Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA-, Gazeti la Kizayuni Yedioth Ahronoth limeripoti kuwa utawala wa Kizayuni wa Israel unakabiliwa na wimbi ambalo halijawahi kushuhudiwa la vikwazo, shinikizo na uhasama kutoka kwa jumuiya ya kimataifa tangu Oktoba 2023.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo iliyochapishwa siku ya Ijumaa, hatua hizo zimejumuisha kutolewa kwa hati za kukamatwa dhidi ya baadhi ya viongozi wa Israel, pamoja na maamuzi ya baadhi ya nchi kuwazuia mawaziri na maafisa wa utawala wa Tel Aviv kuingia katika maeneo yao.
Gazeti hilo limesema kuwa hali hiyo inaonyesha kuongezeka kwa upinzani wa kimataifa dhidi ya sera za utawala wa Kizayuni, huku likibainisha kuwa Israel inakabiliwa na changamoto kubwa zaidi za kidiplomasia na kisiasa katika miaka ya hivi karibuni.
Your Comment