Kwa Mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Iraq, Mohammad Kazem Al-Sadeq, amekutana na Patriarki mpya wa Kanisa la Kaldania nchini Iraq na duniani, Mtakatifu Mar Paulus III Nona, katika makao makuu ya patriarkia jijini Baghdad kufuatia sherehe za kutawazwa kwake rasmi.
Mkutano huo ulihudhuriwa pia na mwakilishi wa Wakristo wa Ashuri na Wakaldania katika Bunge la Iran, Charlie Anouyeh Tekiyeh. Katika mazungumzo hayo, Balozi Al-Sadeq alimpongeza Patriarki mpya kwa kuchukua nafasi hiyo muhimu ya kidini, akimtakia mafanikio katika kuimarisha mshikamano wa kijamii na maelewano miongoni mwa wananchi. Aidha, alieleza kuwa hali ya utulivu inayoshuhudiwa katika eneo hilo ni matokeo ya kujitolea na kujitoa mhanga kwa mataifa ya eneo hilo.
Kwa upande wake, Charlie Anouyeh Tekiyeh alizungumzia hali ya wafuasi wa dini mbalimbali nchini Iran, akisisitiza kuwa msaada unaotolewa na serikali ya Iran kwa makundi ya dini tofauti ni mfano wa kuigwa wa kuishi kwa amani na kuheshimiana. Pia alilaani vikali vitendo vya uchokozi vinavyofanywa na utawala wa Kizayuni dhidi ya mataifa na wananchi wa eneo hilo.
Mwishoni mwa mkutano huo, Patriarki Mar Paulus III Nona alikaribisha ziara ya ujumbe wa Iran na kueleza matumaini yake ya kuitikia mwaliko wa kutembelea Iran katika wakati mwafaka, kwa lengo la kuimarisha mahusiano na maelewano kati ya viongozi wa dini mbalimbali.
Your Comment