestina, Lebanon na Iran.
-
Zakzaky: Mashambulizi ya kigaidi ya Israel yanapasa kulaaniwa duniani kote
Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu nchini Nigeria (IMN), Sheikh Ibrahim Zakzaky amelaani mashambulizi ya Israel dhidi ya Iran na kuelezea hujuma hizo za utawala wa Kizayuni dhidi ya nchi huru kuwa ni kitendo cha juu zaidi cha uchokozi, kinachopaswa kulaaniwa duniani kote.
-
Qari maarufu wa Misri, Sheikh Taruti, afungamana na Iran katika kukabiliana na Israel
Qari mashuhuri wa Misri, Sheikh Abdul Fattah Taruti, ametangaza kufungamana na watu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kukabiliana na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Sherehe ya Eid ya Ghadir - Hawza ya Hazrat Zainab (sa) Kigamboni - Dar-es-Salaam, Tanzania + Picha
Katika sehemu ya sherehe, mmoja wa wanafunzi wa muhula wa tano alitoa hotuba juu ya umuhimu wa kujifunza na kufundisha suala la Wilayat (Kufuata uongozi wa kiroho wa Amirul-Muuini Ali bin Abi Tali na Ahlul-Bayt amani iwe juu yao).
-
Sala ya Ijumaa | Imeswaliwa katika Kituo cha uwakilishi wa Chuo Kikuu cha Al-Mustafa (s.a.w.w) nchini Malawi
Katika Khutba yake, alizungumzia umuhimu wa Siku ya Ghadir katika historia ya Uislamu, akieleza vipengele vyake vya kiitikadi na kijamii, pamoja na nafasi yake katika kuimarisha dhana ya Uwilaya katika Uislamu.
-
Jamiat Al-Mustafa (s) Malawi | Kikao cha Kitaaluma Kuhusu Eid -ul- Ghadir + Picha
Shirika la Habari la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Kwa kuzingatia umuhimu wa nafasi ya Uimamu katika fikra ya Kiislamu na nafasi maalumu ya Imam Ali bin Abi Talib (a.s) kama Imamu na Khalifa wa kwanza kwa Mujibu wa Wafuasi wa Ahlul-Bayt (as) na Mrithi wa Mtume Muhammad (s.a.w.w), mkutano wa kitaaluma kwa anuani: Ghadir: Misingi, Ushahidi na Matokeo ya Kihistoria* umefanyika Nchini Malawi katika Kituo cha Kielimu cha Jamiat Al-Mustafa (s).
-
Majlis ya Kuzaliwa kwa Imam Hadi (as) Zanzibar + Picha
Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Wanafunzi wa Madrasa ya Qur'an Tukufu - Zanzibar, wamehuisha Siku adhimu ya Kuzaliwa kwa Imam Al-Hadi (as) kwa kufanya Majlisi Muhimu ya Kuzungumzia Sifa na Fadhila za Imam Al-Hadi (as).