Kizayuni
-
Hezbollah Yalaani Kuendelea kwa Mashambulizi ya Utawala wa Kizayuni Dhidi ya Lebanon
Hezbollah ya Lebanon imelaani kuendelea kwa mashambulizi ya utawala wa Kizayuni dhidi ya Lebanon, ikisema kuendelea kwa uvamizi, mauaji na uharibifu kunaonyesha kushindwa kwa mchakato wa mazungumzo ya moja kwa moja na makubaliano ya mfumo.
-
Qaani: Utawala wa Kizayuni unasumbuliwa na “saratani ya kijamii”, kuanguka kutoka ndani ni hatima yake
Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) - ABNA - Kamanda wa Kikosi cha Quds, Brigedia Jenerali Ismail Qaani, amesema kuwa utawala wa Israel unasumbuliwa na kile alichokiita “saratani ya kijamii”, akisisitiza kuwa hatima yake ni kuanguka kutoka ndani.
-
Waziri Mkuu wa Malaysia: Kusimama imara kwa Iran dhidi ya uchokozi kunastahili pongezi
Waziri Mkuu wa Malaysia amelaani uchokozi wa kijeshi wa Marekani na utawala wa Kizayuni dhidi ya Iran, akisema kuwa msimamo, azma na uvumilivu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kukabiliana na mashambulizi hayo unastahili pongezi.
-
Brigedia Jenerali Hassan Zadeh: Marekani na utawala wa Kizayuni wameshindwa kufikia malengo yao dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
Kamanda wa Kikosi cha Muhammad Rasulullah (s) cha Tehran amesema kuwa kushindwa kwa Marekani na utawala wa Kizayuni kumedhihirisha uwezo mkubwa wa Iran, huku nguvu ya wananchi na utayari wa vikosi vya uhamasishaji ukiifanya Iran kuwa miongoni mwa nguvu kuu katika eneo na duniani.
-
Mhadhiri wa Sala ya Ijumaa Tehran: Makombora na Diplomasia Vimeimarisha Mizani ya Nguvu kwa Manufaa ya Iran
Mhadhiri / Khatibu wa Sala ya Ijumaa mjini Tehran amesema uwezo wa makombora ya Iran pamoja na diplomasia madhubuti ndivyo vilivyoimarisha mizani ya nguvu kwa manufaa ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, huku akisisitiza umuhimu wa kulinda mshikamano wa kitaifa na kuimarisha imani ya wananchi.
-
Radiamali ya Al-Wefaq kwa Mawasiliano ya Mfalme wa Bahrain na Rais wa utawala wa Kizayuni: Ushirikiano na Tel Aviv hauleti usalama
Jumuiya ya Al-Wefaq: Mawasiliano ya Mfalme wa Bahrain na Rais wa utawala wa Kizayuni yanakwenda kinyume na maslahi ya taifa Jumuiya ya Al-Wefaq imelaani vikali mawasiliano ya simu kati ya Mfalme wa Bahrain na Rais wa utawala wa Kizayuni, ikieleza kuwa hatua hiyo ni kujitenga na msimamo wa pamoja wa kitaifa na wa wananchi wa Bahrain. Katika taarifa yake, Al-Wefaq imesema kuwa kitendo hicho kinaonyesha utegemezi wa serikali ya Bahrain kwa ajenda za Marekani na utawala wa Kizayuni, na kwamba hakilingani na matakwa ya wananchi wala maslahi ya taifa. Aidha, jumuiya hiyo imeeleza kuwa hatua hiyo ni kinyume na maslahi na usalama wa Bahrain, ulimwengu wa Kiarabu na Umma wa Kiislamu, ikisisitiza kuwa kuimarisha uhusiano na utawala wa Kizayuni hakutaleta amani wala utulivu katika eneo, bali kutaongeza migogoro na kuhatarisha usalama wa kikanda.
-
Mkuu wa Mahakama ya Iran: Wahusika wa Uhalifu wa Kivita Dhidi ya Watu wa Iran Lazima Waadhibiwe
Mkuu wa Mamlaka ya Mahakama ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Marekani na utawala wa Kizayuni zimetenda uhalifu wa kivita dhidi ya Iran na wananchi wake, akisisitiza kuwa wahusika watafuatiliwa kisheria, wataadhibiwa na kulipa fidia inayostahili.
-
Qalibaf: Masharti ya Mazungumzo ya Dhati ni Kuwa Tayari Kikamilifu kwa Vita
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema kuwa Marekani na utawala wa Kizayuni wamelazimika kutambua nafasi ya washirika wa Iran katika mhimili wa muqawama, akisisitiza kuwa mazungumzo ya kweli hayawezi kufanikiwa bila kuwa na utayari kamili wa kukabiliana na vita.
-
Kaimu Waziri wa Ulinzi wa Iran: Nchi za Kiislamu Lazima Zizuie Israel Kuchochea Mvutano Mashariki ya Kati
Waziri wa Ulinzi wa Iran (akikaimu), Brigedia Jenerali Majid Ibn al-Ridha, amesisitiza umuhimu wa kuanzishwa kwa mfumo wa pamoja wa kiusalama kati ya nchi za Kiislamu ili kuzuia utawala wa Israel kuchochea mivutano katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Qalibaf: Kulipiza kisasi kwa Kiongozi wa Mapinduzi ni kuwaweka huru Waislamu kutoka katika dhulma za Marekani na utawala wa Kizayuni
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema kuwa njia ya kuenzi urithi wa Kiongozi Shahidi wa Umma wa Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, ni kuendelea kuiunga mkono Kambi ya Muqawama, hususan Lebanon, na kupambana na ubeberu wa Marekani na utawala wa Kizayuni.
-
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi la Iran Latangaza Kufungwa kwa Mlango wa Bahari wa Hormuz
Jeshi la Wanamaji la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC Navy) limetangaza kuwa Mlango wa Bahari wa Hormuz umefungwa kwa meli zote na kuonya kuwa chombo chochote kitakachoukaribia kitakuwa kinahatarisha usalama wake.
-
Qalibaf: Vikosi vya Israel Vinapaswa Kujiondoa Kusini mwa Lebanon
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesisitiza kuwa vikosi vya Israel vinapaswa kujiondoa kusini mwa Lebanon ili wananchi warejee makwao kwa heshima, huku Spika wa Bunge la Lebanon, Nabih Berri, akiishukuru Iran kwa mchango wake katika juhudi za kusitisha vita.
-
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya (S) Yaionya Israel: Mashambulizi dhidi ya Lebanon Yakendelea, Iran Itajibu kwa Nguvu
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya (S) yameionya Israel kwamba ikiwa itaendelea na mashambulizi dhidi ya kusini mwa Lebanon na kukiuka makubaliano ya usitishaji mapigano, itakabiliwa na jibu kali kutoka kwa Vikosi vya Wanajeshi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Iran: "Vitendo vya Israel Vimegeuka Fursa ya Kuimarisha Mhimili wa Muqawama"
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema vitendo vya Israel havikuvuruga maslahi ya Iran na Lebanon, bali vimeimarisha mshikamano na kuongeza nguvu za Mhimili wa Muqawama katika kukabiliana na Israel.
-
Qalibaf: Muqawama wa Lebanon na Diplomasia ya Iran Vinahakikisha Uhuru na Uadilifu wa Ardhi ya Lebanon
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema jihadi ya Muqawama wa Kiislamu nchini Lebanon pamoja na diplomasia madhubuti ya Iran vinahakikisha mamlaka na uadilifu wa ardhi ya Lebanon, akisisitiza kuwa maadui hawataweza kamwe kuitenga au kuisambaratisha nguzo yoyote ya Muqawama.
-
Gazeti la Kizayuni: Israel Yakabiliwa na Wimbi Lisilo la Kawaida la Vikwazo vya Kimataifa
Gazeti la Yedioth Ahronoth limesema utawala wa Kizayuni wa Israel umekumbwa na ongezeko kubwa la vikwazo na shinikizo la kimataifa tangu Oktoba 2023, huku baadhi ya viongozi wake wakikabiliwa na hati za kukamatwa na marufuku ya kuingia katika nchi mbalimbali.
-
Waziri wa Utamaduni wa Iran: Mshikamano kati ya Iran na Lebanon ni Hitaji la Kimkakati la Kujilinda
Waziri wa Utamaduni na Mwongozo wa Kiislamu wa Iran amesema kuwa Iran na Lebanon wanakabiliwa na adui mmoja wa pamoja, na kwamba kuimarisha mshikamano kati ya mataifa hayo mawili si suala la hisia za kibinadamu pekee, bali ni hitaji la kimkakati katika kujilinda dhidi ya vitisho vya pamoja.
-
Shirika la Ushirikiano la Shanghai Latangaza Msimamo wa Kuliunga Mkono Iran Dhidi ya Uvamizi wa Kizayuni na Marekani
🔹 Waziri wa Mambo ya Ndani wa Iran, Eskandar Momeni, amesema kuwa nchi zote wanachama wa Shirika la Ushirikiano la Shanghai, hususan China na Russia, zimeonyesha kuunga mkono Iran katika kukabiliana na kile kinachoitwa uvamizi wa Kizayuni na Marekani, huku zikichukua misimamo chanya kuhusu suala hilo.
-
Qalibaf: Marekani Italazimika Kubeba Gharama ya Uhalifu wa Utawala wa Kizayuni nchini Lebanon
Kwa Mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) – ABNA – Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, ametoa onyo kali kwa Marekani kufuatia mashambulizi makali yanayoendelea kufanywa na utawala wa Kizayuni nchini Lebanon, akisema kuwa Washington italazimika kubeba gharama ya uhalifu huo. Kwa mujibu wa Shirika la Habari la IRNA, Qalibaf aliandika katika ukurasa wake kwenye mtandao wa X siku ya Jumatatu kwamba kuzingirwa kwa njia za baharini na kuongezeka kwa vitendo vinavyotajwa kuwa uhalifu wa kivita dhidi ya wananchi wa Lebanon ni ushahidi wa wazi kwamba Marekani haijaheshimu makubaliano ya kusitisha mapigano. Spika huyo wa Bunge la Iran alisisitiza kuwa kila hatua inayochukuliwa katika medani ya kisiasa na kijeshi ina gharama zake, akionya kuwa wale wanaounga mkono au kufumbia macho mashambulizi hayo hawataepuka kuwajibika kwa matokeo yake. Qalibaf aliongeza kuwa kuendelea kwa mashambulizi dhidi ya Lebanon kunathibitisha ushiriki wa Marekani katika kutoa uungaji mkono wa kisiasa na kijeshi kwa utawala wa Kizayuni, jambo ambalo, kwa mujibu wake, linachangia kuongezeka kwa mzozo na mateso ya raia wasio na hatia. Kauli hiyo imekuja wakati mashambulizi ya Israel dhidi ya maeneo mbalimbali ya Lebanon yakiendelea kuzua wasiwasi mkubwa wa kimataifa kuhusu usalama wa raia na hatari ya kupanuka kwa mzozo katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Iran Yapendekeza Mfumo Mpya wa Usalama wa Kikanda katika Mkutano wa BRICS Moscow
Naibu Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran, Ali Bagheri, amesema pendekezo la Iran la kuanzisha mfumo mpya wa usalama katika eneo limepokelewa vyema katika mkutano wa kimataifa wa viongozi wa usalama wa BRICS uliofanyika Moscow, huku akisisitiza umuhimu wa kuondoa ushawishi wa Marekani na utawala wa Kizayuni katika eneo.
-
Jumuiya ya Kiislamu Bangladesh: Waislamu Bilioni Mbili Wako Pamoja na Iran kwa Roho na Mali
Jumuiya ya Kiislamu ya Bangladesh imetoa tamko rasmi ikitangaza uungaji mkono wake kamili kwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, na kuonya kuwa shambulio lolote la kijeshi dhidi ya Iran litakabiliwa na mwitikio mpana wa Waislamu duniani. Katika tamko hilo imesema: “Ingawa viongozi wa baadhi ya nchi za Kiislamu wanategemea Marekani na Israel, lakini Waislamu bilioni mbili duniani wamesimama pamoja na Palestina. Ikiwa uvamizi wa kijeshi utafanywa dhidi ya Iran, Waislamu kote duniani wataingia uwanjani kwa mali na nafsi zao; na kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, utawala ghasibu wa Kizayuni wa Israel utaanguka hivi karibuni.”
-
Makubaliano ya Al-Julani na Wazayuni chini ya kivuli cha Washington
Pendekezo jipya la Washington la Ushirikiano wa Kijamii Kati ya Syria na Utawala wa Kizayuni. Pendekezo jipya la Marekani la ushirikiano wa usalama kati ya Syria na utawala wa Israel linaonekana kama hatua mpya kuelekea kuhalalisha na kudumisha ukoloni, likifanyika chini ya usimamizi wa moja kwa moja wa Marekani.
-
Makamu wa Rais wa Baraza Kuu la Waishe Shia wa Lebanon: Msitoe hata nafasi wala marupurupu kwa adui Mzayuni
Sheikh Ali Al-Khatib, Rais wa Baraza Kuu la Kiislamu la Mashia wa Lebanon, ameitaka serikali isitoe marupurupu ya kihalisi au kisiasa bila malipo kwa adui wa Kizayuni.
-
Katika siku ya mwisho ya likizo ya Hanuka kilichotokea ni;
Walowezi wa Kizayuni kuuvamia Msikiti wa Al-Aqsa
Walowezi wa Kizayuni leo asubuhi, siku ya Jumatatu, kwa ulinzi na msaada wa majeshi ya uvamizi wa Israel, waliuvamia ua wa Msikiti wa Al-Aqsa.
-
Kuanzia Ulaya hadi Marekani; wimbi jipya na lililopangwa la kudhalilisha Qur’ani chini ya kivuli cha uliberali wa Magharibi
Tukio la kuhujumiwa na kudhalilishwa Qur’an Tukufu huko Stockholm, pamoja na mlolongo wa matusi na dharau zilizotokea Ulaya na Marekani, linafichua uhalisia ambao ndani yake chuki dhidi ya Uislamu imegeuzwa kuwa chombo cha kisiasa mikononi mwa mikondo ya mrengo wa kulia uliokithiri na washirika wao wa Kizayuni.
-
Kufichuliwa kwa muundo wa siri wa utawala wa Kizayuni kwa ajili ya kukwepa uwajibikaji / Haki iko chini ya upanga wa fedha na nguvu ya utawala
Tovuti ya Kifaransa Mediapart, kwa ushirikiano na vyombo vingine nane vya habari vya Ulaya, kupitia mradi unaoitwa “Faili za Utawala wa Kizayuni”, imefichua kuundwa kwa kitengo cha siri ndani ya Wizara ya Sheria ya utawala huo.
-
Sheikh Naim Qassem:
Lebanon inapaswa kukabiliana kikamilifu na uvamizi wa kibeberu wa utawala wa Kizayuni | Mashahidi walijitolea kwa roho, mali na kila walichokuwa nacho
Lebanon inakabiliwa na uvamizi hatari wa Kizayuni: Akirejea mashambulizi ya mara kwa mara ya Israel kusini mwa Lebanon, alisema: “Lebanon inakabiliwa na uvamizi wa hatari na wa kupanua mipaka wa utawala wa Kizayuni. Lazima tukabiliane nao kwa kila njia na mbinu. Adui huyu haheshimu makubaliano yoyote.”
-
Umoja wa Waislamu na kuunga mkono Iran kama mstari wa mbele wa kulinda Quds ni jambo la lazima
Mwanafikra mashuhuri wa Algeria amesisitiza kuwa umoja wa Waislamu, kuacha misimamo ya chuki za kimadhehebu na kuunga mkono Iran kama ngome ya mbele ya kulinda Quds (Msikiti wa Al-Aqsa) na Umma wa Kiislamu ni jambo la lazima, na kwamba mataifa pamoja na wanazuoni wa Kiislamu wanapaswa kusimama bega kwa bega na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika nyanja za vyombo vya habari, siasa, utamaduni na usalama.
-
“Barna”, mgombea madhubuti wa kuchukua nafasi ya Benjamin Netanyahu
Kwa mujibu wa madai ya tovuti moja ya Kizayuni, vyanzo vya kisiasa nchini Israel vinamtaja David Barna, mkuu wa Mossad, kama mmoja wa wagombea wakuu wa kumrithi Benjamin Netanyahu.
-
Mgogoro usio wa kawaida katika Jeshi la Israel / Kupungua kwa kasi kwa hamasa ya wanajeshi kuendelea na utumishi
Jeshi la utawala wa Kizayuni linakabiliwa na mgogoro usio wa kawaida wa upungufu wa askari na kushuka kwa kiwango kikubwa cha hamasa ya wanajeshi kuendelea na utumishi.