Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) – ABNA –, Arubaini ya Imam Hussein (a.s.) inashika nafasi ya kipekee katika mfumo wa fikra wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Imam Sayyid Ali Khamenei.
Kwa mujibu wa makala maalumu ya gazeti la Al-Wefaq, Imam Khamenei anaiona Arubaini ya Imam Hussein (a.s.) kuwa zaidi ya kumbukumbu ya kuuawa shahidi kwa mjukuu wa Mtume Muhammad (s.a.w.w.). Kwa mtazamo wake, Arubaini ni tukio linalobeba ujumbe mpana wa kidini, kijamii, kiutamaduni na kiustaarabu, unaoweza kuimarisha umoja wa Waislamu na kuhuisha maadili ya Uislamu.
Makala hiyo inaeleza kuwa matembezi ya Arubaini ni mfano wa mshikamano wa Umma wa Kiislamu, kujitolea, huduma kwa wengine na kuendeleza utamaduni wa mapambano dhidi ya dhulma, sambamba na kudumisha ujumbe wa milele wa Imam Hussein (a.s.) wa kusimamia haki, uadilifu na heshima ya mwanadamu.
Aidha, katika mtazamo wa Imam Khamenei, Arubaini imekuwa harakati ya kimataifa inayowakusanya mamilioni ya waumini kutoka mataifa mbalimbali, jambo linalodhihirisha nguvu ya imani na nafasi ya mafundisho ya Karbala katika kujenga ustaarabu unaozingatia maadili, udugu na upinzani dhidi ya dhulma.
Kwa msingi huo, Arubaini inaendelea kuwa ishara ya uhai wa ujumbe wa Imam Hussein (a.s.) na darasa endelevu la kusimamisha haki, kulinda dini na kuimarisha mshikamano wa Waislamu duniani.
Maoni yako