Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA-, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmaeil Baghaei, amesema kuwa matukio yaliyotokea usiku uliopita yamethibitisha azma ya vikosi vya ulinzi vya Iran katika kulinda uhuru na usalama wa taifa.
Baqaei alieleza kuwa vikosi vya silaha vya Iran vimeonyesha kwa vitendo kuwa havitasita kujibu kwa uthabiti wowote uchokozi au tishio dhidi ya nchi, akisisitiza kuwa hatua za kujihami zitachukuliwa wakati wowote zitakapohitajika.
Akizungumzia masuala ya kidiplomasia, msemaji huyo aliikosoa Marekani kwa kile alichokitaja kuwa ni kudhoofisha juhudi za mazungumzo kupitia kutuma ujumbe unaokinzana na kuendelea kukiuka makubaliano ya usitishaji vita.
Alisema kuwa ili mchakato wowote wa kidiplomasia uweze kusonga mbele kwa mafanikio, ni lazima kuwe na kiwango cha chini cha mazingira yanayofaa, yakiwemo uaminifu, uthabiti wa kisiasa na kuheshimiwa kwa makubaliano yaliyofikiwa.
Baqaei alisisitiza kuwa Iran inaendelea kuunga mkono njia za kidiplomasia, lakini mafanikio ya juhudi hizo yanategemea pia mwenendo wa upande mwingine na kujitolea kwake kwa vitendo katika kuheshimu ahadi na makubaliano ya kimataifa.
Your Comment