Kizayuni
-
Mkuu wa Mahakama ya Iran: Wahusika wa Uhalifu wa Kivita Dhidi ya Watu wa Iran Lazima Waadhibiwe
Mkuu wa Mamlaka ya Mahakama ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Marekani na utawala wa Kizayuni zimetenda uhalifu wa kivita dhidi ya Iran na wananchi wake, akisisitiza kuwa wahusika watafuatiliwa kisheria, wataadhibiwa na kulipa fidia inayostahili.
-
Qalibaf: Masharti ya Mazungumzo ya Dhati ni Kuwa Tayari Kikamilifu kwa Vita
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema kuwa Marekani na utawala wa Kizayuni wamelazimika kutambua nafasi ya washirika wa Iran katika mhimili wa muqawama, akisisitiza kuwa mazungumzo ya kweli hayawezi kufanikiwa bila kuwa na utayari kamili wa kukabiliana na vita.
-
Kaimu Waziri wa Ulinzi wa Iran: Nchi za Kiislamu Lazima Zizuie Israel Kuchochea Mvutano Mashariki ya Kati
Waziri wa Ulinzi wa Iran (akikaimu), Brigedia Jenerali Majid Ibn al-Ridha, amesisitiza umuhimu wa kuanzishwa kwa mfumo wa pamoja wa kiusalama kati ya nchi za Kiislamu ili kuzuia utawala wa Israel kuchochea mivutano katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Qalibaf: Kulipiza kisasi kwa Kiongozi wa Mapinduzi ni kuwaweka huru Waislamu kutoka katika dhulma za Marekani na utawala wa Kizayuni
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema kuwa njia ya kuenzi urithi wa Kiongozi Shahidi wa Umma wa Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, ni kuendelea kuiunga mkono Kambi ya Muqawama, hususan Lebanon, na kupambana na ubeberu wa Marekani na utawala wa Kizayuni.
-
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi la Iran Latangaza Kufungwa kwa Mlango wa Bahari wa Hormuz
Jeshi la Wanamaji la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC Navy) limetangaza kuwa Mlango wa Bahari wa Hormuz umefungwa kwa meli zote na kuonya kuwa chombo chochote kitakachoukaribia kitakuwa kinahatarisha usalama wake.
-
Qalibaf: Vikosi vya Israel Vinapaswa Kujiondoa Kusini mwa Lebanon
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesisitiza kuwa vikosi vya Israel vinapaswa kujiondoa kusini mwa Lebanon ili wananchi warejee makwao kwa heshima, huku Spika wa Bunge la Lebanon, Nabih Berri, akiishukuru Iran kwa mchango wake katika juhudi za kusitisha vita.
-
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya (S) Yaionya Israel: Mashambulizi dhidi ya Lebanon Yakendelea, Iran Itajibu kwa Nguvu
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya (S) yameionya Israel kwamba ikiwa itaendelea na mashambulizi dhidi ya kusini mwa Lebanon na kukiuka makubaliano ya usitishaji mapigano, itakabiliwa na jibu kali kutoka kwa Vikosi vya Wanajeshi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Iran: "Vitendo vya Israel Vimegeuka Fursa ya Kuimarisha Mhimili wa Muqawama"
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema vitendo vya Israel havikuvuruga maslahi ya Iran na Lebanon, bali vimeimarisha mshikamano na kuongeza nguvu za Mhimili wa Muqawama katika kukabiliana na Israel.
-
Qalibaf: Muqawama wa Lebanon na Diplomasia ya Iran Vinahakikisha Uhuru na Uadilifu wa Ardhi ya Lebanon
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema jihadi ya Muqawama wa Kiislamu nchini Lebanon pamoja na diplomasia madhubuti ya Iran vinahakikisha mamlaka na uadilifu wa ardhi ya Lebanon, akisisitiza kuwa maadui hawataweza kamwe kuitenga au kuisambaratisha nguzo yoyote ya Muqawama.
-
Gazeti la Kizayuni: Israel Yakabiliwa na Wimbi Lisilo la Kawaida la Vikwazo vya Kimataifa
Gazeti la Yedioth Ahronoth limesema utawala wa Kizayuni wa Israel umekumbwa na ongezeko kubwa la vikwazo na shinikizo la kimataifa tangu Oktoba 2023, huku baadhi ya viongozi wake wakikabiliwa na hati za kukamatwa na marufuku ya kuingia katika nchi mbalimbali.
-
Waziri wa Utamaduni wa Iran: Mshikamano kati ya Iran na Lebanon ni Hitaji la Kimkakati la Kujilinda
Waziri wa Utamaduni na Mwongozo wa Kiislamu wa Iran amesema kuwa Iran na Lebanon wanakabiliwa na adui mmoja wa pamoja, na kwamba kuimarisha mshikamano kati ya mataifa hayo mawili si suala la hisia za kibinadamu pekee, bali ni hitaji la kimkakati katika kujilinda dhidi ya vitisho vya pamoja.
-
Shirika la Ushirikiano la Shanghai Latangaza Msimamo wa Kuliunga Mkono Iran Dhidi ya Uvamizi wa Kizayuni na Marekani
🔹 Waziri wa Mambo ya Ndani wa Iran, Eskandar Momeni, amesema kuwa nchi zote wanachama wa Shirika la Ushirikiano la Shanghai, hususan China na Russia, zimeonyesha kuunga mkono Iran katika kukabiliana na kile kinachoitwa uvamizi wa Kizayuni na Marekani, huku zikichukua misimamo chanya kuhusu suala hilo.
-
Qalibaf: Marekani Italazimika Kubeba Gharama ya Uhalifu wa Utawala wa Kizayuni nchini Lebanon
Kwa Mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) – ABNA – Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, ametoa onyo kali kwa Marekani kufuatia mashambulizi makali yanayoendelea kufanywa na utawala wa Kizayuni nchini Lebanon, akisema kuwa Washington italazimika kubeba gharama ya uhalifu huo. Kwa mujibu wa Shirika la Habari la IRNA, Qalibaf aliandika katika ukurasa wake kwenye mtandao wa X siku ya Jumatatu kwamba kuzingirwa kwa njia za baharini na kuongezeka kwa vitendo vinavyotajwa kuwa uhalifu wa kivita dhidi ya wananchi wa Lebanon ni ushahidi wa wazi kwamba Marekani haijaheshimu makubaliano ya kusitisha mapigano. Spika huyo wa Bunge la Iran alisisitiza kuwa kila hatua inayochukuliwa katika medani ya kisiasa na kijeshi ina gharama zake, akionya kuwa wale wanaounga mkono au kufumbia macho mashambulizi hayo hawataepuka kuwajibika kwa matokeo yake. Qalibaf aliongeza kuwa kuendelea kwa mashambulizi dhidi ya Lebanon kunathibitisha ushiriki wa Marekani katika kutoa uungaji mkono wa kisiasa na kijeshi kwa utawala wa Kizayuni, jambo ambalo, kwa mujibu wake, linachangia kuongezeka kwa mzozo na mateso ya raia wasio na hatia. Kauli hiyo imekuja wakati mashambulizi ya Israel dhidi ya maeneo mbalimbali ya Lebanon yakiendelea kuzua wasiwasi mkubwa wa kimataifa kuhusu usalama wa raia na hatari ya kupanuka kwa mzozo katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Iran Yapendekeza Mfumo Mpya wa Usalama wa Kikanda katika Mkutano wa BRICS Moscow
Naibu Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran, Ali Bagheri, amesema pendekezo la Iran la kuanzisha mfumo mpya wa usalama katika eneo limepokelewa vyema katika mkutano wa kimataifa wa viongozi wa usalama wa BRICS uliofanyika Moscow, huku akisisitiza umuhimu wa kuondoa ushawishi wa Marekani na utawala wa Kizayuni katika eneo.
-
Jumuiya ya Kiislamu Bangladesh: Waislamu Bilioni Mbili Wako Pamoja na Iran kwa Roho na Mali
Jumuiya ya Kiislamu ya Bangladesh imetoa tamko rasmi ikitangaza uungaji mkono wake kamili kwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, na kuonya kuwa shambulio lolote la kijeshi dhidi ya Iran litakabiliwa na mwitikio mpana wa Waislamu duniani. Katika tamko hilo imesema: “Ingawa viongozi wa baadhi ya nchi za Kiislamu wanategemea Marekani na Israel, lakini Waislamu bilioni mbili duniani wamesimama pamoja na Palestina. Ikiwa uvamizi wa kijeshi utafanywa dhidi ya Iran, Waislamu kote duniani wataingia uwanjani kwa mali na nafsi zao; na kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, utawala ghasibu wa Kizayuni wa Israel utaanguka hivi karibuni.”
-
Makubaliano ya Al-Julani na Wazayuni chini ya kivuli cha Washington
Pendekezo jipya la Washington la Ushirikiano wa Kijamii Kati ya Syria na Utawala wa Kizayuni. Pendekezo jipya la Marekani la ushirikiano wa usalama kati ya Syria na utawala wa Israel linaonekana kama hatua mpya kuelekea kuhalalisha na kudumisha ukoloni, likifanyika chini ya usimamizi wa moja kwa moja wa Marekani.
-
Makamu wa Rais wa Baraza Kuu la Waishe Shia wa Lebanon: Msitoe hata nafasi wala marupurupu kwa adui Mzayuni
Sheikh Ali Al-Khatib, Rais wa Baraza Kuu la Kiislamu la Mashia wa Lebanon, ameitaka serikali isitoe marupurupu ya kihalisi au kisiasa bila malipo kwa adui wa Kizayuni.
-
Katika siku ya mwisho ya likizo ya Hanuka kilichotokea ni;
Walowezi wa Kizayuni kuuvamia Msikiti wa Al-Aqsa
Walowezi wa Kizayuni leo asubuhi, siku ya Jumatatu, kwa ulinzi na msaada wa majeshi ya uvamizi wa Israel, waliuvamia ua wa Msikiti wa Al-Aqsa.
-
Kuanzia Ulaya hadi Marekani; wimbi jipya na lililopangwa la kudhalilisha Qur’ani chini ya kivuli cha uliberali wa Magharibi
Tukio la kuhujumiwa na kudhalilishwa Qur’an Tukufu huko Stockholm, pamoja na mlolongo wa matusi na dharau zilizotokea Ulaya na Marekani, linafichua uhalisia ambao ndani yake chuki dhidi ya Uislamu imegeuzwa kuwa chombo cha kisiasa mikononi mwa mikondo ya mrengo wa kulia uliokithiri na washirika wao wa Kizayuni.
-
Kufichuliwa kwa muundo wa siri wa utawala wa Kizayuni kwa ajili ya kukwepa uwajibikaji / Haki iko chini ya upanga wa fedha na nguvu ya utawala
Tovuti ya Kifaransa Mediapart, kwa ushirikiano na vyombo vingine nane vya habari vya Ulaya, kupitia mradi unaoitwa “Faili za Utawala wa Kizayuni”, imefichua kuundwa kwa kitengo cha siri ndani ya Wizara ya Sheria ya utawala huo.
-
Sheikh Naim Qassem:
Lebanon inapaswa kukabiliana kikamilifu na uvamizi wa kibeberu wa utawala wa Kizayuni | Mashahidi walijitolea kwa roho, mali na kila walichokuwa nacho
Lebanon inakabiliwa na uvamizi hatari wa Kizayuni: Akirejea mashambulizi ya mara kwa mara ya Israel kusini mwa Lebanon, alisema: “Lebanon inakabiliwa na uvamizi wa hatari na wa kupanua mipaka wa utawala wa Kizayuni. Lazima tukabiliane nao kwa kila njia na mbinu. Adui huyu haheshimu makubaliano yoyote.”
-
Umoja wa Waislamu na kuunga mkono Iran kama mstari wa mbele wa kulinda Quds ni jambo la lazima
Mwanafikra mashuhuri wa Algeria amesisitiza kuwa umoja wa Waislamu, kuacha misimamo ya chuki za kimadhehebu na kuunga mkono Iran kama ngome ya mbele ya kulinda Quds (Msikiti wa Al-Aqsa) na Umma wa Kiislamu ni jambo la lazima, na kwamba mataifa pamoja na wanazuoni wa Kiislamu wanapaswa kusimama bega kwa bega na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika nyanja za vyombo vya habari, siasa, utamaduni na usalama.
-
“Barna”, mgombea madhubuti wa kuchukua nafasi ya Benjamin Netanyahu
Kwa mujibu wa madai ya tovuti moja ya Kizayuni, vyanzo vya kisiasa nchini Israel vinamtaja David Barna, mkuu wa Mossad, kama mmoja wa wagombea wakuu wa kumrithi Benjamin Netanyahu.
-
Mgogoro usio wa kawaida katika Jeshi la Israel / Kupungua kwa kasi kwa hamasa ya wanajeshi kuendelea na utumishi
Jeshi la utawala wa Kizayuni linakabiliwa na mgogoro usio wa kawaida wa upungufu wa askari na kushuka kwa kiwango kikubwa cha hamasa ya wanajeshi kuendelea na utumishi.
-
Kifo cha Kishahidi Klcha Kijana Msyria Usiku wa Harusi Yake Akiwa Anapambana na Uvamizi wa Israel katika Mji wa Bayt Jinn
Kijana mmoja Msyria ameuliwa shahid usiku wa harusi yake wakati akipambana na uvamizi wa jeshi la Israel katika mji wa Bayt Jinn, ulioko katika vitongoji vya kusini mwa Damascus.
-
Hali Zisizo za Kibinadamu Gaza: Janga Linalozidi Kuwa Kubwa na Uhitaji wa Haraka wa Msaada wa Kimataifa / Mauaji ya Kimbari Yanaendelea
Msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu Palestina (Hamas) amesema kuwa mazingira haya mabaya ni matokeo ya kuendelea kwa mzingiro, kuzuia ujenzi upya, uharibifu wa miundombinu na hali mbaya ya hewa. Ameitaka Jumuiya ya Kimataifa, ikiwemo Jumuiya ya Nchi za Kiarabu, OIC na Umoja wa Mataifa, kuchukua hatua za haraka za kutoa makazi na misaada ya kibinadamu.
-
Mwenyekiti wa Chama cha Al-Wafa nchini Lebanon katika mahojiano na ABNA:
Jamii ya kimataifa, haki za binadamu na dhana kama hizi zimelemazwa / “Lugha ya nguvu” ndiyo lugha pekee ambayo Israeli huielewa
Dkt. Alwan alisema: Serikali ya Lebanon, kutokana na mipaka ya diplomasia na kutokuwepo kwa uimarishaji wa kweli wa jeshi (kwa sababu ya vizuizi vya Marekani), kimsingi haiwezi kuilinda nchi kijeshi.
-
Jeshi la Israel Ladai Kumuua Kigaidi Kamanda Mwandamizi wa Hezbollah katika Mji wa Beirut
Kwa mujibu wa kituo cha habari cha Aljazeera, jeshi la Israel limedai kuwa limemuua mmoja wa makamanda wakuu wa Hezbollah katika mji wa Beirut.
-
Jeshi la Mapinduzi la Kiislamu la Iran (IRGC):
Hadithi ya vita vya siku 12 iwe kipaumbele kwa wachapishaji na waandishi
Jeshi la Mapinduzi la Kiislamu (IRGC) limeweka mkazo: Moja ya matukio makuu na yenye mafundisho muhimu katika historia ya kisasa, ambayo inaweza kuwa kipaumbele kwa wachapishaji na waandishi wenye ujuzi na uwezo wa nchi, ni Ulinzi Mtakatifu wa siku 12 dhidi ya vita vya kigaidi vilivyofanywa na muungano wa Marekani, utawala wa Kizayuni, na wafuasi wao wa Magharibi na wa kikanda.
-
Sheikh Ikrimah Sabri, khatibu wa Msikiti wa Al-Aqsa, atafikishwa kwenye mahakama!
Wakili wa Ikrimah Sabri amesema kwamba mashtaka dhidi yake ni sehemu ya “ufuasi wa kisiasa, kidini na kifikra,” na kwamba mamlaka za Kizayuni haziridhiki na misimamo yake ya kidini na kisiasa na wanajitahidi kunyamazisha sauti yake.