Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) –ABNA–, msemaji wa Jeshi la Yemen, Brigedia Jenerali Yahya Saree, ametangaza kuwa vikosi vyao vimefanikiwa kulenga shabaha nyeti ya Saudi Arabia katika Uwanja wa Ndege wa Najran kwa kutumia ndege isiyo na rubani.
Kwa mujibu wa Saree, shambulio hilo lilifikia lengo lake kwa usahihi na lilikuwa ni jibu kwa kile alichodai kuwa ni ukiukaji wa anga la mikoa ya Saada na Hajjah uliofanywa na ndege zisizo na rubani za Saudi Arabia.
Amesisitiza kuwa Jeshi la Yemen halitavumilia ukiukaji wowote wa anga ya nchi hiyo, akionya kwamba hatua yoyote ya aina hiyo itakabiliwa na jibu na hatua za kulipiza kisasi.
Maoni yako